Thursday, December 25, 2014

alhamisi 25/12/2014 mosomo ya sherehe ya kuzaliwa bwana noel

Alhamisi, 25 Desemba 2014
Sherehe ya Kuzaliwa Bwana (Noeli)

Isa 52: 7-10;
Zab 97: 1-6;
Ebr 1:1-6;
Yn 1: 1-18

NENO lilinenwa; Mungu asiyefahamika alilifanya lifahamike, furahini!

Leo Kanisa pamoja na viumbe vyote vyajawa na furaha kwani vimefanywa upya na kuwa kiumbe kipya kwa njia ya kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. “Neno” basi na uwe mwanga (Mwa. 1:3), lililoleta uumbaji sasa limeongelewa tena, kupitia kuzaliwa kwa Bwana wetu na Mkombozi wetu. Mwanga (Yn. 1:8), sasa anang’ara katika giza. Mwanga, atoaye mwanga kwa kila mtu amekuja ulimwenguni. Mungu asiyefahamika, sasa amefanywa afahamike, Baba sasa anajidhihirisha mwenyewe, kupitia mwanae wa kiume, Yesu. Neno alifanyika mwili na akakaa kwetu.

Umwilisho au Noeli ni sherehekeo la furaha hii – Mungu wetu anakuwa mwili na anakuja kukaa ndani yetu wanadamu. Tukio hili lilikuwa kubwa sana kiasi cha dunia ya Magharibi kiutamaduni imefanya karne yake katika vipindi viwili vya nyakati kwa mwaka wa kuzaliwa kwake: BC (Kabla ya Kristo) and AD (Anno Domini,kutoka kilatini ni katika Mwaka wa Bwana). Tukio hili liliufanya ulimwengu ufurahi , malaika walifurahi kwa Utukufu kwa Mungu, waliomba kwaajili ya amani duniani kwa watu. Ingawa ukaribisho wa Bwana Yesu haukuwa wa furaha sana ulimwenguni. Mkombozi hakuwa na nafasi ya kuzaliwa, bali katika uhakika, katika moja ya vijiji vidogo Bethlehemu. Hakuwa na tafrija ya ukaribisho, isipokuwa tu kwa baadhi ya wanyama katika hali ya ukimya na baadae wachungaji wachache waliomuabudu Yeye. Mfalme Herode alimchukulia mtoto kuwa kama ni tishio, alitaka mtoto Yesu auwawe. Katika miaka ya mbeleni, mkombozi wetu alikanwa, alivamiwa na kusurubiwa. Na kwa hayo yote aliyoyapokea, mkombozi pekee alirudisha huruma, huruma na upendo. Leo, Yesu amezaliwa kati yetu tena, katika hali yetu ya kumkana na hali ya dhambi; Yeye amezaliwa Bethrehemu ya hali ya ubinafsi, umimi, mateso, vita, unyonyaji, nakadharika. Je, sisi tupo kama wachungaji, waliokwenda kwa Yesu na kuzitoa heshima zao au tupo kama Herode, aliyemchukua Yesu kuwa kama ni tishio la uhuru wetu, katika hangaiko la kutafuta starehe? Je, tunakwenda kufurahi pamoja na wachungaji au kupanga mabaya kama Herode?

Katika milongo miwili iliyopita, dunia yetu imekuwa nzuri sana kwa wanadamu pamoja na uwepo wa kimungu wa Mungu mwenyewe. Ndani yake pia, wengi wametamani kuwa katika giza. Leo Yesu anahitaji azaliwe ndani yetu, awe Neno linenwalo, mwanga unaoondoa giza lote. Je, tupo tayali kujitoa wenyewe kwake Yeye? Je, tupo tayali kuufahamu mwanga huo? Je, tupo tayali kuupokea upendo wake?

Sala: Bwana Yesu, nakuhitaji Wewe uzaliwe ndani yangu leo, Nakuhitaji Wewe unijaze kwa mwanga Wako na kuondoa giza lote ndani yangu, Ninahitaji kunena juu yako katika maneno na maisha yangu. Amina.

"Kwa sababu ya heshima na utume wao, wazazi wakristo wanao wajibu wa pekee wa kuwalea watoto wao katlka sala, wakiwaingiza katlka ugunduzi wa polepole wa siri ya Mungu na mazungumzo ya binafsi naye. "Ni hasa katika familia ya kikristo, ikitajirishwa kwa neema na msaada wa sakramentl ya ndoa, kwamba toka miaka ya awali kabisa watoto budi wafundishwe, kufuatana na imanl ile waliyopewa katika Ubatizo wawe na elimu ya Mungu, kumwabudu na kuwapenda jirani zao"" – Baba Mtakatifu Yohani Paulo II, Wosia wa Kitume Familiaris Consortio (WAJIBU WA FAMILIA YA KIKRISTU KATIKA ULIMWENGU WA KISASA)- 60.

VIWAWABOKO
www.viwawaboko.blogspot.com

Monday, December 22, 2014

masomo ya jumatatu 22december2014

Jumatatu, 22 Desemba 2014
Juma la 4 la Majilio

1 Sam 1: 24-28;
1 Sam 2: 1, 4-8;
Lk 1: 46-56

Msifu Mungu Muda Wote!

Wimbo wa Bikira Maria lazima ulinganishwa na wimbo wa sifa wa Hana (1 Sam 2:1-10) na Zakaria (Lk 1:68-79). Wakati sifa za kinabii za Maria zinasimama kwa njia mbalimbali, tofauti kubwa zaidi zipo katika hali zao. Hana alimsifu Bwana wakati akimtoa Samweli. Alikuwa katika haibu ya utasa (1Sam 1:7). Kuzaliwa kwa Samweli kulibadilisha hayo yote, na hivyo Hana alikuwa na sababu ya kumsifu Bwana. Vilevile, Zakaria alivumilia miaka mingi sana bila kuwa na mtoto na kuwa kiziwi na bubu kwa muda wa miezi tisa (Lk 1:20, 62). Sasa wakati mwanae wa kiume alipozaliwa, ulimi wake ulifunguka (Lk 1:64), na alikuwa na sababu ya kumsifu Bwana. Kinyume chake, Mwinjili Luka anaweka sifa za Maria mwanzo wa ujauzito wake. Maria alikuwa akimsifu Bwana sio tu baada ya mateso yake bali kabla na wakati wa mateso yake. Yeye hakusifu tu baadae bali alisifu popote pale. Alikuwa akisifu kwa imani na sio kwasababu aliona hali fulani iliyo nzuri. (2 Kor 5:7).

Sala: Tusaidie Maria, kumsifu Bwana daima kama ulivyomsifu wewe. Amina.

"Kwa upande wake, familia ya kikrlsto imepandildzwa katlka fumbo la Kanisa kwa kadiri hiyo hata kuwa mshiriki, kwa namna yake ya pekee katlka utume wa wokovu wa kanisa: Kwa nguvu ya Sakramenti, wakrlsto mume na mke na wazazl "katika hall na jinsi yao ya maisha wanayo karama ya pekee katika Taifa la Mungu". Kwa sababu hii hawapokei tu pendo la Kristo na kuwa jumuiya iliyookolewa, ball wanaitwa pia kuwashirikisha pendo la Kristo ndugu zao, na hivyo kuwa jumuiya yenye kuokoa. Kwa namna hii, pindi familia ya Kikristo ni tunda na ishara ya kuzaa kwa Kanisa kimungu, husimama pia kama mfano, ushuhuda na mshiriki wa umama wa Mungu(116)." – Baba Mtakatifu Yohani Paulo II, Wosia wa Kitume Familiaris Consortio (WAJIBU WA FAMILIA YA KIKRISTU KATIKA ULIMWENGU WA KISASA)- 49.

VIWAWABOKO
www.viwawaboko.blogspot.com

Sunday, December 14, 2014

Masomo yajumapili 14 desemba 2014, juma la tatu la majilio

Jumapili, 14 Desemba 2014
Juma la 3 la Majilio

Isa 61: 1-2, 10-11;
Lk 1: 46-48, 49-50, 53-54;
1Thes 5: 16-24;
Yn 1: 6-8, 19-28

Je, uelewa wako ni upi juu ya Kristo?

Msemo “mtazamo wa kwanza ni mtazamo bora” umekuwa ni mmoja wa msema wa hatari na wenye uharibifu, katika historia ya saikolojia. “Yohane alikuja kushuhudia nuru …huyu hakuwa ile nuru” (Yn 6 – 8). Wayahudi walifurahishwa kutokana na kile Yohane alichokuwa akitenda. Kabla ya kuwa na mtu yeyote yule awe makini na mwenye kushawishi. Wanashangaa kama yeye ni masiha! … au walau nabii kama Eliya. Ingawa Yohane haitaji kujiweka mbele. Kwa umakini anawarekebisha mtazamo wao wa kwanza. Ilimpasa Yesu kujitoa sadaka mwenyewe juu ya msalaba kuwafanya wao vile alivyo.

Leo Dominika ya tatu ya Majilio inatuitwa ‘Dominika ya Furaha’, itokanayo na maneno ya antifona ya kuingilia. “Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema Furahini! Bwana yu karibu” (Flp 4:4) Katika somo letu la Kwanza kuna viashiria vya furaha vilivyoongelewa na nabii kwa ajili ya liturujia hii. Vifungu vyaonyesha kuwa vyafahamika, kwasababu Yesu katika sura ya nne ya Injili ya Luka abadilisha kifungu hiki, anasoma mistari hii na kurudi kwa ndugu zake wa nazareti na anatangaza kuwa somo hili linamuhusu Yeye. Anakuja kutuponya na kutuweka huru!

Sala: Bwana Yesu, ninangojea kwa furaha ya tumaini kuupokea uponyaji na uhuru wako. Amina.

"Hata katika shlda za kazi ya malezi, shida ambazo nl kubwa zaidi aghalabu siku hizi, wazazi sharti wawafunze watoto wao kwa uaminlfu na ujaslrl katika tunu za maisha ya binadamu. Watoto sharti wakue pamoja na msimamo sahihi wa uhuru kuhusu mali ya dunia, kwa kuchagua mtindo wa maisha ulio rahisi na wa kujinyima, na kusadikishwa kabisa kwamba "binadamu ni mwenye thamani zaidi kwa hali aliyo nayo kuliko kwa kile alichonacho"" – Baba Mtakatifu Yohani Paulo II, Wosia wa Kitume Familiaris Consortio (WAJIBU WA FAMILIA YA KIKRISTU KATIKA ULIMWENGU WA KISASA)- 37.


Tuesday, December 9, 2014

Kongamano la Ujirani Mwema Parokia ya Boko na Bunju

Kongamano la Ujirani Mwema Parokia ya Boko na Bunju

Desturi za Krismasi


Sherehe ya Krismasi imekuwa sikukuu muhimu sana katika tamaduni za mataifa yaliyoathiriwa na Ukristo. Kuna desturi nyingi zilizojitokeza katika karne zote za kusheherekea Krismasi. Sehemu ya desturi hizi zimeenea pia nje ya nchi za asili na hata kutumiwa na watu wasiofuata imani ya Kikristo.
  • Pango la Noeli lililoanzishwa na Fransisko wa Asizi mwaka 1223 kijijini Greccio (Italia) na kuenea kila mahali kama sanaa inayoonyesha kwa njia mbalimbali jinsi Yesu alivyozaliwa.
  • Mapambo ya krismasi: ni hasa nuru na taa za pekee. Alama za nyota kwa kukumbuka nyota iliyopeleka mamajusi hadi Bethlehemu inawekwa ndani na nje ya nyumba na maduka.
  • Mti wa Krismasi - ni ishara ya pekee ya Krismasi yenye asili katika Ujerumani kusini-magharibi ya karne ya 16 hivi. Asili yake iko katika maigizo yaliyosimulia hadithi za Biblia na mti wa Paradiso unaohusiana na masimulizi ya dhambi la kwanza na ujumbe wa Kristo kama mwokozi anayekuja kuondoa dhambi hilo. Kutoka maigizo ya kanisani ishara ya mti uliopambwa matunda uliingia katika nyumba za Wakristo ambako ulipambwa zaidi kwa matunda, keki tamu na pipi kwa watoto. Umekuwa mapambo ya nyumbani kwa majira ya Krismasi. Tangu Krismasi kuwa nafasi muhimu kwa uchumi kuna pia maduka mengi yanayoweka miti hii na katika mazingira ya kibiashara uhusiano wake na mti wa Paradiso umesahauliwa mara nyingi.
  • Zawadi za Krismasi - Martin Luther alitaka kuongeza umuhimu wa Krismasi kwa Wakristo ambao wakati wake walikuwa na desturi ya kuwazawadia watoto kwenye siku ya Mtakatifu Nikolasi tarehe 6 Desemba, wiki 2 kabla ya sikukuu. Hapo Luther alipendekeza kuhamisha zawadi kwa watoto kwenda siku ya kuzaliwa kwake Yesu ili wamkumbuke zaidi Yesu kuliko mtakatifu huyo. Hapo alirejea zawadi zilizopelekwa kwa Yesu na mamajusi kutoka mashariki kufuatana na taarifa ya Injili ya Mathayo mlango 2. Desturi ya kuwazawadia watoto kwenye sikukuu hii ilienea hadi kuwa desturi ya kupeana zawadi kati ya watu wa kila umri. Katika karne ya 20 desturi ilienea kiasi cha kuwa nafasi muhimu ya biashara. Katika nchi nyingi mwezi wa Desemba umekuwa mwezi wa mapato makubwa kushinda miezi mingine. Hata katika miji mikubwa ya nchi kama Dubai au Japani ambako Wakristo ni wachache desturi ya kupeana zawadi imeenea na mapambo ya Krismasi katika maduka yanataka kuwahamasisha wateja kununua zawadi za majira.
  • Baba Krismasi / Baba Noeli

Sikuku ya Noel (Krismasi)

Krismasi (pia Noeli) ni sikukuu ambako Wakristo wengi husheherekea kuzaliwa kwake Yesu Kristo zaidi ya miaka 2000 iliyopita.

Kwa kawaida husheherekewa tarehe 25 Desemba katika Ukristo wa magharibi na tarehe 6 Januari katika ule wa mashariki.

Jina

Kuna majina mawili yaliyo kawaida kwa Kiswahili kwa ajili ya sikukuu hii.
  • Krismasi inatokana na neno la Kiingereza lenye maana ya "Christ`s Mass" yaani misa au ibada ya Kristo.
  • Noeli inatokana na Kiingereza "Noel" (au "Nowell") ambako imepokewa kutoka lugha ya Kifaransa "noël". Hilo ni ufupisho wa Kilatini "Natalis (dies)", "(siku ya) kuzaliwa".
  •  

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR