Tuesday, October 30, 2012

BURIANI PADRE LELO MASSAWE

Mwili wa Mkuu wa Shirika la Wamissionari wa Consolata, nchini Tanzania, Padre Salutaris Lucas Massawe unazikwa leo katika Parokia ya Mshindo mkoani Iringa.
Padre Massawe, alikufa kwa kuzama baharini Oktoba 25 katika ufukwe wa Bagamoyo mkoani Pwani.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2XGJBri0B-ul7xK-dRrqUC7wXsI_b3ERAxdWi-BA1sS3cTlV8DwAIGm-I675DPPeUm3zJQtCElyiOZoh9G3oOmAjN1fnwP_5G5YAVj8zU2pSRz4ZAXdkO-AHH19jUAcP26H20fKTeBFk/s1600/P.+Lelo.jpg
Padre massawe na mapadre wenzake washirika la consolata kutoka mataifa mbali mbali barani afrika walikwenda Bagamoyo kupumzika baada ya mkutano wa wakuu wa Shirika la Waconsolata Barani Afrika, uliokuwa unafanyika consolata mission centre bunju,  Jiji la Dar es Salaam.
   
Septemba 7, 2011 alichaguliwa kuwa Mkuu wa Shirika la Waconsolata nchini Tanzania hadi alipokufa Oktoba 25, 2012.
Kabla ya kuwa mkuu wa shirika hilo, Padre Massawe alifanya kazi za umissionari katika nchi za Ethiopia na Italy.
HISTORIA YA MAREHEMU 
Marehemu Padre Salutaris Massawe alizaliwa tarehe 8 Julai 1962, katika kijiji cha kibosho wilaya ya moshi vijijini. 
Alisoma shule ya Msingi Singachini kuanzia mwaka 1971 hadi mwaka 1978 
mwaka 1979-1985 alikuwa akisoma katika  Sekondari Maua Seminari iliyoko mkoani kilimanjaro. 
 
Aliendelea na masomo ya Falsafa na Taalimungu kwenye Chuo cha Waconsolata kilichoko mjini Nairobi kuanzia mwaka 1985 hadi mwaka 1988.

Baada ya masomo na majiundo yake ya Kipadre, kunako tarehe 27 Juni 1993 alipewa daraja takatifu la Upadre katika kanisa la Kristo Mfalme na Askofu Amedeus Msarikie wa Jimbo la Moshi wakati huo. 

Mungu alimpa maisha ya duniani na sasa amemwita, ili ampe maisha ya mbiguni yasiyo na mwisho....
Raha ya milele umpe, ee bwana...
na mwanga wa milele umwangazie
apumzike kwa amani
amina,


 


9 comments:

  1. ASANTE KATIBU, NIPO NAFUATILIA MISA KUPITIA RADIO MARIA. INASIKITISHA, LAKINI HATUNA BUDI KUMUOMBEA DAIMA MPENDWA WETU. MUNGU AMWEKE MAHALI PEMA PEPONI. FRT. PAUL

    ReplyDelete
  2. Amina... FRT kwa mpande wetu sisi vijana tumepoteza padre amabaye alitupenda sana hakuna asiyejua kuwa CMC ilikuwa ni center yenye kutoa malezi ya vijana semina nyingi sana walituandalia TUTAMKUMBUKA MILELE

    ReplyDelete
  3. mungu amempenda zaidi ni masikitiko makubwa kwa vijana wote wa CMC haswa Mabolozi....Mungu aiweke mahala pema peponi.

    ReplyDelete
  4. honest me until now siamin kama PD.Massawe hatunae poleni sana wana CMC Mungu akipenda nitaenda siku moja Iringa Hata niione 2 nyumba yake ya milele

    ReplyDelete
  5. kristu alisema:"mimi ndimi ufufuo na uzima" twakuomba umuweke PD: wetu mpedwa massawe miongoni mwa watakatifu wako

    ReplyDelete
  6. Mungu amlaze mahali pema peponi. Amen, alikuwa nguzo ya shirika huyu jamaa....basi tena ndo MUNGU Ametaka.........Frank Mwombeki:

    ReplyDelete
  7. Mungu Ampuzishe kwa amani.

    ReplyDelete
  8. NAMWOMBEA KWA MUNGU APATE MAKAO YALE MUNGU ALIYOYAANDAA KWA WALE WATEULE WAKE kwani waitwao ni wengi lakini wateule ni wachache, naomba padre huyu awe kati ya wateule.

    ReplyDelete

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR