Kanisa
Katoliki nchini Tanzania linaendelea kuwekeza kikamilifu katika sekta
ya elimu ili kuwasaidia watanzania kuwa na majiundo kamili ili
kukabiliana barabara na changamoto za maisha, ili hatimaye, Tanzania
iweze kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi.
Shirika la Roho Mtakatifu ambalo kwa miaka mingi limewekeza na kuona mafanikio makubwa katika sekta ya elimu nchini Tanzania,
sasa limeanza kujielekeza katika kuanzisha Kitivo cha Sayansi
kitakachokuwa chini ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostino cha Tanzania,
SAUT. Kitivo hiki kitajulikana kama “Marian University College”, kwa kifupi MUCO, ambacho kinajengwa kwenye mji mkongwe wa Bagamoyo, Mkoani Pwani, nchini Tanzania.
Hivi karibuni, Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam
ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo kikuu cha MUCO na kwamba,
mwezi Septemba, 2014 kitaanza kuandikisha wanafunzi, wakati huo huo
ujenzi wa majengo mengine ukiendelea kukamilishwa hatua kwa hatua.
Katika hafla ya kuweka jiwe la msingi, Kardinali Pengo amesema, nchi
ambayo haina wataalam wa sayansi, kwa hakika itachechemea katika
ushindani wa maendeleo na mataifa mengine. Umefika wakati kwa watanzania
kujiekeza zaidi katika masuala ya kisayansi ili kupata maendeleo
endelevu yanayogusa mahitaji msingi ya binadamu: kiroho na kimwili.
Akizungumza katika tukio hili Padre Florentin Mallya, Makamu mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu Afrika
Mashariki amesema, MUCO itaendelea kushirikiana na SAUT, hadi pale
mchakato wa kukiwezesha Chuo kikuu cha MUCO kujitegemea na kuwa Chuo
kikuu kamili. Kuanzishwa kwa MUCO ni kujibu kwa dhati changamoto
inayotolewa na Serikali ya Tanzania kwa sekta binafsi kusaidia mchakato
wa kukuza na kuendeleza sekta ya elimu hususan katika mchepuo wa
sayansi, ili kujibu mahitaji makubwa yanayoendelea kujitokeza ndani na
nje ya Tanzania katika masuala ya elimu.
Huu ni mwendelezo wa
huduma ya elimu inayotolewa na Shirika hili katika shule zake za awali
na sekondari ambazo kwa miaka mingi zimeendelea kupeta nchini Tanzania
kutokana na wanafunzi wanaohitimu katika shule hizi kuwa na kiwango
kikubwa cha ufaulu kwenye mitihani. Wazazi waliokuwa wanahaha
kuwatafutia watoto wao mahali pazuri zaidi pa kusoma, sasa MUCO itakuwa
ni jibu lao makini.
Ni kutokana na changamoto zote hizi, Shirika
la Roho Mtakatifu liliomba ushirikiano na Serikali ya Tanzania ili
kutekeleza azma hii kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya watanzania tangu
shule za msingi hadi chuo kikuu. Shirika linapania kuendelea kutoa
kiwango bora cha
elimu kwa kutambua kwamba, hii ni sehemu ya Uinjilishaji wa kina
unaogusa mahitaji ya mtu mzima: kiroho na kimwili. Shirika linaiomba
Serikali ya Tanzania pamoja na wazazi kuendelea kuonesha mshikamano
katika kufanikisha malengo ya maboresho ya elimu nchini Tanzania.
Tuesday, June 24, 2014
Papa: anayehukumu wengine ni mnafiki, na hujiweka katika katika nafasi ya Mungu
Baba
Mtakatifu Francisko ameonya dhidi ya tabia ya kupenda kuhukumu wengine
bila kutafakari hali zetu wenyewe. Kupenda kujiona sisi tu safi na yule
ni mdhambi. Lakini tukumbuke kipimo kilekile tunacho tumia kuhukumu
wengine, ni hichohicho kitakacho tumika kutuhukumu... Anayehukumu ndugu
yake, naye atahukumiwa kwa njia hiyo hiyo. Mungu ndiye pekee "hakimu".
Na mshutumiwa anaweza daima hutetewa na Yesu. Yesu, Wakili Mkuu wa
Kwanza, na Wakili wa pili ni Roho Mtakatifu. Papa Francisko amesema
katika hotuba yake ya wakati wa Ibada ya Misa, asubuhi Jumatatu ,
katika Kanisa dogo la Mtakatifu Martha, ndani ya Vatican.
Papa Francisko ameonya dhidi ya kuwa watu wa kupenda kuhukumu wengine katika nafasi mbalimbali, kimaisha,au katika uwajibikaji au mamlaka akieleza kwamba jambo kuhukumu ni hatari kwa sababu licha ya kuuumiza wengine, pia, humgeukia mwenyewe na kuishia kuwa mwathirika wa ukosefu wa huruma kwa wengine. Hiki ndicho hutokea katika kuwahukumu wengine.
Papa Francisko alitoa onyo hili, mara baada ya kusoma kifungu cha Injili kuhusu kibanzi na boriti iliyoko katika jicho, akibainisha kwamba , ni wazi inaonyesha mtu anayependa kuhukumu wenzake kuwa anafanya makosa , na huonyesha udhaifu wa mtu wa kushindwa, maana binadamu hana haki ya kumhukumu mtu mwingine kiroho, hakimu ni Mungu peke yake . Kuhukumu wengine ni "unafiki", kama Yesu alivyowaambia kwa mara kadhaa walimu wa sheria, wakati wa matukio kadhaa kwa wakati ule. Na pia ni kwa sababu Papa alieleza, binadamu hutoa hukumu yake harakaharaka, wakati hukumu ya Mungu huchukua muda.
Na hivyo , kutokana na hili , kuhukumu wengine ni makosa , kwa maneno mepesi ni kwa sababu ni kuchukua nafasi isiyokuwa yako. Na si tu ni makosa lakini pia ni kumchanganya mtu. Ni kupagawa na nia kali za kutaka kujitakatifusha, kuonekana kama safi na wengine ni wakosaji , nia zinazowasha moto wa ndani ambazo haziachi nafasi ya utulivu, wa kujitafakari wenyewe. Lakini tunaambiwa kwanza toa boriti katika jicho laki ndipo utoe kibazi kilicho ndani ya ndugu yako.
Homilia ya Papa imesisitiza , mwenye uwezo wa kutoa hukumu ni Mungu peke, na kuongeza, kile kinacho onyesha tabia ya kumtegemea Yesu,ni mfano wake wa kuto hukumu wengne.
Yesu mbele ya Baba, kamwe hakuwatuhumu wengine.Kinyume aliwatetea! Anakuwa Mtetezi wa kwanza. Kisha anampeleka mtetezi wa pili, ambaye ni Roho Mtakatifu. . Yeye ni Wakili mbele ya Baba dhidi ya mashtaka, Papa ameeleza na kuhoji Na ni nani basi mshitaki? Na kutoa jibu la Biblia,kwamba Mshitaki anaitwa Ibilisi , shetani. Na hivyo Mwisho wa Dunia, Yesu atahukumu lakini wakati huo huo ni mwombezi na mtetezi ..
Hatimaye, Papa Francisko , alisema, anayehukumu, humwinga Mkuu wa ulimwengu huu,ibilisi ambaye daima ni nyuma ya watu, akitaka kuwashtaki kwa Baba. Lakini Bwana, atatupa neema ya kumwiga Yesu, wakili na mwanasheria wetu. Na si kuwaiga wengine, ambayo mwisho wao ni huangamiza
Papa ameasa, iwapo tunataka kutembea katika njia ya Yesu, tunapaswa kuwa mawakali watetezi wale wanaotuhumiwa mbele ya Baba. Kwa namna gani tunaweza kuwa watetezi wa wengine wanaoshutumiwa, je ni kuingilia kati mara ? Hapana ni kukaa kimya na kwenda kusali na kumtetea mbele ya Bwana kama Yesu alivyofanya msalabani. Kusali kwa ajili yake na si kuhukumu. Ni vibaya kuhukumu kwa sababu, pia utahukumiwa
Papa aliwataka wote waliokuwa wakimsikiliza kukumbuka hilo siku zote , pale inapokuja hamu ya kutaka kuhukumu wengine , na kusema mabaya ya wengine, kuyashihnda majaribu hayo kwa kusali na kuomba neema ya kusamehe wengine..
Papa Francisko ameonya dhidi ya kuwa watu wa kupenda kuhukumu wengine katika nafasi mbalimbali, kimaisha,au katika uwajibikaji au mamlaka akieleza kwamba jambo kuhukumu ni hatari kwa sababu licha ya kuuumiza wengine, pia, humgeukia mwenyewe na kuishia kuwa mwathirika wa ukosefu wa huruma kwa wengine. Hiki ndicho hutokea katika kuwahukumu wengine.
Papa Francisko alitoa onyo hili, mara baada ya kusoma kifungu cha Injili kuhusu kibanzi na boriti iliyoko katika jicho, akibainisha kwamba , ni wazi inaonyesha mtu anayependa kuhukumu wenzake kuwa anafanya makosa , na huonyesha udhaifu wa mtu wa kushindwa, maana binadamu hana haki ya kumhukumu mtu mwingine kiroho, hakimu ni Mungu peke yake . Kuhukumu wengine ni "unafiki", kama Yesu alivyowaambia kwa mara kadhaa walimu wa sheria, wakati wa matukio kadhaa kwa wakati ule. Na pia ni kwa sababu Papa alieleza, binadamu hutoa hukumu yake harakaharaka, wakati hukumu ya Mungu huchukua muda.
Na hivyo , kutokana na hili , kuhukumu wengine ni makosa , kwa maneno mepesi ni kwa sababu ni kuchukua nafasi isiyokuwa yako. Na si tu ni makosa lakini pia ni kumchanganya mtu. Ni kupagawa na nia kali za kutaka kujitakatifusha, kuonekana kama safi na wengine ni wakosaji , nia zinazowasha moto wa ndani ambazo haziachi nafasi ya utulivu, wa kujitafakari wenyewe. Lakini tunaambiwa kwanza toa boriti katika jicho laki ndipo utoe kibazi kilicho ndani ya ndugu yako.
Homilia ya Papa imesisitiza , mwenye uwezo wa kutoa hukumu ni Mungu peke, na kuongeza, kile kinacho onyesha tabia ya kumtegemea Yesu,ni mfano wake wa kuto hukumu wengne.
Yesu mbele ya Baba, kamwe hakuwatuhumu wengine.Kinyume aliwatetea! Anakuwa Mtetezi wa kwanza. Kisha anampeleka mtetezi wa pili, ambaye ni Roho Mtakatifu. . Yeye ni Wakili mbele ya Baba dhidi ya mashtaka, Papa ameeleza na kuhoji Na ni nani basi mshitaki? Na kutoa jibu la Biblia,kwamba Mshitaki anaitwa Ibilisi , shetani. Na hivyo Mwisho wa Dunia, Yesu atahukumu lakini wakati huo huo ni mwombezi na mtetezi ..
Hatimaye, Papa Francisko , alisema, anayehukumu, humwinga Mkuu wa ulimwengu huu,ibilisi ambaye daima ni nyuma ya watu, akitaka kuwashtaki kwa Baba. Lakini Bwana, atatupa neema ya kumwiga Yesu, wakili na mwanasheria wetu. Na si kuwaiga wengine, ambayo mwisho wao ni huangamiza
Papa ameasa, iwapo tunataka kutembea katika njia ya Yesu, tunapaswa kuwa mawakali watetezi wale wanaotuhumiwa mbele ya Baba. Kwa namna gani tunaweza kuwa watetezi wa wengine wanaoshutumiwa, je ni kuingilia kati mara ? Hapana ni kukaa kimya na kwenda kusali na kumtetea mbele ya Bwana kama Yesu alivyofanya msalabani. Kusali kwa ajili yake na si kuhukumu. Ni vibaya kuhukumu kwa sababu, pia utahukumiwa
Papa aliwataka wote waliokuwa wakimsikiliza kukumbuka hilo siku zote , pale inapokuja hamu ya kutaka kuhukumu wengine , na kusema mabaya ya wengine, kuyashihnda majaribu hayo kwa kusali na kuomba neema ya kusamehe wengine..
Friday, June 20, 2014
MESSAGE OF POPE FRANCIS FOR THE TWENTY-NINTH WORLD YOUTH DAY
MESSAGE OF POPE FRANCIS
FOR THE TWENTY-NINTH WORLD YOUTH DAY
2014
FOR THE TWENTY-NINTH WORLD YOUTH DAY
2014
"Blessed are the
poor in spirit, for theirs is the kingdom of heaven” (Mt 5:3)
Dear Young Friends,
How vividly I recall the
remarkable meeting we had in Rio de Janeiro for the Twenty-eighth World
Youth Day. It was a great
celebration of faith and fellowship! The wonderful people of Brazil welcomed us
with open arms, like the statue of Christ the Redeemer which looks down from
the hill of Corcovado over the magnificent expanse of Copacabana beach. There,
on the seashore, Jesus renewed his call to each one of us to become his
missionary disciples. May we perceive this call as the most important thing in
our lives and share this gift with others, those near and far, even to the
distant geographical and existential peripheries of our world.
The next stop on our
intercontinental youth pilgrimage will be in Krakow in 2016. As a way of
accompanying our journey together, for the next three years I would like to
reflect with you on the Beatitudes found in the Gospel of Saint Matthew
(5:1-12). This year we will begin by reflecting on the first Beatitude:
“Blessed are the poor in spirit, for theirs is the kingdom of heaven” (Mt
5:3). For 2015 I suggest: “Blessed are the pure in heart, for they shall see
God” (Mt 5:8). Then, in 2016, our theme will be: “Blessed are the
merciful, for they shall obtain mercy” (Mt 5:7).
1. The revolutionary
power of the Beatitudes
It is always a joyful
experience for us to read and reflect on the Beatitudes! Jesus proclaimed them
in his first great sermon, preached on the shore of the sea of Galilee. There
was a very large crowd, so Jesus went up on the mountain to teach his
disciples. That is why it is known as “the Sermon on the Mount”. In the Bible,
the mountain is regarded as a place where God reveals himself. Jesus, by
preaching on the mount, reveals himself to be a divine teacher, a new Moses.
What does he tell us? He shows us the way to life, the way that he himself has
taken. Jesus himself is the way, and he proposes this way as the path
to true happiness. Throughout his life, from his birth in the stable in
Bethlehem until his death on the cross and his resurrection, Jesus embodied the
Beatitudes. All the promises of God’s Kingdom were fulfilled in him.
In proclaiming the
Beatitudes, Jesus asks us to follow him and to travel with him along the path
of love, the path that alone leads to eternal life. It is not an easy journey,
yet the Lord promises us his grace and he never abandons us. We face so many
challenges in life: poverty, distress, humiliation, the struggle for justice,
persecutions, the difficulty of daily conversion, the effort to remain faithful
to our call to holiness, and many others. But if we open the door to Jesus and
allow him to be part of our lives, if we share our joys and sorrows with him,
then we will experience the peace and joy that only God, who is infinite love,
can give.
The Beatitudes of Jesus
are new and revolutionary. They present a model of happiness contrary to what
is usually communicated by the media and by the prevailing wisdom. A worldly
way of thinking finds it scandalous that God became one of us and died on a
cross! According to the logic of this world, those whom Jesus proclaimed
blessed are regarded as useless, “losers”. What is glorified is success at any
cost, affluence, the arrogance of power and self-affirmation at the expense of
others.
Jesus challenges us,
young friends, to take seriously his approach to life and to decide which path
is right for us and leads to true joy. This is the great challenge of faith.
Jesus was not afraid to ask his disciples if they truly wanted to follow him or
if they preferred to take another path (cf. Jn 6:67). Simon Peter had
the courage to reply: “Lord, to whom shall we go? You have the words of eternal
life” (Jn 6:68). If you too are able to say “yes” to Jesus, your lives
will become both meaningful and fruitful.
JUMAPILI YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU MASOMO MWAKA A
22
|
JUNI
JUMAPILI YAMWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU
MWAKA "A" 2014
MWAKA "A" 2014
RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI
Zaburi: tazama sala ya siku
Zab:147:12-15. 19-20
K. Msifu Bwana, Ee Yerusalemu
SOMO 1:Kum.8:2-3, 14-16a
Musa aliwaambia makutano:
Utaikumbuka
njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika
jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika
amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana.
Usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu
haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana.
Basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, uliyekutoa katika
nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa
lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji;
aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana,
wasiyoijua baba zao.
SOMO 2:1Kor. 10:16-17
Kikombe kile cha Baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa
damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa maana
sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.
INJILI: Yn.6:51-58
Yesu aliwaambia Wayahudi:
Mimi ndimi
chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki,
ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima
wa ulimwengu. Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu
kutupa sis mwili wake ili tuule? Basi Yesu akawaambia, Amin, Amin, nawaambieni,
msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani
yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu
yangu anao uzima wa milele; name nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili
wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili
wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, name hukaa ndani yake. Kama vile
Baba aliye hai alivyonituma mimi, name ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye
kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si
kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.
MATANGAZO
mara baada ya misa ya pili saa 4:00 asubuhi, Parokiani Boko, Tutakuwa na kikao cha VIjana waote wanaotarajia kushiriki ziara ya uinjilishaji Jimbo la Mbulu Parokia za Dareda, Sanu, Daudi na endabashi, pia kwenda kutembelea mbuga ya Wanyama ya ngorongoro.
Fika na mchango wako ikiwa bado haujamalizia mchango ni tshs 150,000 kwa mshiriki, ziara ni tarehe 01/07 mpaka tarehe 07/07/2014....
Tunawatikia Dominika njema, Amani ya Bwana Iwe nasi.........Mapendo sana,,,,,,,
MAOMO YA YA JUNE 15 SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A
15
|
JUNI
SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU
MWAKA "A" 2014
MWAKA "A" 2014
RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI
Zaburi:Tazama sala ya siku.
Dan.3:52-56
K. Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
SOMO 1:Kut.34:4b-6, 8-9
Musa aliinuka
asubuhi na mapema, naye akakwea katika mlima wa Sinai, kama Bwana alivyomwamuru,
akazichukua hizo mbao mbili za mawe mkononi mwake. Bwana akashuka ndani ya lile
wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana. Bwana akapita
mbele yake, akalitangaza, Bwana , Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye
fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; Musa akafanya haraka,
akainamisha kichwa chake hata nchi, akasujudu. Akasema ikiwa sasa nimepata
neema mbele zako, Bwana, nakuomba, Bwana, uende kati yetu maana ni watu wenye
shingo ngumu; ukasamehe uovu wetu na dhambi yetu, ukatutwae tuwe urithi wako.
SOMO 2:2Kor.13:11-14
Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni
mamoja, make katika Amani; na Mungu wa upendo na Amani atakuwa pamoja nanyi.
Salimianeni kwa busu takatifu. Watakatifu wote wawasalimu. Neema ya Bwana Yesu
Kristo, na pendo la Mungu. Na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.
INJILI:Yn.3:16-18
Yesu alimwambia Nikodemu: kwa maana jinsi hii Mungu
aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanae wa pekee, ili kila mtu amwaminiye
asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma mwana ulimwenguni
ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye
hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la
mwana pekee wa Mungu.
MATANGAZO
mara baada ya misa ya pili saa 4:00 asubuhi, Parokiani Boko, Tutakuwa na kikao cha VIjana waote wanaotarajia kushiriki ziara ya uinjilishaji Jimbo la Mbulu Parokia za Dareda, Sanu, Daudi na endabashi, pia kwenda kutembelea mbuga ya Wanyama ya ngorongoro.
Fika na mchango wako ikiwa bado haujamalizia mchango ni tshs 150,000 kwa mshiriki, ziara ni tarehe 01/07 mpaka tarehe 07/07/2014....
Tunawatikia Dominika njema, Amani ya Bwana Iwe nasi.........Mapendo sana,,,,,,,
Subscribe to:
Posts (Atom)
-
Mkoa wa Njombe ni moja kati ya mikoa Tanzania, ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Ruvuma, Mbeya...
-
Mwandishi wa kitabu cha Kumbukumbu la Torati ambamo tunapata somo la kwanza anatualika kutambua kuwa Mungu haachi kutimiza ahadi yake ya ...
-
Isidore Bakanja, ambaye alitoa maisha yake kwa ajili ya imani ya Kikristo, Akiongozwa na maisha rahisi kama layman Katoliki wakati wa mauaj...