Saturday, April 13, 2013

Shutuma za udini dhidi ya Mwl. J. K. Nyerere, Baba wa Taifa la Tanzania

Shutuma za udini dhidi ya Mwl. J. K. Nyerere, Baba wa Taifa la Tanzania



Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa la Tanzania ni kati ya viongozi wa siasa wanaoheshimika sana Barani Afrika. Lakini kwa bahati mbaya, "Nabii hakosi heshima isipokuwa kwa watu wa nyumbani kwake".

Kwa miaka kadhaa, baadhi ya Waamini wa dini ya Kiislam nchini Tanzania amedai kwamba, wakati wa utawala wa Mwalimu Julius K. Nyerere, waamini hao walinyanyaswa kiasi kwamba, wamebaki nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na waamini wa dini nyingine nchini Tanzania.

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican, katika mahojiano maalum na Askofu Michael Msonganzila wa Jimbo Katoliki Musoma, anakanusa uvumi huu kwa kusema kwamba, ni malalamiko ambayo yamezagaa nchini Tanzania kiasi kwamba, kuna baadhi ya watu wamediriki hata kutengeneza Kanda ili kueneza uvumi huu. Haya ni mawazo yaliyonunuliwa kutoka nje, ili kuvuruga misingi ya haki, amani, upendo na mshikamano wa kitaifa ambao watanzania kwa takribani miaka 50 iliyopita wamekuwa wakiufaidi.

Askofu Msonganzila anasema, hizi ni dalili za ukoloni mambokesho! Kinzani za kidini kwa madai kwamba, Serikali ya Tanzania inaongozwa na mfumo Kristo ni uzushi usiokuwa na msingi. Watanzania watakumbuka kwamba, wakati wa Azimio la Arusha, Serikali ilitaifisha shule zilizokuwa zinamilikiwa na kuendeshwa na Kanisa, ili kutoa fursa kwa watanzania wengi zaidi kupata fursa ya elimu.

Kanisa lilitambua na kuheshimu nia njema iliyooneshwa na Baba wa Taifa bila kunung'unika. Ikumbukwe kwamba, mikakati ya kichungaji katika sekta ya elimu ni sehemu ya Uinjilishaji wa kina unaofanywa na Kanisa Katoliki katika mchakato wa kukomboa mtu mzima: kiroho na kimwili, kumbe kumiliki na kuendesha shule katika viwango mbali mbali si jambo la nasibu bali ni sehemu ya vinasaba vya Kanisa Katoliki.

Hata baada ya kutaifishwa shule, watanzania wengi waliokuwa na kiu ya elimu walipata bila ya ubaguzi wowote, kinyume kabisa cha madai yanayotolewa na baadhi ya waamini kwa sasa! Kuna watanzania wengi ambao baadhi yao ni viongozi waandamizi Serikali wamesoma katika shule zilizotaifishwa au zilizokuwa zinamilikiwa na Kanisa, bila shaka hawa ni mashahidi makini wa hali halisi ilivyokuwa katika shule hizi.

Askofu Michael Msonganzila anasema, hizi ni zama za ukweli na uwazi, watanzania wanapaswa kufungua macho, masikio, mioyo na akili zao ili kuuona ukweli. Huu si muda wa malumbano, bali watu wawekeze katika elimu inayomwangalia mtu mzima: kiroho na kimwili, ili kuweza kuwajengea watoto wa kitanzania, kesho iliyo bora zaidi.

Elimu ya dini na elimu dunia zina nafasi yake. Watanzania wasikubali kutumiwa na watu wasiowatakia mema kwa kufanya ghasia na malumbano yasiyokuwa na tija kwa maendeleo yao. Wakumbuke daima kwamba, vita na ghasia hazina macho, kwa kujiingiza katika migogoro ya kidini, watapoteza hata kile kidogo walicho nacho kwa sasa! Ni wakati wa kujenga na kuimarisha mshikamano na umoja wa kitaifa dhidi ya maadui walioko ndani na nje ya Tanzania wanaotaka kulitumbukiza Taifa katika maafa ya udini.

Msitafute njia ya mkato katika maisha!




Katika maadhimisho ya kumbu kumbu ya mwezi mmoja tangu Baba Mtakatifu Francisko alipochaguliwa kuliongoza Kanisa, Jumamosi, tarehe 13 Aprili 2013 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu iliyohudhuriwa na Wanajeshi wa Kikosi cha Zimamoto cha Vatican na Watawa wa Upendo kwenye Kikanisa cha Domus Sanctae martha, kilichoko mjini Vatican.

Papa amewakumbusha kwamba, hata katika mahangaiko, mateso na shida mbali mbali anazoweza kukabiliana nazo mwamini, kamwe asithubutu kutafuta njia ya mkato bali wajiaminishe kwa Mwenyezi Mungu. Waamini wa Kanisa la Mwanzo, kadiri ya Matendo ya Mitume, walijikuta wanaanza kulalamikiana na kubaguana katika huduma mambo ambayo yalikuwa yanadhohofisha umoja na mshikamano wa upendo miongoni mwa wafuasi wa Kristo. Mitume wakachukua uamuzi wa kuwakutanisha na kujadiliana kwa pamoja na hatimaye, wakapata suluhisho la matatizo yao.

Mitume walibainisha kwamba, dhamana yao ya kwanza ni kusali na kutangaza Habari Njema ya Wokovu; kumbe Mashemasi saba walioteuliwa walipewa dhamana ya kutoa huduma ya upendo ambayo ni mwendelezo wa huduma na mshikamano wa upendo unaofanywa na Mama Kanisa sehemu mbali mbali za dunia. Kristo yuko daima pamoja na wafuasi wake na kamwe hawezi kuwaacha wakaangamia.

Baba Mtakatifu anasema, hivi ndivyo ilivyotokea pale mitume wake walipokuwa wameelemewa na hofu pamoja na woga, akawatokea na kuwaambia wasiogope. Hata kama waamini wanakosea, wasikate tamaa, bali watambue kwamba, Yesu yuko pamoja nao. Wachunguze pale walipokosea, wajiwekee mikakati ya kusahihisha na kurekebisha pamoja na kujipa moyo wa kusonga mbele kwa imani na matumaini zaidi. Waamini kamwe wasitafute njia ya mkato katika maisha!

Tuesday, April 2, 2013

RATIBA YA JUMA TAREHE 02-07/04/2013

Safisha mwenendo wako kuwa mfano kwa jamii yako, toa mafundisho ya dini zaidia wasiojiwezi....Maisha ya Kitakatifu.

lipa ada yako ya mwezi kwa kiongozi wako wa jumuiya, Kanda au Kigango. 
  1.  JUMAMOSI TAREHE 06/04/2013
 Vijana wote unatakiwa kushiriki makusanyiko ya Jumuiya...shiriki katika Jumuiya yako saa 12:30 asubuhi.

  Viongozi wote wa VIWAWA ngazi ya Jumuiya Kigango cha Mt Rafael mnatakiwa kukutana Kanisani saa 10:00 jioni kwa ajili ya kufanya uchaguzi wa viongozi wa Vijana Kigango.

  
 
 2.JUMAPILI TAREHE 24/03/2013
Vijana ndiyo chachu ya Kanisa Nguvu kubwa ya Ujenzi na Mabadiliko yaanze kwetu Hudhuria Misa Jumapili kama Amri ya Kanisa inavyotuelekeza.
  
  JUMAPILI TAREHE 07/04/2013
      RATIBA ZA IBADA 
KIGANGO CHA BOKO.
MISA YA KWANZA 12:30-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 1:00-3:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 3:00-4:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
MISA YA KWANZA SAA 1:00-3:00 ASUBUHI.
MISA YA PILI SAA 3:00-5:00 ASUBUHI 

KANDA MAALUMU YA ANTONY WA PADUA -MBWENI TETA
MISA NI SAA 3:00 ASUBUHI


Kutakuwa na Kikao cha Halamashauri Ya VIWAWA Parokia ya Boko -Kikao kitaanza saa 4:30 asubuhi...Kigangoni Rafael wajumbe ni Viongozi wote wa Vigango fika bila kukosa Tuukuze UTUME wetu

Saturday, March 30, 2013

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Pasaka kwa Mwaka 2013

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Pasaka kwa Mwaka 2013 nchini Tanzania ni: Amani na Maendeleo!



Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salama akitoa ujumbe wake wa Siku kuu ya Pasaka kwa Mwaka 2013 inayokwenda sanjari na Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, anawaalika Wakristo kwa namna ya pekee kabisa kuombea amani, umoja na mshikamano wa kitaifa, hasa kutokana na kushamiri kwa vitendo vya choko choko za kidini nchini Tanzania zilizopelekea: madhulumu na mauaji ya viongozi wa kidini pamoja na uchomaji moto wa nyumba za Ibada.

Kinzani za kidini zinazoendelea nchini Tanzania ni changamoto kwa Wakristo na Waislam kukutana na kujadiliana mustakabali wa Tazania. Kwa vile Serikali inayowajibu wa kulinda na kudumisha misingi ya haki, amani na utulivu inapaswa kuwapo ili kufuatilia majadiliano haya.

Kwa miaka mingi Wakristo na Waislam nchini Tanzania wameishi na kupendana kama ndugu na wala tofauti zao za kidini halikuwa ni jambo la kuwagawa! Lakini mambo yamebadilika katika miaka ya hivi karibuni kiasi cha kuwafanya watu kuanza kujiuliza, hivi kweli ni nani anayehusika na uchochezi wa vurugu za kidini na kwa manufaa ya nani?

Majadiliano ya kidini ni njia muafaka inayoweza kumaliza choko choko za kidini, kila upande ukilijadili suala hili katika ukweli, upendo na haki. Kardinali Pengo anaendelea kuwasihi Wakristo na watanzania wenye nia njema kuepukana na kishawishi cha kutaka kulipiza kisasi kutokana na madhulumu wanayokabiliana nayo. Anasema, ulinzi na usalama wakati wa Maadhimisho ya Juma kuu ni kazi na jukumu la Serikali, kumbe anatumaini kwamba, Wakristo wataweza kuadhimisha Mafumbo ya Imani yao kwa amani na utulivu.

Kardinali Pengo anasema, atakwenda Kanisa kuadhimisha Mafumbo ya Ukombozi, kama ni kufa ni afadhali afie Kanisani na wala hataacha kwenda kusali kwa sababu ya vitisho vya ulipuaji wa Makanisa vilivyozagaa nchini Tanzania wakati huu.

Kardinali Pengo amevishauri vyombo vya dola kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi ya ukweli, uwazi na maadili ya kazi. Anasema, Serikali haiwezi kuacha Tanzania kutawaliwa na "wahuni wachache" wanaoleta vurugu kwa kisingizio cha dini na kukazia kwamba, hatua madhubuti hazina budi kuchukuliwa ili haki, amani na utulivu viweze kudumishwa.

Itakumbukwa kwamba, Waziri mkuu Mizengo Pinda wa Tanzania na ujumbe wake walipotembelea Radio Vatican hivi karibuni alibainisha kwamba, Serikali ya Tanzania inatarajia tarehe 4 Aprili 2013 kukutana na viongozi wa kidini na wadau mbali mbali ili kwa pamoja kuweza kujadili mustakabali wa Tanzania kwa kuangalia amani na utulivu kama nyenzo muhimu katika ustawi na maendeleo ya Tanzania.

Friday, March 29, 2013

Hii ndiyo Aleluya kuu lazima


IBADA YA ALHAMISI KUU-POPE FRANCIS

Nimewapeni mfano, nanyi hudumianeni kwa ukarimu na upendo!



Baba Mtakatifu Francisko, Jioni ya Alhamisi kuu, tarehe 28 Machi 2013 ameadhimisha Ibada ya Karamu ya Mwisho, katika Gereza la Watoto la "Casal del Marmo," lililoko mjini Roma kwa kuwaosha miguu watoto kumi na wawili, kielelezo cha upendo wa Kristo unaomwilishwa katika huduma kwa jirani, lakini zaidi kwa wale wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.

Katika mahubiri yake kwa vijana hawa, amewashirikisha upendo ulioneshwa na Yesu Kristo, Siku ya Alhamisi kuu, alipoweka mavazi yake kando, akaanza kuwaosha mitume wake miguu, kitendo ambacho kilimshangaza Mtume Petro, kiasi cha kutaka kukataa katu katu kuoshwa miguu na Yesu, lakini akafafanuliwa maana yake, kiasi kwamba, akaweza hata kuridhika na uamuzi uliotolewa.

Yesu ambaye ni Mwalimu na Bwana, Nafsi ya Pili ya Fumbo la Utatu Mtakatifu, ndiye aliyetekeleza kitendo hiki cha unyenyekevu, ambacho kilikuwa kinafanywa na watumwa! Akawaachia mfano wa kuigwa na kuendelezwa, kwa kutambua kwamba, uongozi ni huduma hasa kwa wanyonge na wale wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.

Ni mwaliko wa kumegeana upendo unaobubujika kutoka kwa Kristo, aliyewapenda watu wake upeo kiasi cha kuyamimina maisha yake pale juu Msalabani. Huduma ya upendo, iwachangamotishe waamini na watu wenye mapenzi mema kujikita katika msamaha na upatanisho unaopaswa kububujika kutoka katika undani wa mtu mwenyewe.

Baba Mtakatifu Francisko anasema, kama Padre na Askofu wa Roma, anajisikia kuwajibika kuwaonjesha huruma na upendo wa Kristo kwa njia ya huduma inayopata chimbuko lake kutoka katika moyo wake na wala si jambo la kutaka kujionesha mbele ya watu.

Kwa maneno machache, hii ni imani katika matendo, inayowachangamotisha waamini na watu wenye mapenzi mema, kusaidiana kwa hali na mali; wakiungana kwa pamoja kutafuta mafao ya wengi. Huduma ya upendo ni changamoto endelevu inayotolewa na Yesu aliyekuja kutumikia na kuyamimina maisha yake kwa ajili ya ukombozi wa wengi.

Thursday, March 21, 2013

KIPINDI CHA KWARESIMA

Bibilia na Kipindi cha Kwaresima

Katika Agano la Kale Musa ndiye aliyeongoza Waisraeli. Sisi tunakumbuka na kufuata safari yao ya ukombozi, walipokaa jangwani miaka 40 ili kuelimishwa kinaganaga juu ya yale yatokanayo na maneno 10 ambayo Musa alipewa na Mungu alipofunga siku 40 juu ya mlima Sinai.
Hayo yalikamilishwa na Yesu katika Agano Jipya kama kiongozi na mkombozi wa wote. Kabla hajaanza utume wake, yeye pia alifunga siku 40 jangwani akijilisha matakwa ya Baba ili ayatekeleze na kuwatangazia watu wote.

Juhudi za Kwaresima

Kufuatana na hayo yote Kanisa linafunga siku 40 katika jangwa la kiroho. Wakati wa Kwaresima linawaongoza waamini katika safari ya kujirekebisha kulingana na Neno la Mungu la Agano la Kale na la Agano Jipya. Wote wanahimizwa kufunga safari hiyo kadiri ya hali yao: kwanza wale wanaojiandaa kubatizwa usiku wa Pasaka (hasa kwa kufanyiwa mazinguo matatu yanayofuatana katika Dominika III, IV na V), lakini pia waliokwishabatizwa, ambao kabla ya hapo wanatakiwa kutubu na kuungama dhambi ili warudie kwa unyofu ahadi za ubatizo.
Makundi yote mawili watakula pamoja Mwanakondoo ili kuishi upya kwa upendo, jambo litakalofanya hata wasio Wakristo wafurahie Pasaka.
Kazi za urekebisho zinahitaji juhudi za pekee. Vivyo hivyo kwa ukombozi wa kiroho Kwaresima inadai bidii nyingi pande mbalimbali: katika kufunga, kutoa sadaka, kusali na kusikiliza Neno la Mungu hasa wakati wa ibada. Hayo yote yanahusiana na kusaidiana.
Mkristo akijinyima chakula cha mwili anajifunza kufurahia zaidi mkate wa Neno la Mungu na wa ekaristi, tena anatambua zaidi anavyopaswa kuwahurumia wenye njaa na shida mbalimbali. Toba inahimizwa isiwe ya ndani na ya binafsi tu, bali pia ya nje na ya kijamii: itokane na upendo na kulenga upendo kwa kurekebisha kasoro upande wa Mungu (sala), wa jirani (sadaka) na wa nafsi yetu (mfungo).
Mfungo, yaani kujinyima tunavyovipenda na hata tunavyovihitaji, uwe ishara ya njaa yetu ya Neno la Mungu, ya nia yetu ya kushiriki mateso ya Yesu yanayoendelea katika maskini, ya kulipa kwa dhambi zetu na kuachana nazo. Sadaka inayotokana na sisi kujinyima inampendeza Mungu kuliko ile isiyotuumiza; msaada unaweza kutolewa pia kwa kutetea haki za binadamu dhidi ya wanyanyasaji. Sala inastawi kwa kusikiliza sana Neno la Mungu hasa kwa pamoja (katika familia, jumuia, liturujia n.k.). Ndiyo maana wakati wa Kwaresima Kanisa linazidisha nafasi za kulitangaza na hivyo kuelimisha wote kuhusu mambo makuu ya imani na maadili yetu.

Kwaresima katika liturujia.

Kuna mpangilio kabambe wa masomo ya Misa, hasa ya Dominika, ili wote wafuate hatua kuu za historia ya wokovu (somo la kwanza) na kuchimba ukweli wa ubatizo (mwaka A), agano na fumbo la Kristo (mwaka B) na upatanisho (mwaka C). Kwa njia hiyo tunatangaziwa jinsi Mungu anavyotuokoa; pia upande wetu kuanzia Dominika ya kwanza tunajielewa kuwa watu vishawishini ambao tunapaswa kushinda kwa kumfuata Yesu, si Adamu: kwenda jangwani ili kumtafuta Bwana na matakwa yake.
Kilele cha safari ya Kwaresima ni Dominika ya Matawi, tunapoingia Yerusalemu pamoja na Yesu anayekwenda kufa na kufufuka kwa ajili yetu. Liturujia ya siku hiyo ina mambo mawili: kwanza shangwe (katika maandamano), halafu huzuni (kuanzia masomo, ambayo kilele chake ni Injili ya Mateso).
Baada ya Kwaresima kwisha, tutapitia tena historia ya wokovu katika kesha la Pasaka ambapo hatua zote zinaangazwa na ushindi wa Kristo mfufuka.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR