Tuesday, November 18, 2014

Ni kwanini vijana wanaogopa ndoa (kwanini vijana hawataki kuanzisha kanisa dogo)

kuelekea kwenye semina ya Mwaka wa familia tarehe 28-29/11/2014. vijana wanaandaliwa kujenga familia Bora familia ya Kikristo, familia ambayo ni kanisa Dogo, kanisa la nyumbani
 
Matunda ya familia bora ni kuwa na Imani, mapendo na matumaini miongoni kwa wanafamilia, kazi mbayo ni kubwa, familia ilikabiliana na kinzani pamoja na changamoto kubwa za kitamaduni, lakini imani ikaendelea kukua na kuota mizizi katika familia zetu,

tunu za maisingi ya Kikristo kuleta mabadiliko miongoni mwa wa vijana ambao walianza kupata malezi hayo tokea utotoni ,hapo ndipo huibuka miito ya  kipadre na kitawa, neema na baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
 

Kwa sasa vijana  tunaendelea kukabiliana na changamoto mbali mbali katika maisha, hasa kutokana na ongezeko la umaskini, hali ambayo inazifanya familia nyingi kutafuta njia za mkato; mambo ambayo wakati mwingine yanahatarisha imani na matokeo yake ni watu kukata tamaa. Baba Mtakatifu anasema, Familia inapaswa kupewa kipaumbele cha kwanza kwani ni msingi wa Jamii, mahali ambapo watu wanajifunza kuishi kwa pamoja, licha ya tofauti zao msingi na kwamba ni mahali pa kurithisha imani, dhamana inayotekelezwa na wazazi. Familia ni madhabahu ya Injili ya Uhai, inayopaswa kudumishwa na kuendelezwa.

Wanandoa ambao wengi ni wazazi wetu na vijana wenzetu wadumishe uaminifu na mapendo ya ndoa, wasaidie majiundo ya kina kwa watoto wao sanjari na kudumisha tunu msingi za maisha ya ndoa na familia yanayojikita katika Mafundisho tanzu ya Kanisa na kumwilishwa katika uhalisia wa maisha, ili kuwa kivutio kwa vijana wanajianda kuingia kwenye wito huo.

Viongozi wa Kanisa waendelee kuwa karibu zaidi na vijana katika malezi na makuzi yao, ili waweze kuwa na utambulisho makini, tayari kushiriki katika kazi ya uumbaji kwa kujikita katika wito wa ndoa au Daraja takatifu au maisha ya kitawa kwa ajili ya wokovu wa roho za watu. Vijana wafundwe kuchuchumilia usafi wa moyo pamoja na kukuza ushirikiano miongoni mwa utume wa vijana wa Parokia hizi, ili wote waweze kujisikia kuwa wako ndani ya Familia ambayo kimsingi ni Kanisa dogo la nyumbani.
...bonjeza hapa Kuendelea kusoma hapa


Mwaka wa Katekesi Jimbo Katoliki Ifakara

Mwaka wa Imani uliotangazwa na kuzinduliwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita na kuhitimishwa kwa kishindo kikuu na Papa Francisko, lilikuwa ni tukio la neema kubwa kwa maisha na utume wa Kanisa. Ilikuwa ni nafasi kwa waamini kupitia tena Mafundisho ya Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican, ili kuweza kuyapyaisha katika uhalisia wa maisha na utume wa Kanisa katika ulimwengu mamboleo.

Mwaka wa Imani, ulikwenda sanjari na maadhimisho ya miaka 20 tangu Mtakatifu Yohane Paulo II alipochapisha kwa mara ya kwanza Katekesi Mpya ya Kanisa Katoliki, bila kusahau Kitabu cha Sheria za Kanisa; matunda makuu ya Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican. Waamini kwa namna ya pekee kabisa walihamasishwa kufanya tafakari ya kina kuhusu Imani wanayoungama katika Fumbo la Utatu Mtakatifu, Kanisa na Mambo ya nyakati.

Waamini walihimizwa kutambua umuhimu wa maadhimisho ya Sakramenti za Kanisa, ili waweze kushiriki kikamilifu na hatimaye kujipatia neema na baraka zinazotolewa na Mama Kanisa. Mwaka wa imani, ulikuwa ni nafasi kwa waamini kujikita katika ushuhuda unaoonesha imani tendaji kwa kukumbatia Amri za Mungu kama dira na mwongozo wa maisha yao ya kiroho na maisha ya hadhara.

Waamini kwa mara nyingine tena, walihimizwa na Mama Kanisa kumwilisha imani yao kwa Kristo na Kanisa lake kwa njia ya Sala na Matendo ya huruma. Kwa maneno machache, Mwaka wa Imani, ilikuwa ni fursa ya kutafakari kwa kina na mapana kuhusu: Imani, Sakramenti za Kanisa, Amri za Mungu na Maisha ya Sala. Mwaka wa Imani, kimekuwa ni kipindi cha neema ambacho kimeyasaidia Makanisa mahalia kujiwekea mbinu mkakati wa kuimarisha imani kwa njia ya Sinodi za Majimbo au Mwendelezo wa Maadhimosho ya Mwaka wa Imani kwa kuchagua mada mbali mbali kadiri ya mahitaji ya Kanisa mahalia.

Askofu Salutaris Melchior Libena wa Jimbo Katoliki la Ifarakara, Tanzania, katika mahojiano maalum na Gazeti la AMECEA anasema kwamba, mara baada ya kuadhimisha Mwaka wa Imani, kulionekana kwamba, kunahitaji la kuendelea kuwaimarisha waamini katika Mafundisho tanzu ya Kanisa kwa kujikita hasa zaidi katika Katekesi ya kina, zoezi la kiroho linaloigusa Familia ya Mungu Jimboni Ifakara.
http://viwawaboko.blogspot.com/p/mak.htmlKutokana na hitaji hili msingi, Jimbo Katoliki la Ifakara hapo tarehe 19 Marchi 2013, katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Mtakatifu Yosefu mchumba wake Bikira Maria na Msimamizi wa Kanisa la Kiulimwengu, Askofu Libena akazindua Mwaka wa Katekesi Jimbo Katoliki Ifarakara, utakaofungwa rasmi hapo tarehe 19 Marchi 2015, Jimbo Katoliki Ifakara litakapokuwa linaadhimisha Mwaka wa Tatu tangu kuundwa kwake na Baba Mtkatifu mstaafu Benedikto XVI. Ifakara ni kati ya majimbo machanga sana nchini Tanzania, lakini linaendelea kucharuka kwa maendeleo ya watu kiroho na kimwili.

Askofu Libena anasema, Mwaka wa Katekesi umekuwa ni fursa kubwa kwa Familia ya Mungu Jimboni Ifakara kuweza kupyaisha tena mafundisho tangu ya Kanisa, dhamana inayotekelezwa kuanzia kwenye ngazi ya: Familia, Jumuiya ndogo ndogo za Kikristo, Vigango, Parokia na katika ngazi ya Jimbo. Lengo ni kuhakikisha kwamba, Jimbo Katoliki Ifakara litakapokuwa linaadhimisha kumbu kumbu ya miaka mitatu tangu kuundwa kwake, waamini wawe wameifahamu Katekesi kwa kina na mapana yake.

Jimbo Katoliki Ifakara linapenda kumwilisha imani katika matendo kwa kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu ambayo kwa sasa inaonekana inahitaji kupewa uzito wa pekee kutokana na ukweli kwamba, kwa masuala ya afya, Jimbo limejiimarisha kwani kuna Hospitali ya Rufaa yenye vitanda 370 na idadi nzuri ya Zahanati ambazo zinaendelea kutoa huduma bora kwa kuzingatia utu na heshima ya binadamu.

Jimbo Katoliki la Ifakara linamiliki na kuendesha shule kadhaa za msingi, lakini kwa bahati mbaya, linamiliki Sekondari moja tu, changamoto ya kuendelea kuwekeza katika elimu, ili kuweza kuwafunda vijana wa kizazi kipya: kiroho na kimwili, tayari kulitumikia Taifa na Kanisa kwa ujumla.

Itakumbukwa kwamba, Jimbo Katoliki la Ifakara liliundwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI kunako tarehe 14 Januari 2012 na kuzinduliwa rasmi tarehe 19 Marchi 2012 na Askofu Salutarius Libena akawa ni Askofu wa kwanza wa Jimbo Katoliki Ifakara:>>>>>bonyeza hapa soma zaidi hapa

Monday, November 10, 2014

semina ya awali ya kongamano la ujirani mwema yawa chachu ya maandalizi

Mkufunzi wa Semina ya Utawala Bora na Ujasiriamali, Ndugu Dniho alisema juzi kwenye ufunguzi wa semina kuwa; vijana ni tumaini la Kanisa na Jamii kwa ujumla.  
  
Jambo la kusikitisha ni kuona kwamba, kuna kundi kubwa la vijana wanaokimbilia mijini kutafuta riziki ya maisha, lakini mazingira wanamoishi ni hatari na ya kukatisha tamaa kiasi kwamba, vijana wanakosa dira na mwelekeo katika maisha.

Majiundo na malezi makini ni muhimu sana kwa vijana, ili kuwajengea uwezo wa kushiriki kikamilifu katika ustawi na maendeleo ya Jamii zao. Elimu ni ufunguo wa maendeleo na matumaini kwa vijana, lakini kuna haja ya kuwezeka na kuboresha zaidi mfumo wa elimu nchini Tanzania ili vijana waweze kuelimishwa barabara, kwani wao ni matumaini ya leo na kesho iliyo bora zaidi.

Shule za kata au sekondari zisiwe ni "mazizi" ya kuwakusanyia wanafunzi, bali mahali maalum pa vijana kuweza kupata: ujuzi, maarifa, maadili na utu wema. Hii ni changamoto kwa wadau mbali mbali wa elimu nchini Tanzania, kuhakikisha kwamba, wanafanya maboresho makubwa katika mfumo wa elimu, kwani matokeo ya mitihani ya hivi karibuni ni aibu kubwa kwa taifa linalotaka kuwekeza kwa vijana. 

Walimu wanapaswa kutambua dhamana na wajibu wao katika malezi na makuzi ya vijana wanapokuwa shuleni. Watambue kwamba, wana mchango mkubwa katika utoaji wa majiundo makini kwa vijana wa kizazi kipya. .
Ndugu Dniho, anasema kwamba, watanzania wengi ni watu wa kawaida kumbe, hawana uwezo wa kuwapeleka watoto wao katika shule za binafsi. Vijana popote pale walipo wahakikishiwe kwamba, wanapata elimu bora na wala si bora elimu ili kuweza kupambana na mazingira pamoja na changamoto za maisha kwa siku za usoni. Hii inatokana na ukweli kwamba, elimu ndiye mkombozi wa maskini!

Katika Maadhimisho ya Mwaka wa Familia, Mama Kanisa anaendelea kukazia umuhimu wa malezi bora kwa vijana katika Familia , ili waweze kuja kuwa na Familia bora zenye misingi ya Imani ya  Kristo na Kanisa lake. Mikakati ya malezi ya vijana ipewe msukumo wa pekee katika ngazi mbali mbali za maisha na utume wa Kanisa.

Vijana wakifundwa barabara na kuwa ni Wakristo wema, hapana shaka kwamba, watakuwa pia ni raia wema watakaojenga na kuimarisha misingi bora ya kifamilia, hapa familia zitakuwa ni viota vya miito mbali mbali ndani ya Kanisa. Malezi bora na makini ni ujenzi wa Jamii bora kwa sasa na kwa siku za usoni.

Ndugu Dniho, anasema, vijana wasaidiwe kuwa ni watu kadiri ya mpango wa Mungu. Jamii na Kanisa ni wadau wakubwa katika ujenzi wa vijana wa kizazi kipya katika medani mbali mbali za maisha. Elimu na malezi bora yapewe msukumo wa pekee katika maisha ya vijana.
Ndugu Kijana Nazidi kukualika uungane nasi Siku ya Ijumaa tarehe 28/11 mpaka Jumamosi tahere 29/11/2014 kwenye semina Muhimu sana ya Mwaka wa Familia na Elimu ya Ujasiriamali.

Sunday, November 2, 2014

Tabia ya Waamini kuvaa nusu Uchi kanisani

waamnini wanaopenda kuvaa mavazi mafupi kanisani
 
Waumini wa kanisa katoliki la St. Francis mjini Diani kusini mwa pwani ya Kenya walipigwa na butwaa baada ya baadhi yao kuzuiwa kuingia katika kanisa hilo kutokana na mavazi yao yaliokuwa nusu uchi.
Julia baraza ambaye alikuwa amevalia kisibao ,ukanda wa manjano na viatu vyenye kisigino kirefu alishangazwa na sheria hizo mpya ambazo zilimsababisha kukosa misa ya asaubuhi.
Kulingana na gazeti la the standard nchini kenya,Julia alisema kuwa watu wawili walimsimamisha nje ya mlango wa kanisa hilo na kumwambia kwamba mtindo wake wa mavazi ulipigwa marufuku katika kanisa hilo na kwamba ametakiwa kuvaa mavazi ya heshima.
Aidha wasichana waliokuwa wamevalia suruali walilazimishwa kujifunga leso juu yake.
Julia alisema kwamba iwapo makanisa yataanza kufuata sheria kama hizo basi wengi hawatahudhuria maombi.
Baadhi ya waumini wamesema kuwa mhubiri wa kanisa hilo aliyejulikana kama Joseph pekee alikuwa ametangaza katika ibada ya awali kwamba mavazi yasio ya heshima hayatakubalika katika kanisa hilo.

Van Gaal aapa kuishinda Mancity (Man City vs Man u)


Meneja wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal anaamini kwamba timu yake itatumia fursa ya kushuka kwa soka ya kilabu ya Manchester City katika uwanja wa Etihad kuishinda kilabu hiyo.
Kilabu ya Manchester City imepoteza mechi zake mbili za mwisho baada ya kushindwa na West Ham na Newcastle.
''Kile tulichokiona katika mechi mbili za mwisho si matokeo ya kuridhisha,alisema Van Gaal.
''Tuna hisia njema kuhusu mechi hii''.''Tunahitaji matokeo mazuri na huenda yakawa dhidi ya Manchester City''.Aliongezea Van Gaal.
Timu za mancity na man United katika derby 
City iko katika nafasi ya tatu wakiwa nyuma kwa alama sita dhidi ya Chelsea.
Tangu ipoteze kwa mabao 5-3 dhidi ya Leicester mnamo Septemba 21,Manchester United haijapoteza na huenda ikaikaribia Mancity katika nafasi ya nne iwapo itashinda mchuano huu wa 'Derby'.
Hatahivyo ushindi dhidi ya Manchester United utakuwa wa nne kati ya timu hizo mbili hatua ambayo haijaafikiwa kwa takriban miaka 44 na timu hiyo.

Siku ya Marehemu tarehe 02/11(Mungu amewekeza siri ya upendo katika Fumbo la KIFO!)

Kifo ni kitendawili ambacho binadamu ameshindwa kabisa kukitegua. Anabaki kuhoji na kujihoji bila kupata jibu la kwa nini anakufa. Mbele ya kifo binadamu anabaki kutoa visingizio vya kujitetea na kulaumu, hatimaye anakiona kifo kuwa mwiko

Zamani mwiko ulikuwa masuala ya „mapenzi”, kumbe kifo na misiba hakikuwa kitu cha kuogopa sana. Lakini sasa ni kinyume, mambo ya mapenzi yamegeuka kuwa kitu cha kawaida kabisa isipokuwa kifo kimekuwa kiboko chetu.

Watu tunakiogopa na pengine hatutaki hata kukisikia. Tunapolazimika kwenda msiba basi tunawaachia wengine walipambe jeneza maua, nasi tukisubiri kwenda kutia sahihi kwenye kitabu cha maombolezo na kutoa rambirambi kwenye bahasha kisha kukaa mbani na jeneza huku tukizungumza chinichini. Sanasana tunajisahaulisha kwa kuimba nyimbo za maombolezo au kusikiliza nyimbo za Injili. Tunaogopa kabisa kukizungumzia kifo au walau kukijadili. Mbele ya kifo binadamu tunabaki kulaumiana, kushikana uchawi na hasa tunamlaumu Mwenyezi Mungu.

Mathalani, kuna baadhi ya wakristu wa kale hata wa sasa walisali na kuomba msaada kwa Mungu au kwa kupitia watakatifu fulani kusudi waepushwe na kifo. Sala hizo zinapoacha kupokelewa, binadamu anachukia, na kumlaumu Mungu. Kristu aliwahi pia kulaumiwa pale alipokataa mwito wa Marta na Maria walipomwomba aenda kwao kumponyesha kaka yao Lazaro aliyekuwa mgonjwa. Yesu akaenda huko kwa kuchelewa kusudi siku nne baada ya kifo. Siku ile alipojionesha msibani, Maria na Marta wakamjia juu na kumlaumu sana. “Bwana ungalikuwapo ndugu yetu asingalikufa”. Hata katika nafasi hiyo, bado hatutaki kulijibu swali ni sababu gani Yesu alifika duniani. Je Yesu alifika duniani ili kuendeleza uhai huu wa kibaolojia au kushinda mauti?

Tukitaka kujua ukweli wa mwenendo mzima wa maisha yetu, hatuna budi kuangalia pia hatima yake, yaani kuelewa kwamba maisha yetu yana mwanzo (yaani kuzaliwa) na yana ukamilifu wake. Ama sivyo tutaendelea kukiogopa kifo, nacho kitaendelea kupeta na kutuogofya zaidi.

Ndugu zangu, tulishukuru Kanisa limetutengea mwezi mzima wa Novemba tulioishauanza ili tukitafakari kitendawili hiki cha kifo. Asiyetaka kukitafakari kifo anaonywa na methali ya kiswahili isemayo: “Asiyejua kufa na atazame kaburi.” Kwa hiyo tunaalikwa pia kwenda makaburi mara nyingi kuwaona wenzetu walioishapambana na kifo, nao watatusaidia kutafakari vizuri zaidi fumbo hilo la kifo.

Hebu tujaribu kutafakari kidogo na kupata jibu stahiki juu ya kifo na hatima ya maisha yetu. Tuanze utafiti wetu na Wayahudi, hasahasa manabii na wanazaburi. Wenzetu walianza utafiti mpya juu ya kifo wakitegemeza hoja zao juu ya kitu hiki “upendo”. Yaani kama Mungu aliingia katika mahusiano na binadamu na kufanya naye maagano iwe kwa njia ya manabii wa aina yoyote ile ni kwa sababu Mungu alimpenda binadamu na hivi akataka kuwa na mawasiliano naye. Ukimpenda mtu kwa dhati, huwezi ukamwacha tu kienyeji.

Hiyo ndiyo sheria ya upendo. Kwa hiyo ukisema: “Mungu ninakupenda”, naye akikuambia “Ninakupenda”, basi upendo huo hauwezi kwisha. Namna hii ya kufikiri, ina nguvu sana katika maisha. Katika Agano la kale, Mungu anawaambia wayahudi: “Wewe una thamani machoni pangu, nami ninakupenda” (Isaya). Hapo yaonesha wazi kuwa Mungu anao mradi wa kumpenda kiumbe chake kwa sababu amemwumba. Kwa hiyo katika Injili, tunaona kuwa katika mradi huo, Mungu amewekeza katika upendo kwa njia ya udalali ambao ni yeye mwenyewe katika nafsi ya pili ya Mungu, Yesu Kristu.

Injili ya leo imechukuliwa toka mazungumzo juu ya chakula cha uzima Ekaristi. Mradi huo wa Mungu umeanishwa kwa neno moja tu “Mapenzi”. Neno hilo limetamkwa na Yesu karibu mara nne: “sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu”; halafu, “bali niyafanye mapenzi yake aliyenipeleka”; halafu tena “Mapenzi yake aliyenipeleka ni haya”; na mwisho “Kwa kuwa mapenzi yake baba yangu ni haya”.

Hebu tumwangalie kwa undani Dalali aliyekabidhiwa kutekeleza mradi wa Mungu kwa wanadamu anasema: “Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe”. Hivi ndiyo Mungu anavyomwaminisha Yesu mradi huo wa mapendo kwa binadamu. Mungu anauaminisha ubinadamu wote kwa Yesu bila masherti. Kwa hiyo ili kuelewa maana ya kifo na ukombozi toka kifo, yabidi tuingie katika mradi huo wa mahusiano ya upendo (mapenzi) na Yesu.

Hoja ya msingi ya kuingia katika mahusiano hayo ni ile anayoisema Yesu mwenyewe, “Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka.” Hivi ni dhahiri kwamba Yesu amefika duniani kama dalali ili kutekeleza mradi wa Mungu, yaani kunadisha na kuendeleza mahusiano hayo ya upendo. Mungu amemdhamini Kristu mwanae mradi mzima wa upendo. Kama anavyothibitisha Yesu mwenyewe: “Mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho.” Hapo ndipo palipojaa uhondo! Maana yake bila Kristu, hatuwezi kupata jibu sahihi juu ya kifo, jibu linalookoa na kuelewa mwisho au hatima yetu. Na Yesu aliye mdhamini wa mradi huo hataki kujiangusha mwenyewe anaposema, “Katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho” anamaanisha kwamba atatuwapelekesha hao aliokabidhiwa hadi kieleweke.

Kufufuliwa siku ya mwisho, kadiri ya mwinjili Yohane haimaanishi mwisho wa dunia, bali ni Kalvario, juu ya msalaba siku ile anaposulibiwa na kufa. Tendo la mwisho la Yesu la upendo ni pale alipoitoa roho na maisha yake ya kimungu, nguvu ya upendo aliyoitolea yote kabisa wakati wa uhai wake na kuihitimisha pale msalabani. Siku hiyo ya mwisho anaitoa roho yake na maisha yale ya milele yanaingia kwenye mahusiano ya daima na Mungu, na maisha hayo hayana mwisho. Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu.

Mradi huo unatekelezeka tu endapo tutamtambua Mungu katika Kristu: “Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.”
Maana yake, upendo huo wa Baba utatekelezeka kwa namna tatu: kwanza kwa yule “amtazamaye Mwana,” kumbe yatubidi kuona au kutazama. Kuutazama au kuuona huu mradi wa Mungu na kumtambua Kristu ambaye ndiye mdhamini mkuu wa Mungu. Halafu yabidi “kumwamini Yesu”, yaani kutoa ushuhudi wa binafsi kwa huyo mdhamini pekee. Kisha matokeo ya kumtambua na kuishi kama alivyoishi huyo mdhamini yatakuwa ni “kufufuliwa naye”.

Kwa hiyo katika maisha yetu yatubidi tuyadhihirishe hayo mahusiano ya mapendo na Mungu kwa njia ya Kristu mdhamini wa mapendo. Kwa wale wenzetu walioishazaliwa kwa Baba, yaani waliofariki, wameutambua tayari uso wa Yesu na kumwaminia hivi sasa wamepokea maisha ya kimungu. Kwao hao sisi leo tunawapa ushirikiano kwa kuwa karibu sana nao, na siyo leo tu bali daima. Kama maisha yao hayakuwa makamilifu, sisi tuwaombee yaani kuwaonesha upendo, kwani Mungu amewekeza upendo katika Yesu Kristu.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR