Friday, November 28, 2014

YALIYOJIRI BUNGENI DODOMA LEO, MBUNGE ATINGA NA BANGO KUWANIA NAFASI, AAMRIWA ASAUla

Mbunge wa Mwibara Mhe.Kange Lugola  akiomba kura za kuwania nafasi ya Mjumbe  wa Tume ya Utumishi Bungeni kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo Juni 11, 2014.   Mbunge wa Mwibara Mhe.Kange Lugola akivua bango alilokuwa ameva wakati akiomba kura kwa wabunge


MATUKIO KATIKA PICHA LEO ASUBUHI BUNGENI DODOMA

1
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Tundu Lissu akiwasili leo

Wednesday, November 26, 2014

PICHA, JINSI SITTA ALIVYOWATULIZA WAPINZANI KUHUSU UFISADI WA ESROW,

Mwenyekiti wa Bunge, Mh. Mussa Azan Zungu akiongozwa na Mpambe wa Bunge kutoka kwenye ukumbi wa Bunge wakati alipositisha kikao cha Bunge cha asubuhi leo Novemba 26, 2014.
Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda akizugumza na Mbunge wa Viti Maalum Rachel Mashishanga kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma leo Novemba 26, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki na Mbunge wa Urambo, Mh. Samuel Sitta (katikati) akiwatuliza  na baadhi ya wabunge wa Upinzani, Bungeni mjini Dodoma leo Novemba 26, 2014

Tumeuanza Mwaka wa Watawa Duniani, 2014 - 2016


Makanisa mahalia sehemu mbali mbali za dunia, yataadhimisha Ibada ya Misa na kufanya mikesha ya sala na tafakari kama sehemu ya mchakato wa uzinduzi wa Mwaka wa Watawa Duniani, uliotangazwa na Baba Mtakatifu Francisko. Waamini wanaalikwa kusali na kumwomba Roho Mtakatifu ili aweze kulikirimia Kanisa neema na baraka ili kujenga na kulipyaisha Kanisa katika maisha na utume wake
Maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani yanakwenda sanjari na Jubilee ya miaka 50 tangu Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican walipochapisha Waraka kuhusu Fumbo la Kanisa, Lumen Gentium, inayojulikana kama Mwanga wa Mataifa, Kanisa kama Fumbo la Mwili wa Kristo; linaloonekana na lile lisiloonekana; umuhimu wa Taifa la Mungu katika kushiriki katika maisha na utume wa Kanissa pamoja na kukuza ari na moyo wa kimissionari.

Mama Kanisa pia anaadhimisha Jubilee ya miaka 5o tangu Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican walipotoa Tamko kuhusiana na Maisha ya Kitawa: Perfect Caritatis, yaani Upendo Mkamilifu, Waraka uliowataka Watawa kupyaisha maisha yao, kwa kutoa nafasi ya kwanza katika maisha ya kiroho, mashauri ya Kiinjili, maisha ya kijumuiya pamoja na malezi makini kwa wale wote wanaotaka kujisadaka kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake.

Haya ni matukio makuu yatakayoliwezesha Kanisa kufanya tafakari ya kina katika maisha na utume wa Watawa sehemu mbali mbali za dunia. Mwaka wa Watawa Duniani unazinduliwa rasmi, Jumamosi jioni tarehe 29 Novemba 2014 kwenye Kanisa kuu la Bikira Maria Makuu, lililoko mjini Roma kwa Ibada na Mkesha wa Sala, kuanzia saa 1:00 Usiku. Tarehe 30 Novemba, 2014, Jumapili ya kwanza ya Kipindi cha Majilio, kutafanyika Ibada ya Misa Takatifu kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, kuanzia saa 4:00 asubuhi kwa saa za Ulaya.

Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume linasema kwamba, matukio haya ni muhimu sana katika uzinduzi wa Mwaka wa Watawa Duniani, kwa kujiweka chini ya ulinzi na usimamizi wa Bikira Maria, Mama wa Mungu na msimamizi wa maisha ya kitawa. Hiki ni kipindi cha matumaini, sala na tafakari ya kina kuhusu matendo makuu ya Mungu katika maisha ya Watawa wanaoendelea kujisadaka kwa ajili ya Mungu na jirani zao, kwa kutambua kwamba, imani ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ambayo Watawa wanapenda kuwamegea na kuwashirikisha wengine.

Ninyi Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina Langu......

Nifuraha kwetu Kuona yale tunayofanya yana sifa na Utukufu kwa Mungu, tokea 2011 hadi leo 2014 utume wetu upo na unazidi kuimara, tunawashukuru sana Walezi wetu na Wadau wetu wote kwa michango yao mbali mbali, hapo juu vijana wa wa parokia ya Boko wakiwa na Paroko wa Parokia ya Kigenge Chini Jimbo kuu la Arusha


Askofu Nzigirwa akiongoza Ibada ya Matawi Don Bosco, ikiwa ni siku pia ya Azimisho la Vijana Ulimwenguni ilikuwa mwaka 2012.


Mwenyekiti wa Kigango cha Mt. Rafael, Baada ya Semina ya Siku Moja iliyofanyika katika Kijiji cha Furaha Mbweni mwaka 2011

Baadhi ya Vijana wa Kigango cha Bunju, kwa sasa Parokia ya Bunju wakiburudisha kwenye Sherehe ya Pentekoste ilikuwa mwaka 2012.


















Monday, November 24, 2014

Changamkieni Uinjilishaji wa kina kwa furaha na unyofu wa moyo Ungana nasi tena 2015, Kiabakari - Musoma.


Askofu Beatus Kinyaia wa Jimbo la Mbulu

Beatus Kinyaia ateuliwa kuwa Askofu Mkuu wa jimbo kuu Katoliki la Dodoma.

Hatimaye leo baba Mtakatifu Papa Francisco amempandisha kutoka  askofu hadi kuwa askofu Mkuu askofu Beatus Kinyaiya, O.F.M. Cap (pichani) wa jimbo kuu Katoliki la Dodoma.


Askofu Beatus Kinyaiya alizaliwa Mei 9, 1957. Akapata daraja takatifu la Upadre katika shirika la Kimisionari la Wafranciscan Minor  tarehe 25 juni, 1989.


Aliteuliwa kuwa askofu wa jimbo Katoliki la Mbulu tarehe 22 Aprili, 2006, nakusimikwa/ wekwa wakfu rasmi na Kardinali Polycarp Pengo  kuwa askofu wa jimbo la Mbulu tarehe 2 Julai 2006.


Leo tarehe 06 Novemba, 2014 ameteuliwa kuwa askofu Mkuu wa Jimbo Kuu katoliki la Dodoma ambalo nalo limepandishwa hadhi na kuwa jimbo kuu.

Atasimikwa rasmi kuanza utume wake huo mpya katika jimbo hilo mwezi wa Januari, 2015.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR