Wednesday, August 13, 2014

blessed Isidore Bakanja Day

Blessed Isidore Bakanja was beatified on 24 April 1994 by Pope John Paul II. His feast day is 12 August on the Carmelite Calendar of Saints, and 15 August in the general Church calendar. Isidore Bakanja is considered a strong witness to the grace of reconciliation that can be experienced between peoples of different races.bonyeza hapa kuendelea ,endelea kusoma

Wednesday, July 16, 2014

Askofu Mteule Joseph P. Mlola, ALCP / OSS Jimbo la Kigoma

Baba Mtakatifu Francisko amemteua Padre Joseph P. Mlola , wa Shirika la Kazi ya Roho Mtakatifu (ALCP / OSS) kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki Kigoma, Tanzania. Kabla ya uteuzi mpya , alikuwa ni Gombera wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Paulo Kipalapala, Tabora Tanzania.

Askofu Mteule Joseph P. Mlola, ALCP / OSS, alizaliwa Januari 9, 1966 Mashati Rombo, Moshi. Baada ya elimu ya msingi na sekondari, alijiunga na seminari ndogo ya Uru (Moshi), na baadaye kujiunga Shirika la Utume wa Yesu akiwa katika Seminari Kuu Kenya, ambako alichukua masomo ya falsafa. Na alikamilisha masomo ya Teolojia katika Seminari Kuu ya Mtakatifu Paulo Kipalapala, Tabora.
Alipokea Daraja la Upadre Julai 12, 1997, chini ya maisha ya Jumuiya ya Mapadre wa Kazi ya Roho Mtakatifu "Opus Spiritus Sancti - ALCP / OSS". Baada ya Upadrisho alishika nyadhifa mbalimbali ifuatavyo :

1997-1999:Paroko Msaisizi wa Parokia ya Nairagie Enkare, Jimbo la Ngong, Kenya;
1999-2000: Makamu wa Ngombera katika nyumba ya malezi ya Roho Mtakatifu, Morogoro Tanzania
2000-2001: Paroko msaidizi Parokia ya Caliti, Avellino, Italia;
2001-2005: Alijiunga katika masomo ya juu ya shahada ya Uzamivu (udaktari), katika kanuni ya Teolojia, katika Chuo Kikuu cha Kipapa Urbaniana.
2005-2011: Makamu Ngombera katika Seminari Kuu ya Mtakatifu Charles Lwanga Segerea, Dar-es-Salaam Tanzania ;
tangu mwaka 2011 hadi uteuzi mpya, alikuwa Gombera wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Paulo Kipalapala, Tabora Tanzania.

Jimbo la Kigoma, liliundwa mwaka 1953,chini ya Jimbo Kuu La Tabora. LIna eneo la kilomita mraba 45 066 kukiwa na idadi ya watu milioni 2, ambao kati yao 515 701 ni Wakatoliki. Kuna Parokia 22, , Mapadre 55 ( Mapadre wa Jimbo wakiwa 42 na Mapadre wa Mashirika 13 ), watawa ni 65 na Waseminaristi 19.
Jimbo la Kigoma, imekuwa wazi tangu Juni 27, 2012, kufuatia Askofu wake Protase Rugambwa, kuteuliwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI kumteuwa kuwa Askofu mkuu, Katibu mwambata wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu na Rais wa Mshirika ya Kimissionari ya Kipapa mjini Roma.


Friday, June 27, 2014

Ibada ya kumwaga Sr. Crescentia Kapuli -Ubungo Riveside

Jumapili tarehe 29 juni 2013 Sherehe za Watakatifu Petro na Paulo miamba wa Imani

Jumapili tarehe 29 Juni 2014 Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Sherehe za Watakatifu Petro na Paulo, miamba wa imani, kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican. Hawa ni “vigogo” wa imani waliojitosa kimasomaso kutangaza Habari Njema ya Wokovu kwa mataifa kwa njia ya mahubiri, lakini zaidi kwa njia ya ushuhuda wa maisha yao, wakawa tayari kujisadaka kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake.

Hii ni Jumapili ambayo Baba Mtakatifu anatarajiwa kutoa Pallio Takatifu kwa Maaskofu wakuu wa Majimbo makuu walioteuliwa hivi karibuni, kama kielelezo cha umoja na mshikamano kati ya Maaskofu wakuu na Khalifa wa Mtakatifu Petro. Hii pia ni siku ya mshikamano kwa kuonesha upendo kwa Baba Mtakatifu kwa njia ya sala, lakini kwa kuchangia katika Mfuko maalum wa huduma ya mshikamano na upendo unaotekelezwa na Khalifa wa Mtakatifu Petro, sehemu mbali mbali za dunia.

Mchango huu unaotolewa na waamini pamoja na watu wenye mapenzi mema unamwezesha Baba Mtakatifu kuwasaidia watu waliokumbwa na majanga asilia kama vile matetemeko ya ardhi, mafuriko, njaa, ukame. Ni msaada unalenga kumsaidia mtu mzima katika mahataji yake: kiroho na kimwili, kwa kuchangia maboresho katika sekta ya elimu, afya na maendeleo endelevu. Kanisa limeendelea kuwa mstari wa mbele kwa ajili ya kuwasaidia maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii, kwa kuwajengea uwezo ili kukabiliana na changamoto za maisha kwa ujasiri mkuu.

“Usiwasahau maskini” ni maneno ambayo Kardinali Claudio Hummes alimwambia Baba Mtakatifu Francisko mara tu baada ya kuchaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki. Maneno haya yakaingia na kunata katika akili na moyo wa Baba Mtakatifu Francisko, ambaye leo hii maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni anawapatia kipaumbele cha pekee katika maisha na utume wake, si kwa maneno tu bali kwa njia ya ushuhuda wa maisha. Papa akamchagua Mtakatifu Francisko wa Assis mpenda amani, mazingira na mhudumu wa maskini kuwa msimamizi wake, leo hii mjini Vatican wimbo umebadilika, mwenye macho aambiwi tazama!

Siku ya Upendo wa Papa ilianzishwa kunako tarehe 8 Agosti 1871 na Papa Pio IX katika Waraka wake wa kichungaji “Saepe Venerabilis” na tangu wakati huo, kila mwaka ifikapo tarehe 29 Juni, Kanisa linashikamana na Papa kuonesha upendo na ukarimu kwa kuchangia mfuko unaogharimia shughuli mbali mbali za upendo zinazotekelezwa na Baba Mtakatifu sehemu mbali mbali za dunia.

Nawe unaweza kushikamana na Papa kwa kuchangia katika mfuko huu! Kwa njia hii, unashiriki kikamilifu katika mchakato wa Uinjilishaji Mpya kwani maisha na utume wa Kanisa unaendelea kupanuka siku hadi siku!

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR