Monday, October 13, 2014

Masomo ya Dominika ya 28 ya Mwaka A wa kanisa, Tarehe 12/10/2014

12
 October
 JUMAPILI YA 2 YA MWAKA "A" 2014.
SOMO  1. Isa. 25:6-10

Somo katika  kitabu cha Nabii Isaya.
Katika mlima huu Bwana wa majeshi  atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karama ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo  wake, iliyochujwa sana. Naye katika mlima huu atauharibu uso wa sitara iliyowekwa juu ya watu wote, na utaji ule uliyotandwa juu ya mataifa yote. Amemeza mauti hata milele; na Bwana Mungu atafuta machozi katika nyuso zote; na aibu ya watu wake ataiondoa katika ulimwengu wote; maana Bwana amenena hayo. 

Katika siku hiyo watasema, 
Tazama huyu ndiye Mungu wetu, 
Ndiye tuliyemngoja atusaidie; 
Huyu ndiye Bwana tuliyemngoja,
 Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake.
 Kwa maana mkono wa Bwana utatulia katika mlima huu.


SOMO  2. Flp. 4:12-14,19-20
Somo katika waraka wa mtume Paulo kwa Wafilipi. 
Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu. Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amena.


  INJILI.Mt. 21:33-43

Somo katika Injili ilivyoandikwa na Mathayo.


Yesu alijibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanae arusi. Akawatuma watumwa wake wa waite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja. Akatuma tena watumwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni nimeandaa karamu yangu; ng'ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini. Lakini hawakujali, wakaenda zao mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake; nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua. Basi yule mfalme akaghadhibika;akapeleka majeshi yake,akawaangamiza wauaji wake, akauteketeza mji wao. Kisha akawaambia watumwa wake, arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili. Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini. Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni. Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiye vaa vazi la arusi. Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa. Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.

VIKAO VYA MAANDALIZI (KONGAMANO LA UJIRANI MWEMA


VIKAO VYA MAANDALIZI (KONGAMANO LA UJIRANI MWEMA.

Baada ya ya kukutana na wadai na walezi wetu kwa malengo ya kuboresha Kongamano letu, Jumapili ijayo ya tarehe 19/10/2014, tutakuwa na kikao cha kwanza ambacho kitawahusicha wajumbe wote wa Halmashauri ya VIWAWA parokia ya Bunju na Boko, kikao hichi kitafanyikia Parokiani Bunju mara baada ya misa ya Pili ni Muhimu ukiwa mjumbe kuhuzuria, pia Ticketi za ushiriki zitaanza kupatikana hiyo siku tarehe 19/10/2014, kwa Wahazini wote wa Ngazi ya Parokia, Kigango na Jumuiya kwa Tshs 18,000 tu wahi mapema upate ticketi yako. nafasi ni kwa vijana 140 tu

Wednesday, October 8, 2014

Majadiliano ya kidini ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Kanisa!

Adui mkubwa wa mchakato wa majadiliano ya kidini ni woga na wasiwasi usiokuwa na msingi, mambo yanayochangia watu wa dini mbali mbali kushindwa kufahamiana na hatimaye kuishi kwa amani, umoja na udugu kwa kutambua kwamba, wote wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu na hivyo tofauti zao za kidini si sababu msingi ya malumbano na kinzani zisizo na tija wala mashiko kwa watu.

Katika mchakato wa majadiliano ya kidini, Baba Mtakatifu Francisko anaendelea kuhimiza umuhimu wa waamini wa dini mbali mbali kufahamiana. Hii ni kati ya changamoto zilizotolewa na Padre Miguel Angel Ayuso Guixot, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la majadiliano ya kidini pamoja na ujumbe wake walipokuwa wanatembelea na kukutana na viongozi mbali mbali wa kidini nchini Indonesia, ambako kuna idadi kubwa ya waamini wa dini ya Kiislam.

Ujumbe wa Baraza la Kipapa la majadiliano ya kidini, umekumbushia kwamba, majadiliano ya kidini na waamini wa dini mbali mbali ni sehemu ya vinasaba vya Kanisa Katoliki ili kujenga na kudumisha amani, upendo na mshikamano kati ya watu na wala si kwa bahati mbaya kwamba, Kanisa katika mikakati na vipaumbele vyake katika mchakato wa Uinjilishaji linaendelea kukazia majadiliano ya kidini na waamini wa dini mbali mbali duniani. Waamini wanaweza kujenga na kudumisha umoja, udugu na urafiki kwa kusaidiana katika hija ya maisha yao hapa duniani.

Ujumbe wa Vatican nchini Indonesia umepokelewa kwa heshima na taadhima, huo ni ukarimu unaooneshwa na waamini wa dini ya Kiislam wanaoishi huko Indonesia katika ujumla wao. Majadiliano ya kidini kati ya Waislam na Wakristo nchini Indonesia yamejikita katika mang'amuzi na maisha ya kila siku, tofauti kabisa na hali inavyooneshwa na vyombo vya upashanaji habari. Ujumbe wa Vatican umepata nafasi ya kushuhudia na kubadilishana uzoefu na mang'amuzi katika mchakato wa majadiliano ya kidini, ili kujenga na kudumisha misingi ya haki, amani na udugu kati ya watu.

Waamini wa dini ya Kiislam wanaofanya kazi katika taasisi za Kanisa Katoliki wanasema, wanaendelea kufurahia huduma yao na kwamba, wanajisikia wako nyumbani na wala hawajawahi kutengwa wala kunyanyaswa kwa misingi ya kidini. Kila mtu anaheshimiwa kama binadamu na kwamba, tofauti zao za kiimani ni utajiri mkubwa unaoweza kutumika kwa ajili ya kudumisha amani, upendo na mshikamano wa kidugu.


Mkesha wa sala kuombea Sinodi Maalum ya Maaskofu

Jumamosi majira ya saa moja za jioni, makumi ya maelfu ya watu wajumuika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro , kwa ajili ya mkesha wa sala, ulio ongozwa na Baba Mtakatifu Francisko, kuombea Sinodi Maalum ya Maaskofu, ambayo imefunguliwa Jumapili hii kwa Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican. Sinodi hii maalum inachambua changamoto cha Kichungaji katika familia, kwenye muono wa Uinjilishaji .

Katika Mkesha huu wa sala, Baba Mtakatifu Francisko,alitoa wito kwa Waamini wawaombee Mababa wa Sinodi , kwa namna ya pekee, zawadi ya kuisikiliza sauti ya Mungu inavyo waambia na kuwa na moyo wa uwazi katika majadiliano na kukaza macho yao kwa Yesu Kristo.

Kabla ya sala ya Mkesha, kulikuwa na utaratibu wa kusikiliza Neno la Mungu , Maandiko Matakatifu, ushuhuda wa wanandoa, maombi, kuimba na tafakari juu ya maandishi ya Papa Francisco na watangulizi wake.

Baba Mtakatifu alisema, ushirikiano katika maisha ya ndoa, uwazi kwa zawadi ya maisha, kulindana, kuheshimiana, kukutana na kumbukumbu ya vizazi vilivyopita, msaada wa elimu, maambukizi ya imani ya Kikristo kwa watoto wao. . .pamoja na mengine, kwa yote hayo , familia inaendelea kuwa shule iliyosimikwa katika ubinadamu , na mchango muhimu katika haki na umoja katika jamii. (Cf. ibid., N. Evangelii gaudium, 66-68).

Na kwa kadri familia inavyozamisha mzizi wake katika kina kirefu cha umoja wa familia , ndivyo inavyo wezekana maisha hayo kuzama zaidi ndani yake bila kupoteza hisia zake katika mambo mageni. Kwa upeo huo, inatusaidia kufahamu umuhimu wa mkutano huu wa Sinodi Maalum ya Maaskofu, inayofunguliwa kesho.

Zaidi ya yote, Papa alisema, tunaomba Roho Mtakatifu awape Mababa wa Sinodi, zawadi ya kusikiliza, kusikiliza kwa namna ya Kimungu, ili wapate kusikia, pamoja naye, kilio cha watu; kusikiliza kilio cha watu hadi waweze kupumua mapenzi Mungu.

Papa aliomba ili kwamba, Maaskofu waweze kupata zawadi ya kusikiliza kwa makini na uwazi katika majadiliano ya kweli, uwazi wa kidugu, wenye kuwawezesha kulibeba jukumu la Kichungaji, na uwajibikaji kwenye hoja za mabadiliko, yanayojitokeza katika nyakati hizi.

Papa alieleza katika hatua hiyo ya kusikiliza na majadiliano juu ya familia, wakiwa pamoja na Kristo, inakuwa ni tukio la Kikudra ambamo wanaweza kufanya upya utendaji kwa mfano wa Mtakatifu Francisco, kwa Kanisa na jamii.

Pamoja na furaha ya Injili, aliendelea kusema, tutaweza kugundua njia ya mapatano, na huruma ya kanisa katika kuwaona maskini na rafiki wa maskini, kwa nguvu ya kanisa inawezekana, kukua katika uvumilivu na upendo, na kuondokana na hofu na changamoto zake, katika yote, ndani ya kanisa lenyewe na nje yake (Lumen Gentium, 8).

Papa alikamilisha kwa kuomba uvuvio wa Roho Mtakatifu, uvume juu ya kazi za Sinodi na Juu ya Kanisa na juu ya Ubinadamu wote. Uweze kufungua vifundo vyote vinavyozuia watu kukutana mmoja kwa mwingine, kuponya majeraha yanayovuja damu , na kufufua matumaini. Bwana na atupatie mbinu hizi za upendo kama Yesu alivyopenda. Na ili ujumbe wetu uweze kuleta uhai na shauku ya Wamisionari wa kwanza wa Injili.

Washiriki wa sinodi hii, wametoka bara zote tano za dunia kuzungumzia changamoto za Kichungaji kwa familia, katika muono wa Uinjilishaji, ni kama ifuatavyo: Kuna Marais wa Mabaraza ya Maaskofu Katoliki 114, Wakuu wa Makanisa ya Katoliki ya Mashariki 13, Wakuu wa Idara za Curia ya Roma 25, Wajumbe 9 kutoka Sekretariati ya Baraza la kawaida wa Sekretarieti, Katibu Mkuu wa Jimbo la Papa, na katibu mwandamizi, Wajumbe 3 kutoka 3 wanaowakilisha Wakuu wa Mashirika, na wajumbe 26 walioteuliwa na Papa. Washiriki wengine ni pamoja na 8 Mabruda wanane, Wajumbe 38 wakiwa ni wakaguzi, wakimwemo wanandoa 13 wanandoa, na 16 wataalam. Jumla ya idadi ya washiriki wote wa Sinodi ni 253.Sinodi hii ni hatua ya kwanza kwa ajili ya Sinodi ya kawaida ya mwaka kesho 2015, na hivyo itakamilika bila kutoa tamko la mwisho juu yale yaliyojadiliwa, kwa kuwa maoni yatakayotolewa yatafikishwa katika Sinodi ya Kawaida ya mwaka kesho ambayo itatoa hati yenye tamko juu utendaji wa kanisa katika kupambana na changamoto za Kichungaji katika familia.

Monday, October 6, 2014

Maporomoko ya Rusumo - Ngara

haya maporomoko ni ya maji Rusumo Falls
Mto huu unatokea upande wa Tanzania kuingia kwenye haya maporomoko
Maporomoko ya Rusumo-Ngara
Mungu azidi kushukuriwa na kutukuzwa kwa uumbaji




Kipa wa JKT Ruvu, Jackson Chove akiruka juu kuokoa hatari langoni mwake. Ambapo Hii Leo October 05,2014, huko Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Yanga SC wameichapa JKT Ruvu Bao 2-1 na kukwea hadi Nafasi ya 3 ya Ligi Kuu Vodacom
Yanga walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya 32 kupitia Kelvin Yondani na Bao hilo kudumu hadi Haftaimu.

 Dakika ya 73, Haruna Niyonzima aliipatia Yanga SC Bao la Pili lakini JKT Ruvu walipata Bao lao moja katika Dakika za mwishoni Mfungaji akiwa Jabir Aziz.


KONGAMANO NA UJIRANI MWEMA

Kongamano hili litakuwa la Mkesha washiriki watatakiwa kuwasili Parokiani Boko siku ya Ijumaa tarehe 28/11/2014 saa tisa alasiri,na tunatarajia kuwa na semina na midahalo kwa usiku mzima, jumamosi ya tarehe 29/11/2014, saa kumi alasiri washiriki wote watarejea majumbani kwao baada ya kushibishwa kwa semina, midaho na michezo.

Washiriki kwenye Kongamano hili ni Vijana wote wenye Umri kuanzia miaka kumi na nane(18) wa Parokia ya Boko, Bunju na  Vijana wengine kutoka kwenye Parokia Mbali mbali za Jimbo kuu la Dar es  .
MWAKA WA FAMILIA.
Inafurahisha kuona kwamba, wazee wawili na vijana wawili wanakutanishwa na Yesu. Hii
inaonesha kwamba, Yesu ana uwezo wa kukutanisha na kuunganisha vizazi, kwani Yeye ni
chemchemi ya upendo inayovuka ubinafsi, upweke na masikitiko. Baba Mtakatifu anasema,
familia katika hija ya maisha yao wanashirikishana na kumegeana mambo mengi mema:
chakula na mapumziko; kazi za nyumbani, starehe, sala, safari na hija ya maisha ya kiroho
pamoja na matendo ya huruma.
Pale panapokosekana upendo, hapo hukosekana furaha , Upendo wa kweli
unabubujika kutoka kwa Kristo kwa njia ya Neno lake ambalo ni mwanga katika mapito ya
waamini; anawapatia Mkate wa maisha ya uzima wa milele, unaowasaidia waamini kupambana
na changamoto za maisha ya kila siku.
Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Sinodi Maalum ya
Maaskofu kwa ajili ya Familia itakayoadhimishwa Mwezi Oktoba 2014 mjini Vatican, kwa
kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kuhusu familia mintarafu Uinjilishaji"
ameandika barua kwa familia zote duniani ili kukazia dhamana ya Kanisa kuendelea kutangaza
Injili kwa kukabiliana kinaga ubaga na changamoto mpya zinazohusu familia.
Baba Mtakatifu anasema, maandalizi haya yanawahusu Watu wote wa Mungu kwa kuhakikisha
kwamba, wanashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo pamoja na kusindikiza mchakato mzima kwa
njia ya sala, jambo muhimu sana kutoka kwa familia zote. Sinodi hii ni maalum kwa ajili ya: wito
na utume wa Kanisa na Jamii; matatizo yanayowakabili wanandoa; maisha ya kifamilia, elimu
na malezi kwa watoto; dhamana na utume wa familia katika maisha ya Kanisa.
Hivyo nakualika kijana mwenzangu uungane nasi hiyo siku katika kuyachambua haya kwa kina anza sasa kufanya maandalizi

ELIMU YA UJASIRIAMALI.
Elimu ya ujasiriamali katika nchi yetu haina ‘umri’ mkubwa kama zilivyo taaluma nyingine zikiwamo lugha, historia, siasa na sayansi. Hii ni kutokana na historia ya nchi yetu hasa baada ya kupata uhuru, kwamba tuliamua kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea kupitia Azimio la Arusha.
Siasa ya ujamaa na kujitegemea haikushadidia ujasiriamali kwa vile ulifananishwa na ubepari ambao ulichukuliwa kama unyama. Wale wote waliokuwa wanajihusisha na shughuli za kijasiriamali hasa biashara katika kipindi hicho walionekana kama ‘wanyama’ au watu ambao walikuwa wamechepuka kutoka katika njia kuu ambayo ilikuwa inaaminiwa na jamii kubwa wakati huo.
Wafanyakazi serikalini walikuwa hawaruhusiwi kujihusisha na biashara na kwamba shughuli za ujasiriamali zilionekana kufanywa na watu ambao hawakuwa na elimu ya kutosha kupata ajira, na wageni hasa kutoka Bara la Asia kama vile Wahindi.
Hata hivyo, kutokana na hali halisi ya maisha katika nchi yetu na duniani kwa jumla, kwenye miaka ya katikati ya 2000, taifa lilianza utaratibu wa kuingiza elimu ya ujasiriamali katika elimu ingawa haikuwekewa kipaumbele sana. Kwa sasa elimu ya ujasiriamali imekuwa kama wimbo wa taifa, siyo shuleni na vyuoni bali hata katika sekta ambazo si rasmi kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia matangazo mbalimbali juu ya kuendesha elimu ya ujasirimali katika makundi mbalimbali ya jamii yetu.
Kutokana na wanajamii na taifa kwa jumla kuanza kuona elimu ya ujasiriamali kama mwarobaini wa matatizo yanayowakabili kama vile ajira na umaskini, lengo la la Kongamano letu  ni kuelezea umuhimu wa elimu ya ujasiriamali katika Chama chetu cha VIWAWA  kama njia mojawapo yenye kuonyesha jinsi elimu ya ujasiriamali inavyoweza kuisaidia jamii na taifa katika kuleta maendeleo.
Ujasiriamali ni mchakato au hali waliyonayo baadhi ya watu ya kutaka mafanikio yanayoshadadiwa na moyo wa ushindani, kujiamini, uwezo binafsi wa kukabiliana na kutatua changamoto zilizopo ikiwa ni pamoja na uthubutu wa kukabiliana na changamoto ambazo wakati mwingine huweza kuathiri maisha yao katika kipindi cha mpito.
Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kama ujasiriamali hufundishwa au mtu huzaliwa nao ingawa si lengo la kongamano letu si kujikita katika mjadala huo, kwa kuwa tunaelewa nguvu iliyonayo elimu katika kuyatengeneza maisha ya mwanadamu.
Tunaamini kuwa vijana wana maono na matamanio yao katika maisha kama walivyo watu wazima ingawa watu hawa wawili wanaweza kutofautiana hapa na pale kutokana na sababu za umri, mazingira, wakati na uzoefu katika maisha.
Elimu ya ujasiriamali katika Vyama au kikundi  hujenga msingi mzuri wa kujiamini miongoni mwa vijana na hivyo kuwafanya wayakabili maisha bila woga, jambo ambalo litawafanya kufanya kazi zao wanazozipenda kwa umahiri, weledi na kujiamini zaidi.
hivyo basi nakusi sana kuungana nasi katika kupata elimu hiyo, tunatarajia pia kuunda vikundi vya ujasiriamali kwa vijana watano watano na kuwapatia wataalamu watakao wasimamia.
kwa maelezo zaidi tuandikie kupitia viwawaboko@yahoo.com au piga 0713 900 905


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR