Monday, January 7, 2013

jumbe wa Baba Mtakatifu Benedikto XVI kwa Siku ya Vijana Duniani 2013

   Ujumbe wa Baba Mtakatifu Benedikto XVI kwa Siku ya Vijana Duniani 2013



Nendeni ulimwenguni kote mkayafanye mataifa yote kuwa ni wanafunzi wangu ndiyo kauli mbiu inayoongoza maadhimisho ya Siku ya 28 ya Vijana Duniani itakayoadhimishwa Rio de Janeiro, Brazil, mwezi Julai 2013. 

Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, anachukua fursa hii kuwaalika vijana kutoka sehemu mbali mbali za dunia kushiriki katika tukio hili muhimu katika maisha ya imani. Sanamu ya Kristo Mfalme inayopendezesha mji wa Rio de Janeiro, Brazil, ikiwa na mikono wazi, ni kielelezo cha mwaliko wa Kristo ambaye yuko tayari kuwapokea wote wanaomwendea na kwamba, moyo wake unaonesha upendo wa hali ya juu kabisa kwa kila kijana.

Huu ni mwaliko kwa vijana wenyewe kujiachilia mikononi mwa Kristo. Baba Mtakatifu anawaalika vijana kushirikisha mang’amuzi haya kwa vijana wenzao watakaoshiriki katika maadhimisho ya siku ya vijana duniani kwa mwaka 2013 nchini Brazil. Vijana wanapaswa kupokea na kuukumbatia upendo wa Kristo, ili waweze kuwa ni mashahidi wa upendo huu ambao unatakiwa kwa kiasi kikubwa ulimwenguni.

Baba Mtakatifu anasema kwamba, vijana wengi kutokana na kipaji chao cha kujitolea wamesaidia kwa namna ya pekee katika ujenzi wa Ufalme wa Mungu na maendeleo ya ulimwengu huu kwa njia ya kutangaza Habari Njemaya Wokovu. Ni watu wenye ari inayopata chimbuko lake kutoka katika Injili ya upendo wa Mungu unaojionesha kwa njia ya Kristo; walitumia nyenzo na vifaa mbali mbali vilivyokuwepo kwa wakati ule, pengine duni kuliko hali ilivyo kwa sasa.

Vijana wanaendelea kujiuliza umuhimu na maana ya maisha pamoja na hali ngumu wanayokabiliana nayo. Matatizo na changamoto wanazokumbana nazo katika hija ya maisha, vijana wanajiuliza ikiwa kweli wanaweza kufanya jambo lolote?

Mwanga wa Imani anasema Baba Mtakatifu unaondoa giza hili kwa kutambua kwamba, maisha ya binadamu ni jambo nyeti sana kwani ni matunda ya upendo wa Mungu. Mungu anawapenda wote hata wale ambao wamekengeuka na kupoteza imani yao. Mwenyezi mungu anaendelea kuwasubiri kwa utulivu. Ndiyo maana alimtoa Mwanaye wa pekee ili aweze kufa na kufufuka kutoka katika wafu ili kumkomboa mwanadamu kutoka katika utumwa wa dhambi.

Mama Kanisa anapoendelea kutekeleza dhamana na utume wake wa Uinjilishaji anawategemea vijana, kwani wao ni Wamissionari wa kwanza kabisa miongoni mwa vijana wenzao. Mara baada ya maadhimisho ya Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican, Papa Paulo wa sita, alitoa ujumbe kwa vijana ulimwenguni, akiwataka kujenga dunia bora zaidi, kuliko ilivyokuwa kwa wakati ule. Mwaliko huu bado ni endelevu hata leo hii, licha ya muda kuendelea kuyoyoma kwa kasi. Maendeleo ya sayansi na teknolojia yanawezesha mwingiliano wa vijana kutoka sehemu mbali mbali za dunia.

Utandawazi wa mwingiliano huu unaweza kuwa na mwelekeo chanya katika kukuza ubinadamu, ikiwa kama utasimikwa katika upendo wa dhati na badala ya kujikita katika vitu! Ni upendo tu, unaoweza kusheheni katika mioyo ya watu, kwa sababu Mungu ni upendo. Mwanadamu anapomsahau Mwenyezi Mungu, anapoteza tumaini na upendo kwa wengine. Ndiyo maana kuna haja ya kumshuhudia Mungu ili watu wengine waweze kuonja uwepo wake. Wokovu wa watu wote na kila mmoja unategemea kwa kiasi kikubwa upendo huu.

Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, katika ujumbe wake kwa maadhimisho ya Siku ya VIjana Duniani anawakumbusha kwamba, wito wa kimissionari ni muhimu sana kwa ajili ya hija ya imani, wanapotangaza Injili pamoja na kuwawezesha wao wenyewe kukua na kukomaa kikristo wakishikamana na Kristo. Hawataweza kuwa waamini ikiwa kama hawawezi kuinjilisha. Kuwa mmissionari maana yake ni kuwa kwanza kabisa mfuasi wa Kristo, kwa kumsikiliza kwa makini na hatimaye, kumfuasa.

Baba Mtakatifu anawaalika vijana kufanya tafakari ya kina kuhusu karama walizokirimiwa na Mwenyezi Mungu ili waweze kuzitumia kwa ajili ya jirani zao; wajifunze kusoma historia ya maisha ya kila mmoja wao na kuchuchumilia utajiri urithi mkubwa waliobahatika kuupata kutoka kwa vizazi vilivyopita, kwa kutambua kwamba, wanaunganishwa na umati mkubwa wa watu waliotangaza na kurithisha imani ambayo wanapaswa kuwamegea wengine. Kama Wamissionari wanapaswa kutambua Mapokeo ya Imani ya Kanisa. Vijana wanapaswa kutambua kile wanacho amini ili kuweza kukitangaza.

Yesu aliwatumwa mitume wake kwenda ulimwenguni kote ili kutangaza Habari Njema kwa kila kiumbe, yule atakayeamini na kubatizwa atapata uzima wa milele. Kuinjilisha maana yake ni kutangaza Habari Njema ya Wokobu ambayo ni Yesu Kristo mwenyewe. Kadiri watakavyomfahamu Kristo ndivyo watakavyokuwa na hamu ya kutaka kumtangaza zaidi na zaidi; kwa kumpenda na kuvutwa kwake ili kuwa naye karibu zaidi, kwani ana nguvu ya upendo inayoongoza utume wa kutangaza Injili. Roho wa Bwana anawataka kujitoa katika ubinafsi wao na kuwa tayari kwenda Kuinjilisha, daima wakijikita katika nguvu ya upendo wa Mungu, inayowabandua kutoka katika ubinafsi, ulimwengu, matatizo na mazoea yao binafsi.

Kristo mfufuka anasema Baba Mtakatifu, anawatuma Mitume wake kutolea ushuhuda wa uwepo wake unaoyakomboa mataifa, kwani Mwenyezi Mungu ni mwingi wa upendo na anataka kila mtu aweze kuokoka na kamwe asipotee! Vijana wanaalikwa kufungua macho yao ili kuona makando kando yao. Mataifa wanayoalikwa kuyatangazia Habari Njema si nchi nyingine duniani; bali ni kila sehemu ya maisha yao; kama vile familia, jumuiya mahali pa masomo na kazi; makundi ya marafiki zao na “vijiwe” wanapotumia muda wao wa ziada. Utangazaji wa Injili ya Kristo kwa njia ya furaha inamaanisha kugusa kila sehemu ya maisha.

Baba Mtakatifu anapenda kukazia kwa namna ya pekee, Uinjilishaji katika sekta ya mawasiliano ya jamii, hasa katika mtandao, unaotumiwa kwa kiasi kikubwa na vijana, wanaotekwa kwa urahisi zaidi na njia za mawasiliano ya jamii, ili kuweza kuwajibika katika kuuinjilisha ulimwengu wa mtandao.

Sehemu ya pili ni safari na uhamiaji, kwani vijana wengi wanasafiri kwa sababu mbali mbali kama vile masomo na kazi na wakati mwingine ni kwa ajili ya kujifurahisha. Lakini pia kuna mamillioni ya watu, wengi wao wakiwa ni vijana, wanaosafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine wakitafuta fedha au kutokana na sababu mbali mbali za kijamii. Hili linaweza kuwa ni jukwaa pia la kushirikishana Injili.

Baba Mtakatifu anawakumbusha vijana kwamba, kutangaza habari Njema ya Wokovu ni dhamana inayohusu maisha yao yanayogeuzwa kuwa ni alama za upendo, unaofanana na ule wa Kristo. Vijana wanapaswa kujiandaa vyema kama yule Msamaria mwema, kwa kuwa makini kwa watu wanaokutana nao, ili kuwasikiliza, kuwaelewa na kuwasaidia. Kwa njia hii wanaweza kuwaongoza watu wanaotafuta maana ya maisha kwenda nyumbani mwa Mungu, yaani Kanisa, mahali ambapo matumaini na wokovu ni makazi yake.

Kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo na Katekesi makini, wanaweza kuwafanya wengine kuwa ni wafuasi, kwa kuwaongoza wengine ili waweze kukutana na Yesu Kristo kwa njia ya Neno na Sakramenti zake. Kwa njia hii, wanaweza kumwamini na kupata fursa ya kuweza kumfahamu Mungu na hatimaye, kuishi katika neema yake. Baba Mtakatifu anawaalika vijana kumwomba Roho Mtakatifu ili aweze kuwasaidia; kuwaonesha njia ya kumfahamu na kumpenda Kristo kwa ukamilifu zaidi, wakijitahidi kuwa wagunduzi wanapotangaza Injili.

Baba Mtakatifu anawatia moyo vijana kamwe wasikate tamaa wanapojisikia kwamba ni dhaifu na wanyonge kiasi cha kushindwa kuinjilisha, wasikate tamaa, bali watambua kwamba, uinjilishaji si utume unaotegemea karama na uwezo wao. Wanapaswa kuwa waaminifu na watii ili kuitikia wito unaojikita katika nguvu ya Mungu. Vijana wanatakiwa kuyasimika maisha yao katika sala na maisha ya Kisakramenti, kwani uinjilishaji wa kweli ni matunda ya sala na unaenziwa pia kwa sala.

Vijana wajifunze kuzungumza na Mungu ili hatimaye, waweze kuzungumza kuhusu Mungu. Maisha ya imani ya vijana yapate chimbuko lake katika maadhimisho ya Fumbo la Ekaristi Takatifu, pamoja na kujitahidi kupokea Sakramenti ya Upatanisho mara kwa mara. Kwa wale ambao bado hawajaimarishwa kwa Sakramenti ya Kipaimara, waongeze juhudi ya kuipokea sakramenti hii, kwani kama ilivyo pia Sakramenti ya Ekaristi Takatifu ni Sakramenti za utume, kwani zinawakirimia nguvu na mapendo ya Roho Mtakatifu ili kuweza kuungama imani. Vijana wanaalikwa kushiriki kikamilifu katika Ibada ya Kuabudu Ekaristi Takatifu.

Ikiwa kama vijana watafuata njia hii kwa ukamilifu, Yesu mwenyewe atawawezesha kuwa waaminifu kwa Neno ili waweze kutolea ushuhuda amini na wenye nguvu kwake Yeye. Wakati mwingine watajaribiwa ili kuonesha udumifu, pale neno la Mungu linapokatiliwa au kukumbana na upinzani. Baba Mtakatifu anatambua mateso na dhuluma ambayo baadhi ya vijana wanakabiliana nazo sehemu mbali mbali za dunia kiasi kwamba, hawawezi hata kidogo kutolea ushuhuda wa imani yao kwa Kristo na Kanisa lake kutokana na ukosefu wa uhuru wa kidini. Kuna baadhi yao ambao tayari wamekwisha yamimina maisha yao kwa sababu tu ni Wakristo. Baba Mtakatifu anawataka vijana kuwa imara katika imani yao, daima wakitambua kwamba, Yesu Kristo yuko pamoja nao katika kila jaribu la maisha.

Vijana wanalihitaji Kanisa ili kuweza kuwa imara katika imani yao ya Kikristo. Hakuna mtu anayeweza kutolea ushuhuda wa Injili peke yake, kwani Yesu aliwatuma wafuasi wake kwa pamoja. Hivyo, ushuhuda wa imani daima unatolewa ba Jumuiya ya Kikristo na utume wao unaweza kuzaa matunda kwa njia ya umoja unaomwilishwa ndani ya Kanisa. Ni kwa njia ya umoja na upendo kwa jirani, wengine wanaweza kuwatambua kwamba, wao ni wafuasi wa Kristo.

Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, katika ujumbe wake kwa maadhimisho ya siku ya vijana duniani kwa mwaka 2013 anawaalika vijana kusikiliza kutoka katika undani wa mioyo yao sauti ya Yesu inayowaita kutangaza Injili. Kama sanamu ya Yesu Kristo Mfalme inavyoonesha pale Rio de Janeiro, ni moyo ambao umefunguka kwa upendo kwa kila mtu na mikono yake iko wazi kuwafikia watu wote. Ni changamoto kwa vijana wenyewe kuwa ni moyo na mikono ya Yesu, kwa kutolea ushuhuda wa upendo huu sanjari na kuwa ni wamissionari kwa vijana wa kizazi kipya, wanaowajibishwa na upendo ambao uko wazi kwa wote.

Baba Mtakatifu anahitimisha ujumbe wake kwa kusema kwamba, mwaliko anaoutoka kwa vijana ni kwa ajili ya dunia nzima, lakini zaidi kwa vijana wanaoishi Amerika ya Kusini. Katika maadhimisho ya mkutano wa tano wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Amerika ya Kusini, uliofanyika mjini Aparecida kunako mwaka 2007, Maaskofu walizindua kampeni ya utume Barani humo. Vijana wanaunda idadi kubwa ya wananchi wa Amerika ya Kusini. Hawa ni rasilimali muhimu sana kwa Kanisa na Jamii, changamoto ya kutangaza kwa ari zaidi imani kwa vijana wenzao kutoka sehemu mbali mbali za dunia.



MWaka WA IMANI

Tarehe 12/01/2013 Dekania Ya Gasper watakabidhiwa Msalaba wa Imani..tayari kwa kuupitisha kila Parokia...Na utaanzia kwenye Parokia ya Mwenye heri Isidori Bakanja Boko ambapo utafika siku hiyo ya Jumamosi saa nane mchana ukitokea Pugu.
 Hivyo waamini wote wa Parokia ya Boko tujitokeze kwa wingi hiyo siku kuupokea huo Msalaba ambao utapita katika Jumuiya zote na wale wenye Bibilia na Katekisimu ya Kanisa Katoliki zitabarikiwa.CLICK hapa kusoma zaidi kuhusu mwaka wa IMANI

Wednesday, November 7, 2012

PICHA ZA OBAMA AKIWA VATICAN





Hizo picha ni za Obama alipotembelea Vatican, hayo magali mawili ni magali ambayo kampuni ya ya magali ya Renault ilimzawadia Pope kwa matumizi yake. Ni magali ambayo ayatumii mafuta bali umeme, kwahiyo ni kucharge we na moto wako.....

Obama re-elected


CHICAGO (Reuters) - U.S. President Barack Obama won re-election on Tuesday, defeating Republican challenger Mitt Romney.

Following are Obama's remarks early on Wednesday to thousands of supporters at a convention centre in Chicago, the president's hometown.

Thank you. Thank you. Thank you so much. Tonight, more than 200 years after a former colony won the right to determine its own destiny, the task of perfecting our union moves forward. It moves forward because of you. It moves forward because you reaffirmed the spirit that has triumphed over war and depression, the spirit that has lifted this country from the depths of despair to the great heights of hope, the belief that while each of us will pursue our own individual dreams, we are an American family and we rise or fall together as one nation and as one people.
(APPLAUSE)
Tonight, in this election, you, the American people, reminded us that while our road has been hard, while our journey has been long, we have picked ourselves up, we have fought our way back, and we know in our hearts that for the United States of America the best is yet to come. I want to thank every American who participated in this election...
(APPLAUSE)
... whether you voted for the very first time or waited in line for a very long time.
(APPLAUSE)
By the way, we have to fix that.
(APPLAUSE)
Whether you pounded the pavement or picked up the phone...
(APPLAUSE)
... whether you held an Obama sign or a Romney sign, you made your voice heard and you made a difference. I just spoke with Governor Romney and I congratulated him and Paul Ryan on a hard-fought campaign.
(APPLAUSE)
We may have battled fiercely, but it's only because we love this country deeply and we care so strongly about its future. From George to Lenore to their son Mitt, the Romney family has chosen to give back to America through public service and that is the legacy that we honour and applaud tonight.
(APPLAUSE)
In the weeks ahead, I also look forward to sitting down with Governor Romney to talk about where we can work together to move this country forward.
(APPLAUSE)
I want to thank my friend and partner of the last four years, America's happy warrior, the best vice president anybody could ever hope for, Joe Biden. And I wouldn't be the man I am today without the woman who agreed to marry me 20 years ago.
(APPLAUSE)
Let me say this publicly: Michelle, I have never loved you more. I have never been prouder to watch the rest of America fall in love with you, too, as our nation's first lady.
(APPLAUSE)
Sasha and Malia, before our very eyes you're going up to become two strong, smart beautiful young women, just like your mom. And I'm so proud of you guys. But I will say that for now one dog's probably enough.
(LAUGHTER)
To the best campaign team and volunteers in the history of politics...
(APPLAUSE)
The best. The best ever. Some of you were new this time around, and some of you have been at my side since the very beginning.
(APPLAUSE)
But all of you are family. No matter what you do or where you go from here, you will carry the memory of the history we made together and you will have the life-long appreciation of a grateful president. Thank you for believing all the way, through every hill, through every valley.
(APPLAUSE)
You lifted me up the whole way and I will always be grateful for everything that you've done and all the incredible work that you put in.
(APPLAUSE)
I know that political campaigns can sometimes seem small, even silly. And that provides plenty of fodder for the cynics that tell us that politics is nothing more than a contest of egos or the domain of special interests. But if you ever get the chance to talk to folks who turned out at our rallies and crowded along a rope line in a high school gym, or saw folks working late in a campaign office in some tiny county far away from home, you'll discover something else. You'll hear the determination in the voice of a young field organizer who's working his way through college and wants to make sure every child has that same opportunity.
(APPLAUSE)
You'll hear the pride in the voice of a volunteer who's going door to door because her brother was finally hired when the local auto plant added another shift.
(APPLAUSE)
You'll hear the deep patriotism in the voice of a military spouse whose working the phones late at night to make sure that no one who fights for this country ever has to fight for a job or a roof over their head when they come home.
(APPLAUSE)
That's why we do this. That's what politics can be. That's why elections matter. It's not small, it's big. It's important. Democracy in a nation of 300 million can be noisy and messy and complicated. We have our own opinions. Each of us has deeply held beliefs. And when we go through tough times, when we make big decisions as a country, it necessarily stirs passions, stirs up controversy. That won't change after tonight, and it shouldn't. These arguments we have are a mark of our liberty. We can never forget that as we speak people in distant nations are risking their lives right now just for a chance to argue about the issues that matter, the chance to cast their ballots like we did today.
(APPLAUSE)
But despite all our differences, most of us share certain hopes for America's future. We want our kids to grow up in a country where they have access to the best schools and the best teachers.
(APPLAUSE)
A country that lives up to its legacy as the global leader in technology and discovery and innovation, with all the good jobs and new businesses that follow. We want our children to live in an America that isn't burdened by debt, that isn't weakened by inequality, that isn't threatened by the destructive power of a warming planet.
(APPLAUSE)
We want to pass on a country that's safe and respected and admired around the world, a nation that is defended by the strongest military on earth and the best troops this - this world has ever known.
(APPLAUSE)
But also a country that moves with confidence beyond this time of war, to shape a peace that is built on the promise of freedom and dignity for every human being. We believe in a generous America, in a compassionate America, in a tolerant America, open to the dreams of an immigrant's daughter who studies in our schools and pledges to our flag.
(APPLAUSE)
To the young boy on the south side of Chicago who sees a life beyond the nearest street corner.
(APPLAUSE)
To the furniture worker's child in North Carolina who wants to become a doctor or a scientist, an engineer or an entrepreneur, a diplomat or even a president - that's the future we hope for. That's the vision we share. That's where we need to go: forward.
(APPLAUSE)
That's where we need to go. Now, we will disagree, sometimes fiercely, about how to get there. As it has for more than two centuries, progress will come in fits and starts. It's not always a straight line. It's not always a smooth path. By itself, the recognition that we have common hopes and dreams won't end all the gridlock or solve all our problems or substitute for the painstaking work of building consensus and making the difficult compromises needed to move this country forward. But that common bond is where we must begin. Our economy is recovering. A decade of war is ending. A long campaign is now over.
(APPLAUSE)
And whether I earned your vote or not, I have listened to you, I have learned from you, and you've made me a better president. And with your stories and your struggles, I return to the White House more determined and more inspired than ever about the work there is to do and the future that lies ahead.
(APPLAUSE)
Tonight you voted for action, not politics as usual.
(APPLAUSE)
You elected us to focus on your jobs, not ours. And in the coming weeks and months, I am looking forward to reaching out and working with leaders of both parties to meet the challenges we can only solve together: reducing our deficit, reforming our tax code, fixing our immigration system, freeing ourselves from foreign oil. We've got more work to do.
(APPLAUSE)
OBAMA: But that doesn't mean your work is done. The role of citizen in our democracy does not end with your vote. America's never been about what can be done for us. It's about what can be done by us together through the hard and frustrating, but necessary work of self- government. That's the principle we were founded on.
(APPLAUSE)
This country has more wealth than any nation, but that's not what makes us rich. We have the most powerful military in history, but that's not what makes us strong. Our university, our culture are all the envy of the world, but that's not what keeps the world coming to our shores. What makes America exceptional are the bonds that hold together the most diverse nation on Earth. The belief that our destiny is shared, that this country only works when we accept certain obligations to one another and to future generations. The freedom which so many Americans have fought for and died for come with responsibilities as well as rights. And among those are love and charity and duty and patriotism. That's what makes America great.
(APPLAUSE)
I am hopeful tonight because I've seen the spirit at work in America. I've seen it in the family business whose owners would rather cut their own pay than lay off their neighbours, and in the workers who would rather cut back their hours than see a friend lose a job. I've seen it in the soldiers who reenlist after losing a limb and in those SEALs who charged up the stairs into darkness and danger because they knew there was a buddy behind them watching their back.
(APPLAUSE)
I've seen it on the shores of New Jersey and New York, where leaders from every party and level of government have swept aside their differences to help a community rebuild from the wreckage of a terrible storm.
(APPLAUSE)
And I saw just the other day, in Mentor, Ohio, where a father told the story of his 8-year-old daughter, whose long battle with leukaemia nearly cost their family everything had it not been for health care reform passing just a few months before the insurance company was about to stop paying for her care.
(APPLAUSE)
I had an opportunity to not just talk to the father, but meet this incredible daughter of his. And when he spoke to the crowd listening to that father's story, every parent in that room had tears in their eyes, because we knew that little girl could be our own. And I know that every American wants her future to be just as bright. That's who we are. That's the country I'm so proud to lead as your president.
(APPLAUSE)
And tonight, despite all the hardship we've been through, despite all the frustrations of Washington, I've never been more hopeful about our future.
(APPLAUSE)
I have never been more hopeful about America. And I ask you to sustain that hope. I'm not talking about blind optimism, the kind of hope that just ignores the enormity of the tasks ahead or the roadblocks that stand in our path. I'm not talking about the wishful idealism that allows us to just sit on the sidelines or shirk from a fight. I have always believed that hope is that stubborn thing inside us that insists, despite all the evidence to the contrary, that something better awaits us so long as we have the courage to keep reaching, to keep working, to keep fighting.
(APPLAUSE)
America, I believe we can build on the progress we've made and continue to fight for new jobs and new opportunity and new security for the middle class. I believe we can keep the promise of our founders, the idea that if you're willing to work hard, it doesn't matter who you are or where you come from or what you look like or where you love. It doesn't matter whether you're black or white or Hispanic or Asian or Native American or young or old or rich or poor, able, disabled, you can make it here in America if you're willing to try.
(APPLAUSE)
I believe we can seize this future together because we are not as divided as our politics suggests. We're not as cynical as the pundits believe. We are greater than the sum of our individual ambitions, and we remain more than a collection of red states and blue states. We are and forever will be the United States of America.
(APPLAUSE)
And together with your help and God's grace we will continue our journey forward and remind the world just why it is that we live in the greatest nation on Earth. Thank you, America. God bless you. God bless these United States.
(Editing by Will Dunham)

Tafakari Nasi.....


Vijana Wakatoliki inatubidi tuisha kwa tafakari na mifano ya watakatifu wakubwa kama vile  Francis wa Assisi ambao Mungu
aliwatukuza kutokana na bidii yao ya kuwahubiria wakristo ili waishi vema ujumbe wa Injili.
 “Tuirejee Injili, la sivyo Kristo hataishi miongoni mwetu”  Kuirejea Injili ni
kumkubali Yesu wa  Nazareti kufanya makao mwetu kwa kuishi maisha ya umaskini wa roho,
kujitoa kwa wote huku tukijiweka katika daraja ya chini, kujitolea kwa ajili ya wenzetu, n.k.
Kama ilivyosalamu yetu..ya mapendo..,kijana akijawa na mapendo ya dhati kwa Yesu, alijitoa kikamilifu kuishi Injili, basi yeye atakuwa ni kijana wamfano na kuwarekibisha wengine,
Kurejea kwenye Injili ni jambo la msingi kwa maisha ya kikristo, kadhalika kuna mambo ambayo
nayo ni muhimu sana katika dunia yetu ya leo.

Je Ujana wako unauishi kwa  kukosa imani. ni  dhahiri kuwa wapo vijana wengi waliopoteza imana na mwelekeo wa maisha, je mkiwa kama Kijana Mkatoliki umeyakabidhi maisha yako kwa huyu Yesu wa Nazaerti? 
Maisha yetu yote  ni ya hangaiko kwa ajili ya Yesu wa Nazareti. hapo ndipo utaweza
kutambua mapenzi ya Mungu kupitia matukio mbalimbali. Katika ulimwengu huu wenye
kubadilika kwa kasi, Kijana mkatoliki unaweza kusaidia katika kukabiliana na mabadiliko haya ili
kukidhi mahitaji yetu ya kiimani.

Jiulize Maswali yafuatayo kisha tuandikie comment yako unaweza pia kutuandika katika E mail yetu viwawaboko@yahoo.com

1) Je nimeweza kubaini nini kutokana na tafakari yangu juu ya maisha ya Utume

2) Ni nini hasa ambacho naweza kuiga ambacho kinaendana kabisa na maisha yangu,
  uhusiano wangu na Mungu na wa watu wengine?
3)Ni kwa namna gani maisha na ujumbe wa Watakatifu unatusaidia  vilivyo kumfuasa
Kristo?

4)Napata ujumbe gani? Huo ujumbe nitauishi vipi katika maisha yangu ya kila siku?

“Endapo punje ya ngano haitadondoka ardhini na kufa, haitazaa, lakini ikifa, huzaa sana
                                     matunda” Yn. 12: 24

Bwana, Anatufundisha ,Nasisi Tusali.......


Zipo Silaha mbalimbali za Kiroho alizovaa Yohane Mbatizaji nazo ni Sala,.. kufunga na sadaka. Kwa leo tutafakari silaha ya kwanza: Ambayo ni
                                             ................SALA.....
 Tumeitwa na Kirsto. Tumeitika wito wake. Hivyo, tunafanya kazi yake. Yeye alikuwa mtu wa sala. Aliwafundisha watu namna ya kusali kwa mafundisho yake na tendo halisi la kusali. Sisi kama wafuasi wake na tulioitika mwito wake wa kuwa viongozi wa taifa lake, tuige mfano wake. Katika tafakari hiyo, tusaidiwe na Yesu wa Mwinjili Luka.... Mwinjil Luka, anatilia mkazo mkubwa katika umuhimu wa sala. Kwa yakini, umuhimu huo unaonekana bayana. Kwanza jinsi Yesu aliivyosali mara nyingi. Pili, alivyowahimiza watu wasali. Tatu, jinsi alivyota mifano bora ya kusali.

Injili ya Luka inaonesha dhahiri kuwa kabla ya kuchukua hatua kubwa na muhimu, yesu anaanza kwa sala. Tuzitazame fasuli zifuatazo:


l1. Ubatizo wa Yesu (Lk 3:21-22)
Katika nafasi ya kubatizwa kwa Yesu, Luka anasema kuwa watu wote walipokuwa wamebatizwa, naye Yesu alibatizwa. Na alipokuwa anasali, mbingu zilifunguka, na Roho Mtakatifu alimshukia akiwa katika umbo la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ndiwe Mwanangu, nimependezwa nawe".
Hatua hiyo ya kubatizwa ilikuwa ya maana sana. yesu alithibitishwa kuwa Mwana tena mpenzi wa Mungu. Alijiunga na foleni ya wadhambi ili apokee ubatizo wa toba, toba iletaya ondoleo la dhambi. Lakini yeye hakuwa na dhambi. Alihakikishiwa kuwa njia aliyochukua yaani utume wake ilikuwa sahihi, na kwa kweli yalikuwa mapenzi ya Mungu.

l2. Yesu anawateua mitume kumi na wawili (Lk 6:12-16).
Tendo lilitanguliwa na sala. Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akisali. Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, miongoni mwao akawachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume. Alijitenga na watu ili awe karibu na Mungu baba yake. Kwa hiyo, uteuzi wa mitume uliongozwa na Baba. Hatua hiyo ilibeba umuhimu mkubwa sana - kuwateua viongozi wanaofaa. tunasoma pia uteuzi wa mitume ukitanguliwa na sala katika Mdo 13:1-3. Katika kanisa la Antiokia kulikuwepo na watu wengine waliokuwa manabii na walimu. Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: :Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia." Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawekea mikono, wakawaacha waende zao.
l3. Petro anamkiri Yesu Kristo (Lk 9:!8-20) Yesu alikuwa akisali peke yake na wanafunzi wake walikuwa karibu kabla hajaanza kuwauliza: :Eti, watu wanasema mimi ni nani?" Baada ya kutoa majibu mbali mbali, Yesu anawauliza wanafunzi wenyewe: "Ninyi je, mwasema mimi ni nani?" Petro kwa niaba ya wanafunzi wenzake alitoa jibu sahihi: "Wewe ndiwe kristo wa Mungu." Hiyo ilikuwa hatua kubwa, yaani azma ya Yesu kujua kama watu na wanafunzi wake wanamfahamu: Yeye ni nani na utume wake ni upi. Kumfahamu ni sharti muhimu ili utume wake uzae matunda.

Friday, November 2, 2012

LEO NI SIKU YA MAREHEMU WOTE DUNIANI....TUWAOMBEE!

                             MAKABURI YA CHINI YA ARDHI.

                                       MAKABURI YA CHINI YA ARDHI.
ANGALIA MAKABURI YA WENZETU YA NDANI, KATIKA VIMBA VIMBA!
















Leo ni siku ya marehemu wote duniani, kila ifikapo tarehe 02/11 tunawakumbuka wapendwa wetu wote waliotutangulia mbele ya haki. Kwa namna ya pekee nimepata nafasi ya kutembelea makaburi ya hapa Cesena leo mchana huu, ambapo nimeenda kusali na kuwatembelea marafiki ambao tayari walishatutangulia mbele ya haki. Ili kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu apende kuwaweka miongoni mwa wateule wake mbinguni, na kama bado wanayo mapungufu ya dhambi zao basi waweze kutakaswa, ili hatimaye waonje pendo na huruma ya Mungu.
  
   Ibada za kuwaombea marehemu zinafanyika katika kila Parokia.....na katika maeneo ya makaburi......

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR