Monday, February 2, 2015

Mwaka watawa wafunguliwa rasmi Jimbo kuu la Dar es salam

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania linafungua rasmi Maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani, uliotangazwa na Baba Mtakatifu Francisko, tarehe 2 Februari 2015, Siku kuu ya kutolewa Bwana Hekaluni, sanjari na maadhimisho ya siku ya kumi na tisa ya watawa duniani, iliyoanzishwa na Mtakatifu Yohane Paulo II. Maadhimisho haya yanafanyika katika ngazi ya Kijimbo na katika baadhi ya Majimbo makuu.  
Hayo yamesemwa na Askofu Renatus Nkwande, Mwenyekiti wa Tume ya Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mahojiano maalum na Radio Vatican. Kwa namna ya pekee anasema, Watawa wanapaswa kuwa ni mashuhuda wa imani dhidi ya ukanimungu, kwa kujikita katika maongozi ya Mungu, Injili ya Kristo na Mashauri ya Kiinjili.

Mons. Liberatus Sangu ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, Tanzania!

Baba Mtakatifu Francisko amemteua Monsinyo Liberatus Sangu kutoka Jimbo Katoliki la Sumbawanga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Tanzania. Kabla ya uteuzi wake, Askofu mteule Sangu alikuwa ni Afisa mwandamizi katika Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu mjini Vatican.

Sunday, February 1, 2015

Tafakari ya Jumapili ya 4 ya Masomo ya Mwaka B tarehe 01/02/2015

Mwandishi wa kitabu cha Kumbukumbu la Torati ambamo tunapata somo la kwanza
anatualika kutambua kuwa Mungu haachi kutimiza ahadi yake ya kale kwamba atamtuma Nabii atakayetangaza hukumu zake kwa haki, atakayesema yale ya Bwana na kama atasema kinyume atakufa. Manabii wengi walitangaza ujumbe wa Mungu lakini hasa katika zama zetu Mungu anasema nasi kwa njia ya Masiha kama ambavyo Wayahudi walielewa ujumbe huo wa Neno la Mungu.

Masomo ya Tarehe 01/02/2015, Jumapili: Dominika ya 4 ya Mwaka "B".

01

February

 Jumapili: Dominika ya 4 ya Mwaka "B".
SOMO  1. Kumb. 18:15-20

 Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye. Kama vile ulivyotaka kwa Bwana, Mungu wako, huko horebu, siku ya kusanyiko, ukisema, nisisikie tena sauti ya Bwana, Mungu wangu, wala nisiuone tena moto huo mkubwa, nisije nikafa. Bwana akaniambia, wametenda vyema kusema walivyosema . Mimi nitawaondoshea Nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru. Hata itakuwa, mtu asiyesikiliza maneno yangu atakayosema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake. Lakini Nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.

Wednesday, January 28, 2015

UJUMBE WA KWARESIMA MWAKA HUU 2015: IMARISHENI MIOYO YENU!

Kanisa litakianza kipindi cha Kwaresima hapo tarehe 18 Februari 2015 kwa kupakwa majivu, mwaliko wa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa kipindi cha Kwaresima kwa mwaka 2015 unaongozwa na kauli mbiu "Imarisheni mioyo yenu" kwa kutambua kwamba, kila mtu anapendwa na Mwenyezi Mungu na anamfahamu kila mtu kwa jina na hata pale mwanadamu anapokengeuka, Mungu bado anamtafuta.

Dhamana na nafasi ya Baba kwenye Familia

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 28 Januari 2015 ameendelea na Katekesi yake kuhusu Familia, kwa kuangalia: utu, dhamana na nafasi ya Baba wa familia, jina ambalo Wakristo wamefundishwa na Yesu mwenyewe kumwita Mwenyezi Mungu; jina lenye utajiri mkubwa wa mahusiano katika jamii.

Monday, January 26, 2015

Mazishi ya Padre Anthony Chonya Tosa Maganga iringa leo

Marehemu Padre Anthony Chonya, alikuwa Padre wa Jimbo la Iringa, Mzaliwa wa Parokia ya Malangali na Parokia yake ya mwisho kuitumikia ni Parokia ya Magungu Mgololo.


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR