Thursday, February 21, 2013

Msalaba wa Yesu

Msalaba wa Yesu ni msalaba ule ambao Yesu Kristo alisulubiwa juu yake huko Yerusalemu kwa mamlaka ya Ponsio Pilato labda tarehe 7 Aprili 30 BK.
Adhabu hiyo kali ilianza huko Uajemi na kuenea hadi Dola la Roma ambalo liliitumia hasa katika maeneo ya pembeni.
Tukio hilo, pamoja na ufufuko wa Yesu unaosadikiwa na Ukristo kutokea siku ya tatu (Jumapili ya Pasaka), ndio kiini cha imani ya dini hiyo mpya iliyotokana na ile ya Uyahudi.

Kwa Wakristo fumbo hilo la Pasaka ndilo kilele cha historia ya wokovu inayotangazwa na Biblia ya Kikristo.
Fumbo hilo lilisababisha kazi nyingi za sanaa, hasa uchoraji.
Na tunatakiwa kuyafananisha mahangaiko ya maisha yetu kama msalaba wa Yesu tukiwa na imani kuwa mwisho tutaufikisha na tutafariki na kurudi kwa Mungu Baba hapo tutapata raha ya milele pamoja na Watakatifu wote.

No comments:

Post a Comment

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR