Tuesday, June 24, 2014

Kardinali Pengo aweka jiwe la msingi la Chuo Kikuu MUCO Bagamoyo!

Kanisa Katoliki nchini Tanzania linaendelea kuwekeza kikamilifu katika sekta ya elimu ili kuwasaidia watanzania kuwa na majiundo kamili ili kukabiliana barabara na changamoto za maisha, ili hatimaye, Tanzania iweze kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi.

Shirika la Roho Mtakatifu ambalo kwa miaka mingi limewekeza na kuona mafanikio makubwa katika sekta ya elimu nchini Tanzania, sasa limeanza kujielekeza katika kuanzisha Kitivo cha Sayansi kitakachokuwa chini ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostino cha Tanzania, SAUT. Kitivo hiki kitajulikana kama “Marian University College”, kwa kifupi MUCO, ambacho kinajengwa kwenye mji mkongwe wa Bagamoyo, Mkoani Pwani, nchini Tanzania.

Hivi karibuni, Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo kikuu cha MUCO na kwamba, mwezi Septemba, 2014 kitaanza kuandikisha wanafunzi, wakati huo huo ujenzi wa majengo mengine ukiendelea kukamilishwa hatua kwa hatua. Katika hafla ya kuweka jiwe la msingi, Kardinali Pengo amesema, nchi ambayo haina wataalam wa sayansi, kwa hakika itachechemea katika ushindani wa maendeleo na mataifa mengine. Umefika wakati kwa watanzania kujiekeza zaidi katika masuala ya kisayansi ili kupata maendeleo endelevu yanayogusa mahitaji msingi ya binadamu: kiroho na kimwili.

Akizungumza katika tukio hili Padre Florentin Mallya, Makamu mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu Afrika Mashariki amesema, MUCO itaendelea kushirikiana na SAUT, hadi pale mchakato wa kukiwezesha Chuo kikuu cha MUCO kujitegemea na kuwa Chuo kikuu kamili. Kuanzishwa kwa MUCO ni kujibu kwa dhati changamoto inayotolewa na Serikali ya Tanzania kwa sekta binafsi kusaidia mchakato wa kukuza na kuendeleza sekta ya elimu hususan katika mchepuo wa sayansi, ili kujibu mahitaji makubwa yanayoendelea kujitokeza ndani na nje ya Tanzania katika masuala ya elimu.

Huu ni mwendelezo wa huduma ya elimu inayotolewa na Shirika hili katika shule zake za awali na sekondari ambazo kwa miaka mingi zimeendelea kupeta nchini Tanzania kutokana na wanafunzi wanaohitimu katika shule hizi kuwa na kiwango kikubwa cha ufaulu kwenye mitihani. Wazazi waliokuwa wanahaha kuwatafutia watoto wao mahali pazuri zaidi pa kusoma, sasa MUCO itakuwa ni jibu lao makini.

Ni kutokana na changamoto zote hizi, Shirika la Roho Mtakatifu liliomba ushirikiano na Serikali ya Tanzania ili kutekeleza azma hii kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya watanzania tangu shule za msingi hadi chuo kikuu. Shirika linapania kuendelea kutoa kiwango bora cha elimu kwa kutambua kwamba, hii ni sehemu ya Uinjilishaji wa kina unaogusa mahitaji ya mtu mzima: kiroho na kimwili. Shirika linaiomba Serikali ya Tanzania pamoja na wazazi kuendelea kuonesha mshikamano katika kufanikisha malengo ya maboresho ya elimu nchini Tanzania.

Papa: anayehukumu wengine ni mnafiki, na hujiweka katika katika nafasi ya Mungu

Baba Mtakatifu Francisko ameonya dhidi ya tabia ya kupenda kuhukumu wengine bila kutafakari hali zetu wenyewe. Kupenda kujiona sisi tu safi na yule ni mdhambi. Lakini tukumbuke kipimo kilekile tunacho tumia kuhukumu wengine, ni hichohicho kitakacho tumika kutuhukumu... Anayehukumu ndugu yake, naye atahukumiwa kwa njia hiyo hiyo. Mungu ndiye pekee "hakimu". Na mshutumiwa anaweza daima hutetewa na Yesu. Yesu, Wakili Mkuu wa Kwanza, na Wakili wa pili ni Roho Mtakatifu. Papa Francisko amesema katika hotuba yake ya wakati wa Ibada ya Misa, asubuhi Jumatatu , katika Kanisa dogo la Mtakatifu Martha, ndani ya Vatican.

Papa Francisko ameonya dhidi ya kuwa watu wa kupenda kuhukumu wengine katika nafasi mbalimbali, kimaisha,au katika uwajibikaji au mamlaka akieleza kwamba jambo kuhukumu ni hatari kwa sababu licha ya kuuumiza wengine, pia, humgeukia mwenyewe na kuishia kuwa mwathirika wa ukosefu wa huruma kwa wengine. Hiki ndicho hutokea katika kuwahukumu wengine.
Papa Francisko alitoa onyo hili, mara baada ya kusoma kifungu cha Injili kuhusu kibanzi na boriti iliyoko katika jicho, akibainisha kwamba , ni wazi inaonyesha mtu anayependa kuhukumu wenzake kuwa anafanya makosa , na huonyesha udhaifu wa mtu wa kushindwa, maana binadamu hana haki ya kumhukumu mtu mwingine kiroho, hakimu ni Mungu peke yake . Kuhukumu wengine ni "unafiki", kama Yesu alivyowaambia kwa mara kadhaa walimu wa sheria, wakati wa matukio kadhaa kwa wakati ule. Na pia ni kwa sababu Papa alieleza, binadamu hutoa hukumu yake harakaharaka, wakati hukumu ya Mungu huchukua muda.


Na hivyo , kutokana na hili , kuhukumu wengine ni makosa , kwa maneno mepesi ni kwa sababu ni kuchukua nafasi isiyokuwa yako. Na si tu ni makosa lakini pia ni kumchanganya mtu. Ni kupagawa na nia kali za kutaka kujitakatifusha, kuonekana kama safi na wengine ni wakosaji , nia zinazowasha moto wa ndani ambazo haziachi nafasi ya utulivu, wa kujitafakari wenyewe. Lakini tunaambiwa kwanza toa boriti katika jicho laki ndipo utoe kibazi kilicho ndani ya ndugu yako.

Homilia ya Papa imesisitiza , mwenye uwezo wa kutoa hukumu ni Mungu peke, na kuongeza, kile kinacho onyesha tabia ya kumtegemea Yesu,ni mfano wake wa kuto hukumu wengne.
Yesu mbele ya Baba, kamwe hakuwatuhumu wengine.Kinyume aliwatetea! Anakuwa Mtetezi wa kwanza. Kisha anampeleka mtetezi wa pili, ambaye ni Roho Mtakatifu. . Yeye ni Wakili mbele ya Baba dhidi ya mashtaka, Papa ameeleza na kuhoji Na ni nani basi mshitaki? Na kutoa jibu la Biblia,kwamba Mshitaki anaitwa Ibilisi , shetani. Na hivyo Mwisho wa Dunia, Yesu atahukumu lakini wakati huo huo ni mwombezi na mtetezi ..

Hatimaye, Papa Francisko , alisema, anayehukumu, humwinga Mkuu wa ulimwengu huu,ibilisi ambaye daima ni nyuma ya watu, akitaka kuwashtaki kwa Baba. Lakini Bwana, atatupa neema ya kumwiga Yesu, wakili na mwanasheria wetu. Na si kuwaiga wengine, ambayo mwisho wao ni huangamiza

Papa ameasa, iwapo tunataka kutembea katika njia ya Yesu, tunapaswa kuwa mawakali watetezi wale wanaotuhumiwa mbele ya Baba. Kwa namna gani tunaweza kuwa watetezi wa wengine wanaoshutumiwa, je ni kuingilia kati mara ? Hapana ni kukaa kimya na kwenda kusali na kumtetea mbele ya Bwana kama Yesu alivyofanya msalabani. Kusali kwa ajili yake na si kuhukumu. Ni vibaya kuhukumu kwa sababu, pia utahukumiwa

Papa aliwataka wote waliokuwa wakimsikiliza kukumbuka hilo siku zote , pale inapokuja hamu ya kutaka kuhukumu wengine , na kusema mabaya ya wengine, kuyashihnda majaribu hayo kwa kusali na kuomba neema ya kusamehe wengine..

Friday, June 20, 2014

MESSAGE OF POPE FRANCIS FOR THE TWENTY-NINTH WORLD YOUTH DAY



MESSAGE OF POPE FRANCIS
FOR THE TWENTY-NINTH WORLD YOUTH DAY

2014
"Blessed are the poor in spirit, for theirs is the kingdom of heaven” (Mt 5:3)
Dear Young Friends,
How vividly I recall the remarkable meeting we had in Rio de Janeiro for the Twenty-eighth World Youth Day. It was a great celebration of faith and fellowship! The wonderful people of Brazil welcomed us with open arms, like the statue of Christ the Redeemer which looks down from the hill of Corcovado over the magnificent expanse of Copacabana beach. There, on the seashore, Jesus renewed his call to each one of us to become his missionary disciples. May we perceive this call as the most important thing in our lives and share this gift with others, those near and far, even to the distant geographical and existential peripheries of our world.
The next stop on our intercontinental youth pilgrimage will be in Krakow in 2016. As a way of accompanying our journey together, for the next three years I would like to reflect with you on the Beatitudes found in the Gospel of Saint Matthew (5:1-12). This year we will begin by reflecting on the first Beatitude: “Blessed are the poor in spirit, for theirs is the kingdom of heaven” (Mt 5:3). For 2015 I suggest: “Blessed are the pure in heart, for they shall see God” (Mt 5:8). Then, in 2016, our theme will be: “Blessed are the merciful, for they shall obtain mercy” (Mt 5:7).
1. The revolutionary power of the Beatitudes
It is always a joyful experience for us to read and reflect on the Beatitudes! Jesus proclaimed them in his first great sermon, preached on the shore of the sea of Galilee. There was a very large crowd, so Jesus went up on the mountain to teach his disciples. That is why it is known as “the Sermon on the Mount”. In the Bible, the mountain is regarded as a place where God reveals himself. Jesus, by preaching on the mount, reveals himself to be a divine teacher, a new Moses. What does he tell us? He shows us the way to life, the way that he himself has taken. Jesus himself is the way, and he proposes this way as the path to true happiness. Throughout his life, from his birth in the stable in Bethlehem until his death on the cross and his resurrection, Jesus embodied the Beatitudes. All the promises of God’s Kingdom were fulfilled in him.
In proclaiming the Beatitudes, Jesus asks us to follow him and to travel with him along the path of love, the path that alone leads to eternal life. It is not an easy journey, yet the Lord promises us his grace and he never abandons us. We face so many challenges in life: poverty, distress, humiliation, the struggle for justice, persecutions, the difficulty of daily conversion, the effort to remain faithful to our call to holiness, and many others. But if we open the door to Jesus and allow him to be part of our lives, if we share our joys and sorrows with him, then we will experience the peace and joy that only God, who is infinite love, can give.
The Beatitudes of Jesus are new and revolutionary. They present a model of happiness contrary to what is usually communicated by the media and by the prevailing wisdom. A worldly way of thinking finds it scandalous that God became one of us and died on a cross! According to the logic of this world, those whom Jesus proclaimed blessed are regarded as useless, “losers”. What is glorified is success at any cost, affluence, the arrogance of power and self-affirmation at the expense of others.
Jesus challenges us, young friends, to take seriously his approach to life and to decide which path is right for us and leads to true joy. This is the great challenge of faith. Jesus was not afraid to ask his disciples if they truly wanted to follow him or if they preferred to take another path (cf. Jn 6:67). Simon Peter had the courage to reply: “Lord, to whom shall we go? You have the words of eternal life” (Jn 6:68). If you too are able to say “yes” to Jesus, your lives will become both meaningful and fruitful.

Jiandae na tarehe 1 mpaka 7/7/2014

www.viwawaboko.blogspot.com

JUMAPILI YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU MASOMO MWAKA A



22
   JUNI 
 JUMAPILI YAMWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU
 MWAKA "A" 2014


RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI



Zaburi: tazama sala ya siku
Zab:147:12-15. 19-20
K. Msifu Bwana, Ee Yerusalemu

SOMO 1:Kum.8:2-3, 14-16a
Musa aliwaambia makutano:
         Utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana. Usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, uliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zao.

SOMO 2:1Kor. 10:16-17
Kikombe kile cha Baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

INJILI: Yn.6:51-58
Yesu aliwaambia Wayahudi:
          Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sis mwili wake ili tuule? Basi Yesu akawaambia, Amin, Amin, nawaambieni, msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye  mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; name nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, name hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, name ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.



 MATANGAZO

mara baada ya misa ya pili saa 4:00 asubuhi, Parokiani Boko, Tutakuwa na kikao cha VIjana waote wanaotarajia kushiriki ziara ya uinjilishaji Jimbo la Mbulu Parokia za Dareda, Sanu, Daudi na endabashi, pia kwenda kutembelea mbuga ya Wanyama ya ngorongoro.

Fika na mchango wako ikiwa bado haujamalizia mchango ni tshs 150,000 kwa mshiriki, ziara ni tarehe 01/07 mpaka tarehe 07/07/2014....

Tunawatikia Dominika njema, Amani ya Bwana Iwe nasi.........Mapendo sana,,,,,,, 

MAOMO YA YA JUNE 15 SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A



15
   JUNI 
 SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU
 MWAKA "A" 2014


RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI


Zaburi:Tazama sala ya siku.

Dan.3:52-56
K. Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

SOMO 1:Kut.34:4b-6, 8-9
  Musa aliinuka asubuhi na mapema, naye akakwea katika mlima wa Sinai, kama Bwana alivyomwamuru, akazichukua hizo mbao mbili za mawe mkononi mwake. Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana. Bwana akapita mbele yake, akalitangaza, Bwana , Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; Musa akafanya haraka, akainamisha kichwa chake hata nchi, akasujudu. Akasema ikiwa sasa nimepata neema mbele zako, Bwana, nakuomba, Bwana, uende kati yetu maana ni watu wenye shingo ngumu; ukasamehe uovu wetu na dhambi yetu, ukatutwae tuwe urithi wako.

SOMO 2:2Kor.13:11-14
Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni mamoja, make katika Amani; na Mungu wa upendo na Amani atakuwa pamoja nanyi. Salimianeni kwa busu takatifu. Watakatifu wote wawasalimu. Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu. Na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.

INJILI:Yn.3:16-18
Yesu alimwambia Nikodemu: kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanae wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la mwana pekee wa Mungu.

 

 MATANGAZO

mara baada ya misa ya pili saa 4:00 asubuhi, Parokiani Boko, Tutakuwa na kikao cha VIjana waote wanaotarajia kushiriki ziara ya uinjilishaji Jimbo la Mbulu Parokia za Dareda, Sanu, Daudi na endabashi, pia kwenda kutembelea mbuga ya Wanyama ya ngorongoro.

Fika na mchango wako ikiwa bado haujamalizia mchango ni tshs 150,000 kwa mshiriki, ziara ni tarehe 01/07 mpaka tarehe 07/07/2014....

Tunawatikia Dominika njema, Amani ya Bwana Iwe nasi.........Mapendo sana,,,,,,, 

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR