Tuesday, February 17, 2015

Jumatano ya Majivu (ASH WEDNESDAY)

Jumatano ya Majivu ni siku ya kwanza ya kwaresima.
Jumatano ya Majivu Waamini hupakwa Majivu kichwani pamoja na kutamkiwa maneno ya kuhimizwa kufanya toba “ulitoka mavumbini na mavumbini utarejea.
Kwa kawaida siku hii ndiyo Kipindi cha kwaresima huanza rasmi . Waamini hufunga, mfungo unaofuata kilelezo cha Yesu kufunga siku Arobaini jagwani baada ya kubatizwa na Yohane Mbatizaji na kabla ya kuunza utume wake mwenyewe

UMUHIMU WA JUMATANO YA MAJIVU.
Ili kuelewa vizuri maana na umuhimu wa kipindi hiki, tutazame kwa ufupi haya yafuatayo: 
Sala ya mwanzo:
“Ee Bwana utujalie sisi waamini wako tuanze vita vya roho kwa mfungo Mtakatifu. Nasi tulio tayari kupigana na pepo wabaya, tujipatie nguvu kwasababu ya kufunga…”
Majivu’ tunayopakwa siku ya leo ni ishara ya kufanya toba, ni ishara ya kumrudia Mungu! Tukitazama kwa ufupi baadhi ya vifungu katika Biblia tunaona ukweli huu:
-         Jer 6:26
-         Daniel 9:3
-         Yona 3:6
-         1Wamakabayo 3:46, ambapo Mathatia pamoja na wenzake walijipaka majivu kichwani kabla ya kuanza vita dhidi ya ukoloni. Ilikiwa ishara ya kumrudia Mungu ili awe nguvu ao katika mapambano waliokusudia kuyaanza dhidi ya ukoloni/ukandamizaji waliokuwemo!
-         Mt 10:13, Kristu naye alijua utamaduni huu wa toba wa kujipaka majivu pale alipoionya Korazin na Betsaida!
Mapokeo ya Kanisa Katoliki yameendeleza utamaduni huu wa toba:
-         Mnamo Karne ya 6 hadi ya 11 utamaduni huu ulifanyika, hata karne ya 12, papa Urbano wa Pili aliidhinisha majivu yatumike yale yatokanayo na matawi ya mizeituni yaliyotumika katika Jumapili ya Matawi.
Nabii Yoeli katika somo la kwanza (Yoe 2:12-18) anasistiza turarue mioyo wala si mavazi yetu…yaani, tufanye mabadiliko ya ndani na siyo ya nje tu!, kwa maneno mengine, mapinduzi ya kweli yaanze na yatoke mioyoni mwetu na si maonyesho ya njenje tu!
Injili ya leo (Mt 6:1-6, 16-18) iametuasa juu ya suala hilohilo la kufanya mfungo wenye msukumo wa kiroho unaotoka ndani ya moyo wa toba wa mtu na si kufanyakama Mafarisayo walivyokuwa wakifanya. Wao walifunga na kusali ili watazamwe na watu.
Tunapoanza kipindi cha Kwaresma kwa kupakwa majivu siku hii ya leo, tukumbuke wajibu wetu; -kufunga
-         Kusali zaidi na
-         kutenda matendo mema (matendo ya huruma) kwa jirani zetu!    

     Basi, Tumwombe Mungu ili zoezi la mfungo wa Kwaresima lisiwe la historian na la          kupita tu, bali lizae matunda ya kiroho ndani mwetu, tufanye mapinduzi ya kweli ya          kiroho Na hatimaye atustahilishe kushiriki utukufu wake.

No comments:

Post a Comment

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR