Friday, February 14, 2014

MPANGO KAZI WA VIWAWA PAROKIA YA BOKO 2014


UTANGULIZI
Kwa mwaka 2013, Vijana Parokia ya Boko tulifanikiwa kuyafanikisha matukio yote tuliyokuwa tumejipanga.
Pamoja na ufanisi huo yapo mengi ambayo yalishindwa kufanikiwa kwa asilimia zote na hii nikutokana na hali mbaya ya uchumi kwa Vijana wetu, na chama chetu kwa ujumla.
Kwa Mwaka 2014, Halmashauri ya VIWAWA Parokia imeridhia kupunguza baadhi ya matukio, ili kuweza kuleta ufanisi zaidi.
Kutokana na kutokuwepo kwa mashindo ya Vijana ya Dekania (dekania Cup) na  ya Jimbo (Pengo Cup), Uongozi wa Parokia umeona pia ni vyema kutoa mashindano ya Paroko Cup kwa Msimu huu.
MATUKIO YA MWAKA 2014
1.      Tutakuwa na  Mafungo ya Vijana wote wa Parokia yatakayo fanyika mwanzo wa kipindi cha kwaresima, na Mafungo haya hatafanyikia Mlango wa Imani Bagamoyo. Lengo la mafungo haya ni kuwafanya vijana waweze kuanza kutafakari safari ya Ukombozi wa Mwanadamu kwa Mateso, Kifo na Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo.
2.      Hija ya Vijana jimbo kuu la Dar es salaam itafanyikia Parokia kwetu Juma la nne la kwaresima siku ya Jumamosi.
3.      Siku ya JUMATATU YA PASAKA VIJANA WETU WOTE WA PAROKIA watakutana pamoja kwa ajili ya kusheherekea Ufufuko wake Bwana, hii ikiwa ni pamoja na kushirikishana mambo mbali mbali ya kimaisha.
4.      Mwanzo wa mwezi wa saba tutakuwa na ziara ya UINJILISHAJI JIMBO LA MBULU; Licha ya kwamba mwaka jana tulifanya ziara katika Jimbo hili kwa kutembelea Parokia tatu, bado changamoto za Kiimani ni kubwa sana ambapo sasa jamii ya kule inahitaji elimu zaidi juu ya mambo ya kiimani.
Hivyo kwa mwaka huu tunaenda na ujumbe wa IMANI MSINGI WA KANISA, na kuelimisha kwa kina zaidi juu utume wetu,
Tunatarajia kutembelea Jumla ya parokia nne, kwa ziara hii wenyeji wetu ni Parokia ya Dareda, zaidi ya hayo pia tutapata nafasi ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Ngorongoro
5.      Tamasha la Vijana; huu ni utamaduni wetu wa kila mwaka, tamasha la mwaka huu litafanyika mwezi wa nane na litakuwa na semina, michezo ya ndani ambayo ni Maigizo, Ngoma, Kwaya, Nyimbo, Vichekesho na Show mbali mbali, tamasha hili linatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku mbili(ijumaa jioni hadi Jumapili baada ya Misa).
6.      Kongamano la Ujirani Mwema (Parokia ya Bunju na Boko) halmashauri ya Viwawa Parokia inatarajia kuandaa kongamano la Ujirani mwema kwa Vijana na Viongozi wa Halmashauri ya Walei wa Parokia hizi, Kongamano hili litafanyika mwezi wa kumi na moja.
7.      Mwisho wa mwaka tunatarajia kuwa na semina ya siku moja kwa vijana wote; Lengo ni kuwakumbusha vijana wajibu wao katika kanisa na jamii kwa jumla.
NB: LIPA ADA YA CHAMA KWA MAENDELEO YA CHAMA CHETU, PIA UNAWEZA KULIPIA ADA ZA USHIRIKI YA MATUKIO YOTE YA VIWAWA KWA MWAKA 2014 KATIKA ACCOUNT YETU YA CRDB TAWI LA TEGETA.
ADA KWA MWEZI NI SHS 2000/= NA KWA MWAKA NI TSHS 24,000/= KWA KILA KIJANA.
ADA ZA USHIRIKI WA MATUKIO YOTE YA MWAKA NI TSHS 276,000/=
ACCCOUNT  NAME:VIWAWA PAROKIA YA BOKO
 ACCCOUNT  NO: 01524526820100


RATIBA HII YAWEZA KUBADILIKI KWA SABABU AMBAZO ZITAKUWA NJE YA UWEZO WETU, MATUKIO HAYA YAKIGONGANA NAYA PAROKIA YAKO ONYESHA UTII, FUATA YA PAROKIA.


TAREHE
TUKIO
WAHUSIKA
MAHALI
19/01/2014
MKUTANO MKUU
VIONGOZI WA VIGANGO, KANDA NA JUMUIYA
BOKO
08/03/2014
MAFUNGO
VIJANA WOTE
BAGAMOYO
16/03/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WA VIGANGO
BOKO
29/03/2014
HIJA
VIJANA WOTE
PAROKIANI-BOKO
5-6/04/2014
MAFUNGO
VIONGOZI WA PAROKIA, VIGANGO NA JUMUIYA
CONSOLATA – BUNJU-KIDEKANIA
13/04/2014
MISA YA MATAWI

VIJANA WOTE
DONBOSCO UPANGA
19/04/2014
MATENDO YA HURUMA
VIJANA WOTE
KIJIJI CHA FURAHA MBURAHATI –KIJIMBO
21/04/2014
GET TOGETHER
VIJANA WOTE

01/05/2014
SOMO WA VIWAWA (MT. YOSEPH)
VIJANA WOTE
DONBOSCO –UPANGA-KIJIMBO
11/05/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WA VIGANGO
 RAFAEL
08/06/2014
MKUTANO MKUU
VIONGOZI WA VIGANGO, KANDA NA JUMUIYA
BOKO
28-29/06/2014
KONGAMANO LA VIJANA JIMBO
VIJANA WOTE
SEKONDARI YA LOYOLA
01-07/07/2014
ZIARA YA UINJILISHAJI
VIJANA WOTE
JIMBO LA MBULU
20/07/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WOTE WA VIGANGO
MBWENI
15-17/08/2014
TAMASHA LA VIJANA
VIJANA WOTE
BOKO
23/08/2014
MAFUNGO
VIJANA  WOTE
BAGAMOYO-KIDEKANIA
21/09/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WOTE WA VIGANGO
RAFAEL
01-06/10/2014
KONGAMANO LA VIJANA KITAIFA
VIJANA WOTE
JIMBO LA NJOMBE(KITAIFA)
19/10/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WOTE WA VIGANGO
BOKO
15/11/2014
UJIRANI MWEMA
VIJANA BOKO NA BUNJU
BOKO
06/12/2014
SEMINA
VIJANA WOTE

13/12/2014
SEMINA
VIJANA WOTE
ST. GASPER – MBEZI-KIDEKANIA




18/01/2015
MKUTANO MKUU
VIONGOZI WA PAROKIA, VIGANGO NA JUMUIYA
BOKO








Tuesday, November 12, 2013

Mwaka wa Imani wafungwa Rasmi kitaifa Bagamoyo 10/11/2013





Sikiliza . Tamko la Familia ya Mungu nchini Tanzania likisomwa na Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
.chagua hapa......  RealAudioMP3







Bonyeza hapa kusoma zaidi kuhusu mwaka wa imani................

Monday, November 11, 2013

MABIGWA WA DEKANI YA MT. GASPER - MBEZI BEACH

Baada ya kumalizika kwa mashindano ya Dekania Cup, sasa nguvu zote tumeizihamimishia kwenye Pengo cup, tukiwa tuna wachezaji wengi wenye Vipaji kwenye michezo ya Mpira wa Miguu, Pete na Mpira wa Wavu, ni matumaini yetu tutaleta mshindani mkubwa na kuchukua ubigwa

Mabigwa wa mwaka 2013 - 2014

Mpira wa Miguu
Bigwa ni Parokia ya Gasper
Mshindi wa Pili ni Parokia ya Tegeta
Mshindi wa Tatu ni Parokia Ya Bahari Beach

Mpira wa Pete (Netball)
Bigwa ni Parokia ya Dominiko
Mshindi wa Pili ni Parokia ya Kunduchi
Mshindi wa Tatu ni Parokia Ya Boko

Mpira wa Wavu (Vollyball)
Bigwa ni Parokia ya Domoniko
Mshindi wa Pili ni Parokia ya Bunju





na Abel Reginald Katibu Vijana Dekania

Thursday, November 7, 2013

Masomo ya Dominika 32 jumapili ya tarehe 10/11/2013


click hapa kusikiliza tafakari ya masomo ya kesho. RealAudioMP3

  

10
   NOVEMBER
JUMAPILI DOMINIKA YA 32 MWAKA C



RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI TETA.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI



MASOMO YA DOMINIKA 32
SOMO LA 1: 2Mak. 7:1-2, 9-14

Ilitokea ya kuwa ndugu saba, pamoja na mama yao, walikamatwa kwa amri ya mfalme na kuteswa sana kwa mijeledi na mapigo ili kuwashurutisha kuonja nyama marufuku ya nguruwe. Mmoja akajifanya mnenaji wao, akasema, wataka kuniuliza nini juu yetu? Sisi tu tayari kufa kuliko kuzivunja amri za wazee wetu. Wa pili alipokuwa kufani alisema,wewe, mdhalimu, unatufarikisha na maisha ya sasa, lakini Mungu wa ulimwengu atatufufua sisi tuliokufa kwa ajili ya amri zake, hata tupate uzima wa milele. Na baada yake alidhihakiwa Yule wa tatu, naye mara alipoagizwa, alitoa ulimi wake, akanyosha mikono yake bila hofu akasema kwa ushujaa, kutoka mbinguni nalipewa hivi, na kwa ajili ya amri za Mungu navihesabu kuwa si kitu, na kwake natumaini kuvipokea tena. Hata mfalme na watu wake walishangazwa kwa roho ya kijana huyu, kwa jinsi alivyoyadharau  maumivu yake. Akiisha kufa huyu, walimtesa wa nne na kumtenda mabaya yale yale. Naye alipokaribia kufa alisema hivi; ni vema kufa kwa kwa mikono ya mwanadamu na kuzitazamia ahadi zitokazo kwa Mungu, kuwa tutafufuliwa naye. Lakini kwako wewe hakuna ufufuo.


Somo 2: 2The.2:16 – 3:1-5

Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupatia faraja ya milelena tumaini jema, katika neema, awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neon na tendo jema. Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neon la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu; tukaokolewena watu wasio haki; wabaya; maana si wote walio na imani. Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na Yule mwovu. Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba unayafanya tuliyowaagiza, tena kwamba mtayafanya. Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na saburi ya Kristo.


INJILI:Lk. 20:27-38

Baadhi ya wasadukayo, wale wasemayo ya kwamba hakuna ufufuo, walimwendea Yesu, wakamwuliza, wakisema Mwalimu, Musa alituandikia ya kuwa, mtu akifiwa na ndugu yake mwenye mke, lakini hana mtoto, na amtwae huyo mke,  ampatie ndugu yake mzao. Basi,kulikuwa na ndugu saba . na wa kwanza alioa mke, akafa hana mtoto; wa pili akamtwaa Yule mke, akafa hana mtoto; hata wa tatu akamwoa, na kadhalika wote saba, wakafa, wasiache watoto. Mwisho akafa Yule mke naye. Basi, katika ufufuo atakuwa mke wa yupi? Maana aliolewa na wote saba. Yesu akawaambia, wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa; lakini, wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kafufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, wala hawawezi kufa tena; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kwa vile walivyo wana wa ufufuo. Lakini, ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.


Matangazo mbali mbali
Jumapili hii tarehe 10/11/13 kutakuwa na kikao cha Halmashauri ya Viwawa Parokia ya Boko, kikao kitafanyikia parokiani Saa 4:00 asubuhi mara baada ya ibada ya pili. Wajumbe ni viongozi wote wa Viwawa ngazi ya Vigango.
Agenda za kikao.
ü Maandalizi ya semina ya Tarehe 23/11/13 – Mbweni
ü Mapendekezo ya mipango ya mwaka 2014 – 2015
ü mengineyoendelea zaidi......

jdhibitisha ushiriki wako kwenye semina ya tarehe 23/11/13 kwa kulipa ada sasa ni tshng 5000 lipa kwa mhazini wako jumuiya, kigango au parokia.....tunawatakia maandalizi mema.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR