Tuesday, October 30, 2012

NAFASI NYINGINE TENA KWETU...

Vijana wasanii waalikwa kujiandikisha kwa ajili ya matamasha ya WYD 2013


Vijana kutoka pande zote za dunia , watakusanyika huo Rio de Janeiro kwa ajili ya kushiriki kaitka adhmisho la Siku ya Vijana a dunia , itakayo fanyika Julai mwakani. Vijana hayo si kwamba watakuwa mahujaji tu lakini pia iatkuw ni nafasi kwa vijana kuifahamisha dunia juu ya uwezo wao katika sanaa, tamasha za kuigiza , michezo, ngoma na muziki. Kwa ajili hiyo, hapo tarehe 15 Desemba 2012,wale wanaopenda kushirki wanaweza kuanza kujiandikisha. Uadikishaji huo umetengwa katika makundi matatu , Muziki, wachoraji wa sanaa na tamasha. Masharti ya kujiunga katiak vikundi hivyo yametolewa kwamba, wale wanao penda kushiriki katika tamasha la sanaa , utendaji wa onyesho lao ni lazima uonyeshe sura ya mafundisho ya kanisa na ubora wa sanaa. Na kwa wanamuziki , muziki huo ni lazima, uendane na mapokeo na mafundisho ya kanisa Katoliki, ingawa kila kikundi kitatenda na kuimba kwa mahadhi ya utamaduni wao. Na kwamba , baada ya makundi yote yanayotaka kushiriki kujiandisha, waandaaji wa WYD, watachagua vikundi vitakavyoshiriki katika matukio hayo na vitatangazwa March 13 2013. Nwa kwamba, Sherehe hizi za sanaa , hazitaingiliana na Katekesi zitakazo kuwa zikitolewa na matukio mengine yaliyoandaliwa rasmi kwa ajili ya WYD. Lengo la maonyesho ya kisanii, ni kuanzisha mazungumzano kati ya imani na tamaduni, na asili yake ni tangu mwaka 1997. Fomu za kujiandikisha zinapatikana katika tovuti ya CLICK HAPA http://www.rio2013.com/en

1 comment:

  1. Nipigo kubwa kwa vijana, kwakuondokewa na mpendwa wetu Patri Massawe, tutamkumbuka kwamengi mazuri aliyo tutendea kama vijana, hasa kwasemina mbalimbali na majitoleo yake ya semina mbalimbali Consolatha. Tuungane vijana weto tulipo kwakuya fanyia kazi mawazo yake ambayo bado yanaishi mioyoni mwetu. Kwama ombezi ya Mama Bikira Maria na Msimamizi wetu wa vijana Mt. Yoseph, alale pema peponi amina.

    ReplyDelete

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR