Monday, October 13, 2014

VIKAO VYA MAANDALIZI (KONGAMANO LA UJIRANI MWEMA


VIKAO VYA MAANDALIZI (KONGAMANO LA UJIRANI MWEMA.

Baada ya ya kukutana na wadai na walezi wetu kwa malengo ya kuboresha Kongamano letu, Jumapili ijayo ya tarehe 19/10/2014, tutakuwa na kikao cha kwanza ambacho kitawahusicha wajumbe wote wa Halmashauri ya VIWAWA parokia ya Bunju na Boko, kikao hichi kitafanyikia Parokiani Bunju mara baada ya misa ya Pili ni Muhimu ukiwa mjumbe kuhuzuria, pia Ticketi za ushiriki zitaanza kupatikana hiyo siku tarehe 19/10/2014, kwa Wahazini wote wa Ngazi ya Parokia, Kigango na Jumuiya kwa Tshs 18,000 tu wahi mapema upate ticketi yako. nafasi ni kwa vijana 140 tu

Wednesday, October 8, 2014

Majadiliano ya kidini ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Kanisa!

Adui mkubwa wa mchakato wa majadiliano ya kidini ni woga na wasiwasi usiokuwa na msingi, mambo yanayochangia watu wa dini mbali mbali kushindwa kufahamiana na hatimaye kuishi kwa amani, umoja na udugu kwa kutambua kwamba, wote wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu na hivyo tofauti zao za kidini si sababu msingi ya malumbano na kinzani zisizo na tija wala mashiko kwa watu.

Katika mchakato wa majadiliano ya kidini, Baba Mtakatifu Francisko anaendelea kuhimiza umuhimu wa waamini wa dini mbali mbali kufahamiana. Hii ni kati ya changamoto zilizotolewa na Padre Miguel Angel Ayuso Guixot, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la majadiliano ya kidini pamoja na ujumbe wake walipokuwa wanatembelea na kukutana na viongozi mbali mbali wa kidini nchini Indonesia, ambako kuna idadi kubwa ya waamini wa dini ya Kiislam.

Ujumbe wa Baraza la Kipapa la majadiliano ya kidini, umekumbushia kwamba, majadiliano ya kidini na waamini wa dini mbali mbali ni sehemu ya vinasaba vya Kanisa Katoliki ili kujenga na kudumisha amani, upendo na mshikamano kati ya watu na wala si kwa bahati mbaya kwamba, Kanisa katika mikakati na vipaumbele vyake katika mchakato wa Uinjilishaji linaendelea kukazia majadiliano ya kidini na waamini wa dini mbali mbali duniani. Waamini wanaweza kujenga na kudumisha umoja, udugu na urafiki kwa kusaidiana katika hija ya maisha yao hapa duniani.

Ujumbe wa Vatican nchini Indonesia umepokelewa kwa heshima na taadhima, huo ni ukarimu unaooneshwa na waamini wa dini ya Kiislam wanaoishi huko Indonesia katika ujumla wao. Majadiliano ya kidini kati ya Waislam na Wakristo nchini Indonesia yamejikita katika mang'amuzi na maisha ya kila siku, tofauti kabisa na hali inavyooneshwa na vyombo vya upashanaji habari. Ujumbe wa Vatican umepata nafasi ya kushuhudia na kubadilishana uzoefu na mang'amuzi katika mchakato wa majadiliano ya kidini, ili kujenga na kudumisha misingi ya haki, amani na udugu kati ya watu.

Waamini wa dini ya Kiislam wanaofanya kazi katika taasisi za Kanisa Katoliki wanasema, wanaendelea kufurahia huduma yao na kwamba, wanajisikia wako nyumbani na wala hawajawahi kutengwa wala kunyanyaswa kwa misingi ya kidini. Kila mtu anaheshimiwa kama binadamu na kwamba, tofauti zao za kiimani ni utajiri mkubwa unaoweza kutumika kwa ajili ya kudumisha amani, upendo na mshikamano wa kidugu.


Mkesha wa sala kuombea Sinodi Maalum ya Maaskofu

Jumamosi majira ya saa moja za jioni, makumi ya maelfu ya watu wajumuika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro , kwa ajili ya mkesha wa sala, ulio ongozwa na Baba Mtakatifu Francisko, kuombea Sinodi Maalum ya Maaskofu, ambayo imefunguliwa Jumapili hii kwa Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican. Sinodi hii maalum inachambua changamoto cha Kichungaji katika familia, kwenye muono wa Uinjilishaji .

Katika Mkesha huu wa sala, Baba Mtakatifu Francisko,alitoa wito kwa Waamini wawaombee Mababa wa Sinodi , kwa namna ya pekee, zawadi ya kuisikiliza sauti ya Mungu inavyo waambia na kuwa na moyo wa uwazi katika majadiliano na kukaza macho yao kwa Yesu Kristo.

Kabla ya sala ya Mkesha, kulikuwa na utaratibu wa kusikiliza Neno la Mungu , Maandiko Matakatifu, ushuhuda wa wanandoa, maombi, kuimba na tafakari juu ya maandishi ya Papa Francisco na watangulizi wake.

Baba Mtakatifu alisema, ushirikiano katika maisha ya ndoa, uwazi kwa zawadi ya maisha, kulindana, kuheshimiana, kukutana na kumbukumbu ya vizazi vilivyopita, msaada wa elimu, maambukizi ya imani ya Kikristo kwa watoto wao. . .pamoja na mengine, kwa yote hayo , familia inaendelea kuwa shule iliyosimikwa katika ubinadamu , na mchango muhimu katika haki na umoja katika jamii. (Cf. ibid., N. Evangelii gaudium, 66-68).

Na kwa kadri familia inavyozamisha mzizi wake katika kina kirefu cha umoja wa familia , ndivyo inavyo wezekana maisha hayo kuzama zaidi ndani yake bila kupoteza hisia zake katika mambo mageni. Kwa upeo huo, inatusaidia kufahamu umuhimu wa mkutano huu wa Sinodi Maalum ya Maaskofu, inayofunguliwa kesho.

Zaidi ya yote, Papa alisema, tunaomba Roho Mtakatifu awape Mababa wa Sinodi, zawadi ya kusikiliza, kusikiliza kwa namna ya Kimungu, ili wapate kusikia, pamoja naye, kilio cha watu; kusikiliza kilio cha watu hadi waweze kupumua mapenzi Mungu.

Papa aliomba ili kwamba, Maaskofu waweze kupata zawadi ya kusikiliza kwa makini na uwazi katika majadiliano ya kweli, uwazi wa kidugu, wenye kuwawezesha kulibeba jukumu la Kichungaji, na uwajibikaji kwenye hoja za mabadiliko, yanayojitokeza katika nyakati hizi.

Papa alieleza katika hatua hiyo ya kusikiliza na majadiliano juu ya familia, wakiwa pamoja na Kristo, inakuwa ni tukio la Kikudra ambamo wanaweza kufanya upya utendaji kwa mfano wa Mtakatifu Francisco, kwa Kanisa na jamii.

Pamoja na furaha ya Injili, aliendelea kusema, tutaweza kugundua njia ya mapatano, na huruma ya kanisa katika kuwaona maskini na rafiki wa maskini, kwa nguvu ya kanisa inawezekana, kukua katika uvumilivu na upendo, na kuondokana na hofu na changamoto zake, katika yote, ndani ya kanisa lenyewe na nje yake (Lumen Gentium, 8).

Papa alikamilisha kwa kuomba uvuvio wa Roho Mtakatifu, uvume juu ya kazi za Sinodi na Juu ya Kanisa na juu ya Ubinadamu wote. Uweze kufungua vifundo vyote vinavyozuia watu kukutana mmoja kwa mwingine, kuponya majeraha yanayovuja damu , na kufufua matumaini. Bwana na atupatie mbinu hizi za upendo kama Yesu alivyopenda. Na ili ujumbe wetu uweze kuleta uhai na shauku ya Wamisionari wa kwanza wa Injili.

Washiriki wa sinodi hii, wametoka bara zote tano za dunia kuzungumzia changamoto za Kichungaji kwa familia, katika muono wa Uinjilishaji, ni kama ifuatavyo: Kuna Marais wa Mabaraza ya Maaskofu Katoliki 114, Wakuu wa Makanisa ya Katoliki ya Mashariki 13, Wakuu wa Idara za Curia ya Roma 25, Wajumbe 9 kutoka Sekretariati ya Baraza la kawaida wa Sekretarieti, Katibu Mkuu wa Jimbo la Papa, na katibu mwandamizi, Wajumbe 3 kutoka 3 wanaowakilisha Wakuu wa Mashirika, na wajumbe 26 walioteuliwa na Papa. Washiriki wengine ni pamoja na 8 Mabruda wanane, Wajumbe 38 wakiwa ni wakaguzi, wakimwemo wanandoa 13 wanandoa, na 16 wataalam. Jumla ya idadi ya washiriki wote wa Sinodi ni 253.Sinodi hii ni hatua ya kwanza kwa ajili ya Sinodi ya kawaida ya mwaka kesho 2015, na hivyo itakamilika bila kutoa tamko la mwisho juu yale yaliyojadiliwa, kwa kuwa maoni yatakayotolewa yatafikishwa katika Sinodi ya Kawaida ya mwaka kesho ambayo itatoa hati yenye tamko juu utendaji wa kanisa katika kupambana na changamoto za Kichungaji katika familia.

Monday, October 6, 2014

Maporomoko ya Rusumo - Ngara

haya maporomoko ni ya maji Rusumo Falls
Mto huu unatokea upande wa Tanzania kuingia kwenye haya maporomoko
Maporomoko ya Rusumo-Ngara
Mungu azidi kushukuriwa na kutukuzwa kwa uumbaji




Kipa wa JKT Ruvu, Jackson Chove akiruka juu kuokoa hatari langoni mwake. Ambapo Hii Leo October 05,2014, huko Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Yanga SC wameichapa JKT Ruvu Bao 2-1 na kukwea hadi Nafasi ya 3 ya Ligi Kuu Vodacom
Yanga walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya 32 kupitia Kelvin Yondani na Bao hilo kudumu hadi Haftaimu.

 Dakika ya 73, Haruna Niyonzima aliipatia Yanga SC Bao la Pili lakini JKT Ruvu walipata Bao lao moja katika Dakika za mwishoni Mfungaji akiwa Jabir Aziz.


KONGAMANO NA UJIRANI MWEMA

Kongamano hili litakuwa la Mkesha washiriki watatakiwa kuwasili Parokiani Boko siku ya Ijumaa tarehe 28/11/2014 saa tisa alasiri,na tunatarajia kuwa na semina na midahalo kwa usiku mzima, jumamosi ya tarehe 29/11/2014, saa kumi alasiri washiriki wote watarejea majumbani kwao baada ya kushibishwa kwa semina, midaho na michezo.

Washiriki kwenye Kongamano hili ni Vijana wote wenye Umri kuanzia miaka kumi na nane(18) wa Parokia ya Boko, Bunju na  Vijana wengine kutoka kwenye Parokia Mbali mbali za Jimbo kuu la Dar es  .
MWAKA WA FAMILIA.
Inafurahisha kuona kwamba, wazee wawili na vijana wawili wanakutanishwa na Yesu. Hii
inaonesha kwamba, Yesu ana uwezo wa kukutanisha na kuunganisha vizazi, kwani Yeye ni
chemchemi ya upendo inayovuka ubinafsi, upweke na masikitiko. Baba Mtakatifu anasema,
familia katika hija ya maisha yao wanashirikishana na kumegeana mambo mengi mema:
chakula na mapumziko; kazi za nyumbani, starehe, sala, safari na hija ya maisha ya kiroho
pamoja na matendo ya huruma.
Pale panapokosekana upendo, hapo hukosekana furaha , Upendo wa kweli
unabubujika kutoka kwa Kristo kwa njia ya Neno lake ambalo ni mwanga katika mapito ya
waamini; anawapatia Mkate wa maisha ya uzima wa milele, unaowasaidia waamini kupambana
na changamoto za maisha ya kila siku.
Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Sinodi Maalum ya
Maaskofu kwa ajili ya Familia itakayoadhimishwa Mwezi Oktoba 2014 mjini Vatican, kwa
kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kuhusu familia mintarafu Uinjilishaji"
ameandika barua kwa familia zote duniani ili kukazia dhamana ya Kanisa kuendelea kutangaza
Injili kwa kukabiliana kinaga ubaga na changamoto mpya zinazohusu familia.
Baba Mtakatifu anasema, maandalizi haya yanawahusu Watu wote wa Mungu kwa kuhakikisha
kwamba, wanashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo pamoja na kusindikiza mchakato mzima kwa
njia ya sala, jambo muhimu sana kutoka kwa familia zote. Sinodi hii ni maalum kwa ajili ya: wito
na utume wa Kanisa na Jamii; matatizo yanayowakabili wanandoa; maisha ya kifamilia, elimu
na malezi kwa watoto; dhamana na utume wa familia katika maisha ya Kanisa.
Hivyo nakualika kijana mwenzangu uungane nasi hiyo siku katika kuyachambua haya kwa kina anza sasa kufanya maandalizi

ELIMU YA UJASIRIAMALI.
Elimu ya ujasiriamali katika nchi yetu haina ‘umri’ mkubwa kama zilivyo taaluma nyingine zikiwamo lugha, historia, siasa na sayansi. Hii ni kutokana na historia ya nchi yetu hasa baada ya kupata uhuru, kwamba tuliamua kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea kupitia Azimio la Arusha.
Siasa ya ujamaa na kujitegemea haikushadidia ujasiriamali kwa vile ulifananishwa na ubepari ambao ulichukuliwa kama unyama. Wale wote waliokuwa wanajihusisha na shughuli za kijasiriamali hasa biashara katika kipindi hicho walionekana kama ‘wanyama’ au watu ambao walikuwa wamechepuka kutoka katika njia kuu ambayo ilikuwa inaaminiwa na jamii kubwa wakati huo.
Wafanyakazi serikalini walikuwa hawaruhusiwi kujihusisha na biashara na kwamba shughuli za ujasiriamali zilionekana kufanywa na watu ambao hawakuwa na elimu ya kutosha kupata ajira, na wageni hasa kutoka Bara la Asia kama vile Wahindi.
Hata hivyo, kutokana na hali halisi ya maisha katika nchi yetu na duniani kwa jumla, kwenye miaka ya katikati ya 2000, taifa lilianza utaratibu wa kuingiza elimu ya ujasiriamali katika elimu ingawa haikuwekewa kipaumbele sana. Kwa sasa elimu ya ujasiriamali imekuwa kama wimbo wa taifa, siyo shuleni na vyuoni bali hata katika sekta ambazo si rasmi kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia matangazo mbalimbali juu ya kuendesha elimu ya ujasirimali katika makundi mbalimbali ya jamii yetu.
Kutokana na wanajamii na taifa kwa jumla kuanza kuona elimu ya ujasiriamali kama mwarobaini wa matatizo yanayowakabili kama vile ajira na umaskini, lengo la la Kongamano letu  ni kuelezea umuhimu wa elimu ya ujasiriamali katika Chama chetu cha VIWAWA  kama njia mojawapo yenye kuonyesha jinsi elimu ya ujasiriamali inavyoweza kuisaidia jamii na taifa katika kuleta maendeleo.
Ujasiriamali ni mchakato au hali waliyonayo baadhi ya watu ya kutaka mafanikio yanayoshadadiwa na moyo wa ushindani, kujiamini, uwezo binafsi wa kukabiliana na kutatua changamoto zilizopo ikiwa ni pamoja na uthubutu wa kukabiliana na changamoto ambazo wakati mwingine huweza kuathiri maisha yao katika kipindi cha mpito.
Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kama ujasiriamali hufundishwa au mtu huzaliwa nao ingawa si lengo la kongamano letu si kujikita katika mjadala huo, kwa kuwa tunaelewa nguvu iliyonayo elimu katika kuyatengeneza maisha ya mwanadamu.
Tunaamini kuwa vijana wana maono na matamanio yao katika maisha kama walivyo watu wazima ingawa watu hawa wawili wanaweza kutofautiana hapa na pale kutokana na sababu za umri, mazingira, wakati na uzoefu katika maisha.
Elimu ya ujasiriamali katika Vyama au kikundi  hujenga msingi mzuri wa kujiamini miongoni mwa vijana na hivyo kuwafanya wayakabili maisha bila woga, jambo ambalo litawafanya kufanya kazi zao wanazozipenda kwa umahiri, weledi na kujiamini zaidi.
hivyo basi nakusi sana kuungana nasi katika kupata elimu hiyo, tunatarajia pia kuunda vikundi vya ujasiriamali kwa vijana watano watano na kuwapatia wataalamu watakao wasimamia.
kwa maelezo zaidi tuandikie kupitia viwawaboko@yahoo.com au piga 0713 900 905


Sunday, October 5, 2014

Maomo ya tarehe 05 October 2014 dominika ya 27 Mwaka "A" wa kanisa

05
 October
 JUMAPILI YA 27 YA MWAKA "A" 2014.


RATIBA ZA IBADA

KIGANGO CHA BOKO.
Kutakuwa na ibada ya Kipaimara itakuwa saa 5:00 asubuhi na itaongozwa na Askofu Mdoe.

IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI.

IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI.

KIGANGO CHA MBWENI.
Kutakuwa na Ibada moja saa: 1:15 – 2:55 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
Ibada itakuwa Moja tu: 1:00 – 2:55 ASUBUHI

KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA itakuwa asubuhi;

SOMO  1. Isa. 5:1-7

Somo katika  kitabu cha Nabii Isaya.
Na nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi 

wangu katika habari za shamba lake la mizabibu.
Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu, 
Kilimani penye kuzaa sana; 
Akafanya handaki kulizunguka pande zote, 
Akatoa mawe yake, 
Akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri,
Akajenga mnara katikati yake, 
Akachimba shinikizo ndani yake;
Akatumaini ya kuwa utazaa mzabibu, 
Nao ukaza zabibu-mwitu. 
Na sasa, enyi wenyeji wa Yerusalemu, nanyi watu wa Yuda, amueni, nawasihi, kati ya mimi na shamba langu la mizabibu. Je! ni kazi gani iliyoweza kutendeka ndani ya shamba langu la mizabibu nisiyoitenda? Basi, nilipotumaini ya kuwa litazaa zabibu, mbona lilizaa zabibu-mwitu? Haya basi, sasa nitawaambieni nitakalolitenda shamba langu la mizabibu; nitaondoa kitalu chake, nalo litaliwa; nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa; nami nitaliharibu, wala halitapogolewa wala kulimwa, bali litamea mbigili na miiba; nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake. kwa maana shamba la mizabibu la Bwana wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza; akatumaini kuona hukumu ya haki, na kumbe! aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na kumbe! alisikia kilio.


SOMO  2. Flp. 4:6-9
Somo katika waraka wa mtume Paulo kwa Wafilipi.
Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zujulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. Hatimaye, ndugu zangu,  mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote. yatafakarini hayo. Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.



  INJILI.Mt. 21:33-43

Somo katika Injili ilivyoandikwa na Mathayo.


Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee wa watu, Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu mwenye nyumba, naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri. Wakati wa matunda ulipokuwa karibu, akawatuma watumwa wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake. Wale wakulima wakawakamata watumwa wake, huyu wakampiga, na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe, Akawatuma tena watumwa wengine wengi kuliko wa kwanza, wakawatenda vile vile. Mwishowe akamtuma mwanae kwao, akisema, Watamstahi mwanangu. Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi; haya na tumwue, tuutwae urithi wake. wakamkamata wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi atakapokuja yule Bwana wa shamba la mizabibu. atawatendaje wale wakulima? wakamwambia, Atawaangamiza vibaya wale wabaya; na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake. Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko,
Jiwe walilolikataa waashi,
Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni;
Neno hili limetoka kwa Bwana,
Nalo ni ajabu machoni petu?
kwa sababu hiyo nawaambia, ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.

Matangazo


 
 

 


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR