Thursday, March 21, 2013

JUMA KUU LA PASAKA

Juma kuu


Juma kuu ni juma la mwaka ambalo Ukristo unaadhimisha kwa namna ya pekee matukio makuu ya historia ya wokovu, kuhusiana na mwisho wa maisha ya Yesu huko Yerusalemu, uliofuatwa na ufufuko wake.
Katika madhehebu mengi, juma hilo linaanza na Jumapili ya matawi ambapo linaadhimishwa kwa shangwe tukio la Yesu Kristo kuingia huo mji mtakatifu kama mfalme wa Wayahudi huku akipanda punda na kushangiliwa na umati wa wafuasi wake, waliofurahia hasa alivyomfufua Lazaro wa Betania.
Lakini Yesu alieleza kuwa ufalme wake si wa dunia hii, na kuwa yeye hakuja kutumikiwa bali kutumikia na kutoa uhai wake uwe fidia ya umati.
Hivyo siku zilizofuata alikabili kwa hiari mateso na kifo kutoka kwa wapinzani wake na kwa mamlaka ya Ponsio Pilato, na hatimaye akafufuka mtukufu usiku wa kuamkia Jumapili.
Kabla ya hapo Yesu alijumlisha hayo matukio yajayo katika karamu ya mwisho aliyokula pamoja na mitume wake 12, akiwaachia agizo la kufanya daima karamu ya namna hiyo kama ukumbusho wake.
Basi, kuanzia Alhamisi kuu jioni hadi Jumapili ya Pasaka jioni Wakristo wanaadhimisha siku tatu kuu za Pasaka, zinazofanya ukumbusho wa Yesu mteswa, mzikwa na mfufuka.

Wednesday, March 20, 2013

IBADA YA MATAWI

Katika mwaka wa Kanisa wa madhehebu mbalimbali ya Ukristo, Jumapili ya matawi inaadhimishwa jinsi Yesu Kristo alivyoingia Yerusalemu ili kufa na kufufuka kwa wokovu wa binadamu wote. Siku hiyo alishangiliwa na umati kwa kutumia matawi, ndiyo asili ya jina.
Ndiyo mwanzo wa Juma kuu linaloadhimisha matukio makuu ya historia ya wokovu kadiri ya imani ya Wakristo.
Tangu mwaka 1985 siku hiyo Kanisa Katoliki linaadhimisha pia "Siku ya kimataifa ya vijana"

Kulikuwa Jumapili ya Matawi hasubihi, na kijana wa familia moja alikuwa amepatwa na mafua, na hivyo hakuweza kwenda Kanisani pamoja na wana familia wengine. Aliachwa nyumbani. Basi wana familia waliporuri kutoka sherehe za Jumapili walifika nyumbani na matawi yao. Yule kijana akawauliza umaana wa matawi yale. Mama akamjibu, “Umati ulimshangia Yesu akipita kwa kuinua ya matawi juu. Basi yule kijana akajibu kwa mshangao, Jumapili ya pekee ambao sikuweza kwenda Kanisani, na Yesu anakuja binafsi!” Kwa sherehe za Jumapili hii ya Matawi, Kanisa huadhimisha ukubusho wa Bwana Yesu wakati aliingia Yerusalemu mahali atakapokamilisha fumbo la Pasaka, yaani, mateso, kufa na kufufuka kwake. Kwa maandamano ya matawi Jumapili hii, tunaanza rasmi Wiki Takatifu tukielekea Pasaka. Maandamano yenyewe humshangilia Yesu, ambaye hivi punde kwa kifo na ufufuko wake, atarudi kwenye utukufu wa Baba. Jumapili ya Matawi ina pande mbili, yaani pande moja ya furaha na nyingine ya mateso. Tunaona kwanza Yesu akiingia Yerusalemu kwa shangwe na furaha, na pia hivi punde atateswa. Yule anayeingia Yerusalemu kwa shangwe, ndiye pia atayehukumiwa na umati afe msalabani kwa ajili ya dhambi zetu. Hivyo Yesu ndiye mfano maalum wa kutuonyesha jinsi safari yetu ya imani itakapokuwa hapo mwisho, yaani kujinyenyekesha na kuteswa hadi kukubali kufa msalabani, ili Mungu atufufue siku ya mwisho.

Kwenye Injili juu ya Mateso ya Bwana iliyoandikwa na Mtk. Luka tunashirikishwa kwenye mchezo wa kuwiga juu wa ukombozi wetu, lakini mchezo wenyewe ni wa hali ya juu sana. Yesu ndiye anayechukua mahali pa katikati kwenye mchezo huu. Mtk. Luka anatuonyesha kwamba Yesu anateseka na kufa asipokuwa na kosa hata moja (Lk 23:4, 14-15, 22). Yesu anateswa na kuuawa na hadui zake ambao sio Warumi, lakini Mayahudi wenzake (Lk 22: 3,31,53). Maandishi ya Luka juu ya mateso na kufa kwa Yesu umaana wake hasa ni Habari Njema juu ya huruma na usamaho wa Mungu Baba. Hivyo Injili yenyewe ni kama mujiza wa vile Baba huendelea kuonyesha huruma wake kwa wote. Hivyo Yesu anaponya sikio la askari aliyekatwa na Petro; Yesu anamwangalia Petro kwa huruma wakati alimkana mara tatu; na Yesu anamuhurumia mwizi aliyekuwa amehukumiwa kufa msalabani. Kwenye mateso yake huko gethsemani, wakati alikuwa akichekelewa na umati na mateso yake yote msalabani, Yesu ni ishara ya Mungu baina ya watu wake; na pia kama chombo kinachoonyesha upendo na huruma wa Mungu. Kuna ujumbe gani tungepeleka nyumbani Jumapili hii? 1) Tunapotafakari juu ya mateso na kifo cha Bwana, tuyaone pia kwenye maelfu ya watu wetu barani Afrika wanaoteswa na kufa bila kosa lolote. Pia tukumbuke mateso yetu binafsi. 2) Kwenye mateso ya Yesu tunaonyeshwa kwamba Mungu katika upendo na huruma wake hawezi kutuacha peke. Pia tunagundua kwamba hapo mwisho, mateso yatageuzwa kuwa furaha, na kifo kuwa maisha mapya. 3) Tukumbuke kwamba ni kwa ajili ya dhambi zetu Yesu anahukumiwa kufa msalabani, na ni kwa ajili ya upenda na huruma wa Mungu tunapata maondoleo ya dhambi tukitubu na kuungama dhambi zetu.


 ABEL R. REGINALD.

Tuesday, March 19, 2013

PICTURE ZA HIJA YA VIJANA - BAGAMOYO 2013

 Vijana wakiwa kwenye njia ya msalaba wakielekea kituo cha mwisho ndani ya kanisa la Bagamoyo.



Viongozi wa Parokia ya Boko kutoka kulia ni Eppie Mwikola-Mhazin, Flora Magele-Mwenyekit Msaidizi, Abel Reginald-Mwenyekiti, Frida Meeda-Katibu na Timoth Jafethy-Katibu Msaidizi






Monday, March 18, 2013

MATANGAZO YA JUMA LA MATAWI-18-24/03/2013

Mazoezi ya Igizo la Ijumaa kuu yanaendelea Kigangoni Boko fika kuanzia jumatatu hadi jumapili  saa kumi jioni. 

Wasilisha Mchango wako wa Matawi kwa Viongozi wako wa jumuiya na kigango. 
  1.  JUMAMOSI TAREHE 23/03/2013
 Vijana wa Kigango cha Rafael wanatakiwa kukutana jumamosi asubuhi kwa ajili ya kufanya maandalizi ya Matawi Muda ni saa 12:30 asubuhi.
  Vijana wa Kigango cha Mbweni nao wanabidi wakutane asubuhi kwa ajili ya kujiandaa Kusimamia ibada siku ya jumapili ya Matawi.
   jumamosi saa 7:00 mchana tutakuwa na kikao cha halmashauri agenda na maandalizi ya ibada ya matawi don bosco.
  
 
 2.JUMAPILI TAREHE 24/03/2013
Vijana wote wa Parokia tutashiriki katika Ibada ya Matawi itakayofanyika don bosco upanga kuanzia saa tatu asubuhi.
   
  JUMAPILI TAREHE 24/03/2013
      RATIBA ZA IBADA YA MATAWI
KIGANGO CHA BOKO.
MISA YA KWANZA 12:30-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 1:00-3:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 3:00-4:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 2:00-4:00 ASUBUHI.


CHAGIA USHIRIKI WAKA WA  ibada ya matawi don bosco MAPEMA...tarehe 24/03/2013 mchango ni tshs 3500

Friday, March 15, 2013

speech ya Pope

Wasifu wa Baba Mtakatifu Francis!



Baba Mtakatifu Francis ni Myesuiti wa kwanza kuwa Khalifa wa Mtakatifu Petro. Ni Papa wa kwanza katika historia ya Kanisa kutoka nje ya Bara la Ulaya na Papa wa kwanza katika historia ya Kanisa kutoka katika nchi za Amerika ya Kusini, nchi ambazo kwa sasa zina idadi kubwa ya waamini wa Kanisa Katoliki. Kwa mara ya kwanza Jina la Mtakatifu Francis linatumiwa na Khalifa wa Mtakatifu Petro.

Lakini ikumbukwe kwamba, kuna watakatifu wanne wenye majina ya Francis. Hawa ni akina Mtakatifu Francis wa Assisi, Msimamizi wa Italia; Mtakatifu Francis wa Sale, Mwalimu wa Kanisa na Msimamizi wa Waandishi wa Habari; Mtakatifu Francis Xsaveri, Myesuit na Msimamizi wa Wamissionari pamoja na Mtakatifu Francis wa Paulo, Mkaa pweke na mwanzilishi wa Shirika la Ndugu wadogo wa Calabria.

Kardinali Jorge Mario Bergoglio, SJ, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Buenos Aires, Argentina, alizaliwa tarehe 17 Desemba 1936 mjini Buenos Aires. Yeye ni mtoto wa Mzee Mario na Mama Regina Sivori, waliobahatika kupata watoto watano. Katika ujana wake, alisoma na kufuzu kama mtaalam wa kemia, baadaye akaacha kazi hii na kujiunga Seminarini huko Villa Devoto.

Tarehe 11 Machi 1958 alijiunga na malezi ya Kinovisi katika Shirika la Wayesuit akaendelea pia na masomo dunia nchini Cile na kunako mwaka 1963 alirejea tena Buenos Aires na kujipatia shahada ya uzamili kutoka katika Kitivo cha Falsafa, Chuo Kikuu cha San Josè huko San Miguel.

Kati ya mwaka 1964 na mwaka 1965 alikuwa ni Jaalim wa Fasihi Andishi na Saikolojia katika Chuo cha Bikira Maria wa Santa Fe. Kunako mwaka 1966 akafundisha masomo haya kwenye Chuo Kikuu cha Salvatore cha Buenos Aires. Kuanzia mwaka 1967 hadi mwaka 1970, alijiendeleza kwa masomo ya Taalimungu katika Chuo Kikuu cha San Josè kilichoko San Miguel na kujipatia shahada ya uzamili.

Tarehe 13 Desemba 1969 akapewa daraja takatifu la Upadre. Kati ya mwaka 1970 hadi mwaka 1971 alikamilisha hatua ya tatu ya majiundo yake kama Myesuit huko Hispania na tarehe 22 Aprili 1973 akaweka nadhiri za daima. Kati ya mwaka 1972 hadi mwaka 1973 alikuwa ni mlezi wa Wanovisi, Jaalim, Mshauri na Gombera wa Chuo cha Massimo. Tarehe 31 Julai 1973 akateuliwa kuwa Mkuu wa Jimbo la Argentina kwa upande wa Shirika, utume ambao aliutekeleza kwa muda wa miaka 6. Kati ya Mwaka 1980 hadi mwaka 1986, alikuwa ni Gombera wa Chuo cha Massimo na Paroko wa Parokia ya Patriaki San Josè, Jimboni San Miguel.

Kunako mwaka 1986 alikwenda nchini Ujerumani kumalizia masomo yake katika Shahada ya Uzamivu na wakuu wake wa Shirika wakampatia jukumu la kuwa mkuu wa malezi ya kiroho na muungamishi katika Chuo cha Salvatore.

Tarehe 20 Mei 1992 Papa Yohane Paulo II akamteuwa kuwa Askofu msaidizi wa Jimbo kuu la Buenos Aires, akawekwa wakfu kama Askofu tarehe 27 Juni 1992. Tarehe 3 Juni 1997 akateuliwa kuwa Askofu mwandamizi wa Jimbo kuu la Buenos Aires na tarehe 28 Februari 1998 akasimikwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Buenos Aires baada ya kifo cha Kardinali Antonio Quarracino na hivyo kuwa pia ni Mkuu wa Kanisa Katoliki Argentina.

Mwenyeheri Yohane Paulo II akamteuwa na kumsimika kuwa Kardinali kunako tarehe 21 februari 2001. Ameshiriki katika Sinodi ya Maaskofu iliyofanyika kunako mwaka 2001. Akashiriki pia kwenye mkutano wa Makardinali wakati wa uchaguzi wa Papa kati ya tarehe 18 na 19 Aprili 2005. Alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri ya Sinodi ya kumi na moja ya Maaskofu kuanzia tarehe 2 hadi 23 Oktoba 2005.

Mjini Vatican alikuwa ni mjumbe wa Baraza la Kipapa la Ibada na Nidhamu ya Sakramenti za Kanisa, Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makleri, Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume, Tume ya Kipapa ya Amerika ya Kusini, Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makleri na Mjumbe wa Sekretarieti ya Sinodi.

Nchini Argentina alikuwa ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki Argentina.
Rais wa Tume ya Baraza la Maaskofu kwa ajili ya Chuo Kikuu cha Kipapa cha Argentina. Alikuwa ni mratibu mkuu wa Mahakama ya Kanisa; Mratibu wa Mahakama ya Jimbo kuu la Buonos Aires. Tangu mwaka 2005 hadi 2011 alikuwa ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Argentina.
Ni mwandishi wa Vitabu vifuatavyo:
    1982: Meditaciones para religiosos
    1986: Reflexiones sobre la vida apostólica
    1992: Reflexiones de esperanza
    1998: Diálogos entre Juan Pablo II y Fidel Castro
    2003: Educar: exigencia y pasión
    2004: Ponerse la patria al hombro
    2005: La nación por construir
    2006: Corrupción y pecado
    2006: Sobre la acusación de sí mismo
    2007: El verdadero poder es el servicio

Wednesday, March 13, 2013

Tamasha 2011


 HICHI KILIKUWA KIKOSI CHA TIMU YA KIGANGO CHA BOKO - 2001
NA HII NDIYO ILIKUWA TIMU YA KIGANGO CHA BUNJU KWA MWAKA 2011

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR