Friday, June 21, 2013

ziara ya Mbulu tarehe 26June13

Tumsifu Yesu Kristo,
YAH:SAFARI YA ZIARA YA UINJILISHAJI PAROKIA YA DAUDI JIMBO LA MBULU MKOANI MANYARA.
Husika na kichwa cha habari hapo juu, siku ya jumatano tarehe 26/06/2013, VIWAWA wataanza safari ya kuelekea Jimbo la Mbulu Mkoani Manyara.
Kwanza tunatoa shukrani kwa Wazazi, Walezi, Viongozi wa JNNK kwa ushirikiano mkubwa waliotupatia kwa kuwachangia Vijana na kuwaruhusu kushiriki katika ziara hii.
Safari itaanzia Parokiani Boko saa kumi na moja asubuhi, na tunatarajia kwenda kupumzika katika mji wa Karatu Mkoani Arusha, Siku ya Alhamisi tarehe 27/06/13 tutaenda Ngorongoro na mchana tutafanya ziara katika Parokia ya Endabashi, Jioni tutaenda Parokia ya Mt. Francisco wa Asizi –Kijiji cha Daudi hapo tutakaa mpaka tarehe 29/06/2013. Jumapili Tarehe 30/06/2013 tutaenda Parokia ya Mt. Yosefu Mfanyakazi(JIMBONI), na kushiriki Ibada ya Misa Takatifu na baadaye kukutana na Vijana wenzetu. Jioni tutaanza safari na tutapumzika Karatu na tarehe 01/-7/2013, saa kumi na moja asubuhi tutaanza safari ya kurudi Dar es salaam.
Tuzidi kuombeana katika kufanikisha ziara hii ya kitume. Tunamwomba Mungu aongoze safari yetu, malaika mikaeli mlinzi wa safari atuongoze.
Mapendo..................................................

No comments:

Post a Comment

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR