Wednesday, January 28, 2015

UJUMBE WA KWARESIMA MWAKA HUU 2015: IMARISHENI MIOYO YENU!

Kanisa litakianza kipindi cha Kwaresima hapo tarehe 18 Februari 2015 kwa kupakwa majivu, mwaliko wa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa kipindi cha Kwaresima kwa mwaka 2015 unaongozwa na kauli mbiu "Imarisheni mioyo yenu" kwa kutambua kwamba, kila mtu anapendwa na Mwenyezi Mungu na anamfahamu kila mtu kwa jina na hata pale mwanadamu anapokengeuka, Mungu bado anamtafuta.

Dhamana na nafasi ya Baba kwenye Familia

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 28 Januari 2015 ameendelea na Katekesi yake kuhusu Familia, kwa kuangalia: utu, dhamana na nafasi ya Baba wa familia, jina ambalo Wakristo wamefundishwa na Yesu mwenyewe kumwita Mwenyezi Mungu; jina lenye utajiri mkubwa wa mahusiano katika jamii.

Monday, January 26, 2015

Mazishi ya Padre Anthony Chonya Tosa Maganga iringa leo

Marehemu Padre Anthony Chonya, alikuwa Padre wa Jimbo la Iringa, Mzaliwa wa Parokia ya Malangali na Parokia yake ya mwisho kuitumikia ni Parokia ya Magungu Mgololo.


Saturday, January 24, 2015

MASOMO YA TAREHE 25/01/2015 jumapili ya 3 ya mwaka B wa kanisa

25

Januari

 Jumapili: Dominika ya 3 ya Mwaka "B".
SOMO  1. Yon. 3:1-5, 10

 Neno la bwana likamjia Yona mara ya pili, kusema, ondoka uende Ninawi, mji ule mkubwa, ukaihubiri habari nitakayo kuamuru. Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikua mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu, Yona akaanza kuingia mjini mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini ninawi utaangamizwa. Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo. Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.

Walei na Kanisa letu

Tumsifu Yesu Kristo. Kwa mara nyingine tena tunakukaribisha katika mada hii ya utume wa walei, ili tuisikie sauti ya Mama Kanisa anayetuelekeza nini cha kufanya ili Kanisa lizidi kuwa hai na Injili ya Kristo isonge mbele kwa ajili ya wokovu wa ulimwengu.

Thursday, January 22, 2015

18

 Januari
 Jumapili: Dominika ya 2 ya Mwaka "B".
SOMO  1. 1 Sam. 3:3b-10, 19

 Samueli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu; basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, mimi hapa. Akamwendea Eli kwa haraka, akasema mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena. Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, sikukuita, mwanangu; kalale tena. Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akamtambua ya kuwa Bwana ndiye alimwita yule mtoto. Kwa hiyo Eli akamwambia Samweli, enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena Bwana; Samweli akaenda akalala mahali pake. Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Samweli akakua, naye Bwana alikuwa pamoja naye, wala hakuliacha neno lake lo lote lianguke chini.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR